kumaro tafadhali fafanua aina ya jengo kama ifuatavyo;
1. Jengo la aina gani
a) makazi
b) biashara
c)shule
d) hospitali nk
2. Jengo la kawaida au ghorofa
3. Litajengwa wapi yaani;
a) mji mdogo
b) manispaa
c) jiji
Lengo langu nikushauri, Watanzania wengi hamzingatii ushauri wa kitaalam kabla ya kupata hasara.
Ili upate kibali cha kujenga hasa mijini unatakiwa kuwa na;
a) ramani iliyogongwa muhuri na architect aliyesajiliwa na AQRB
b) uwe na BOQ iliyotengenezwa na kugongwa muhuri na Qs aliyesajiliwa na AQRB.
Ndipo hatua zingine zifuate. Ikiwa unahitaji ushauri wa bure nicheki.
Epuka kugongewa muhuri na asiyesajiliwa hata kama ni bure itakula kwako