nahitaji mbao 4x2,na 6x2,treated kwa bei ya jumla

Parachichi

JF-Expert Member
Jul 22, 2008
510
102
Wakuu heshima zenu,nataka kufungua duka la ujenzi hivi karibuni,nilikua nataka hizo mbao tajwa hapo juu kwa jumla,kwa yeyote anayefanya hii business ani pm tufanye business!dalal hatakiw manake nafahamu bei ya soko.nawasilisha wakuunipo dar wandugu
 
Nenda Pale Mbeya Cement MBELE YA KITUO CHA DALADALA KUNA KIJANA PALE ANAZO.
 
Mkuu bila dalali hupati mzigo Dar. Shamba (sao hill) zinauzwa cubic meter moja Tsh. laki nne, jijini zinauzwa kati ta Tsh. laki 5 na 20 mpaka 30.

wauzaji wa leja leja 2 by 6 wanapima futi moja tsh 1200
 
Mkuu kwa hiyo nikiwasiliana na Sao Hill je siwezi kupata mzigo hapa dar?naonaga yale malory yanashusha mzigo mitaa ya mwenge,nadhani wale ni wafanya biashara wanaufuata huo mzigo huko Iringa wanakuja kuuza huku dar,ndio nilikua nataka niwapate wale!manake madalali wanawezxa kukuuzia mzigo faida yote keshachukua!

Nawasilisha mkuu
 
mkuu nashukuru nimeona kwenye website ya sao mill industries ngoja nipate mawili matatu kwanza
 
Mkuu kwa hiyo nikiwasiliana na Sao Hill je siwezi kupata mzigo hapa dar?naonaga yale malory yanashusha mzigo mitaa ya mwenge,nadhani wale ni wafanya biashara wanaufuata huo mzigo huko Iringa wanakuja kuuza huku dar,ndio nilikua nataka niwapate wale!manake madalali wanawezxa kukuuzia mzigo faida yote keshachukua!

Nawasilisha mkuu

Unazungumzia Mwenge upande wa kushoto baada ya mataa ukiwa kama unaelekea Ubungo?? kwani zile mbao zinazoshushwaga pale mwenge ni mbao ambazo ni "treated"?? C ni mbao za kawaida tu zile??
Tumia madalali, kwa makubaliano maalum, ishu yako ifanyike fasta uokoe rasilimali muda, otherwise wasiliana na Sao Hill wenyewe...
 
Back
Top Bottom