Juzi nilikaa tangu saa 6 usiku hadi karibia saa 11 alfajiri lakini hakuna kilichendelea zaidi ya kuniambia kuwa in progress, yaani tafsiri yangu ni kuwa entity return niliyofile inaendelea kuwa processed.
Jana mchana kutwa hivyo hivyo. Usiku wa kuamkia leo nimenza saa 9 usiku hadi saa 10 nikaona hakuna mabadiliko yoyote.
Hadi sasa ni vile vile, tena leo ni mbaya zaidi mara sijui 504 Gateway time-out nk.
Ni kama hawakuwa wamejiandaa kwa mzigo mkubwa hivi (server yao ina capacity ndogo). Maana ebu fikiria enities zote Tanzania zenye wafanyakazi wanaokatwa PAYE, katika muda wa siku saba wawe wamefile return zao, ziwe processed, ziwe assessed na wapate control number kwa ajili ya malipo!
Si hivyo tu kuna na SDL return nk. Hii ni volume kubwa sana ndani ya muda mfupi.
Nashauri uwezo wa server uongezwe na muda wa kufile returns uongezwe, na waongeze links mbalimbali. Nakumbuka wakati wa matokeo ya NECTA mambo yalikuwa hivi hivi lakini walipoweka links nyingi kazi ikawa rahisi - waulizeni hao walifanyaje?
Mimi nimekata tamaa, kama ni faini basi wapige tu maana nimechoka kukesha. Zile namba zao za contact centerToll free za 0800750075 na 0800780078 wala usijaribu maana utasikia wimbo uleule hadi chaji ya simu inaisha