Nahitaji kunyonya majitaka shimo limejaa. Nipo Dar

Nahitaji kunyonya majitaka shimo limejaa. Nipo Dar

Nlijuwa kifuru kuna mfumo wa maji taka kwenye nyumba zenu huko
Kumbe bado mnatumia mashimo ya choo

Ova
Hivi ni maeneo gani hapa town kuna huo mfumo?
Si ule pipes zinaunganishwa nyumba kwa nyumba halafu bomba moja inabeba?
 
Hivi ni maeneo gani hapa town kuna huo mfumo?
Si ule pipes zinaunganishwa nyumba kwa nyumba halafu bomba moja inabeba?
Shekilango upo, changamoto ni ulijengwa kuhudumia watu elfu20 sasahivi wapo watu laki2
 
Nlijuwa kifuru kuna mfumo wa maji taka kwenye nyumba zenu huko
Kumbe bado mnatumia mashimo ya choo

Ova
Mbna hata mbezi ya kimaraa had Malamba kuelekea Segerea.
 
Na la kwangu linakaribia kujaa,lina jaa na maji ya mvua tu yani
 
Tatizo kashasema, pesa hana za kutosha kufanya hiyo kazi
Mkuu sisi wanaume tunajuana nmesema ukweli wangu ili nisaidiwe nilipokwama nisiposema nani atajua shida yangu na atanisaidiaje!? Issue ni kuwa wanaume wa leo hatuna ubinadamu hatusaidiani unaona ni bora mwanaume mwenzio ateseke ama kudhalilika nawe unafurahia hali hiyo..

Ujue Mpaka mwanaume anasema ukweli wake kuwa anahitaji msaada sio hali ya kawaida!? Sasa labda ninyioshe maelezo naomba kwa atakae wiwa ama kugushwa anaongezee kiasi kilichopelea cha laki 1 Tsh 100,000 nitakuwa nimetimiza laki na nusu ambapo nitapata gari...nitashukuru mno,

Unaweza usinipe mimi hiyo hera ila nikakupa namba za atakae fanya kazi hii ya kunyonya ukampa ama kumtumia yy mwenyewe hiyo laki au ukamtafuta wewe mwenyewe huyo mtu akimaliza na mimi nikaconfirm kuwa amemaliza kazi nitapiga na picha nikutumie uone na ujiridhishe ndo umpe yy mwenyewe moja kwa moja hiyo laki na mimi nimalizie hiyo inayobaki utakuwa umenisaidia pakubwa, asante na mkawe na siku njema.
 
Mkuu hilo shimo hukusakafia kwa ndani baada ya kulijenga?
Hapana mkuu mafundi waliniambia tusisakafie ili maji yawe wanaenda chini kwamba ardhi iwe inanyonya maji ndio maana sijasakafia chini lakini naona kama hili ndo kosa tulifanya maana eneo hili inaonekana kama kuna chemchem au maji yapo karibu sana maana hata majirani wanalalamika mashimo kipindi hiki cha mvua yanajaa. Nn ushauri wako je naweza chimba lingine na nikalisakafia na nafanyaje yote yatumike na tatizo liwe limeisha!??
 
Hapana mkuu mafundi waliniambia tusisakafie ili maji yawe wanaenda chini kwamba ardhi iwe inanyonya maji ndio maana sijasakafia chini lakini naona kama hili ndo kosa tulifanya maana eneo hili inaonekana kama kuna chemchem au maji yapo karibu sana maana hata majirani wanalalamika mashimo kipindi hiki cha mvua yanajaa. Nn ushauri wako je naweza chimba lingine na nikalisakafia na nafanyaje yote yatumike na tatizo liwe limeisha!??
Ooh hata mimi mwanzo sikusakafia maji yalikuwa yanajaa sana nikiwa bado sijahamia mvua ikinyesha kinakuwa kisima watu wanakuja kuchota maji ikabidi nisakafie ndiyo ikawa mwisho huu naenda mwaka wa tano toka nihamie sijawahi kuvuta.
Kwa hapo labda uchimbe lingine tena uwe nayo mawili

Ulifanikiwa kunyonya mkuu?
 
Ooh hata mimi mwanzo sikusakafia maji yalikuwa yanajaa sana nikiwa bado sijahamia mvua ikinyesha kinakuwa kisima watu wanakuja kuchota maji ikabidi nisakafie ndiyo ikawa mwisho huu naenda mwaka wa tano toka nihamie sijawahi kuvuta.
Kwa hapo labda uchimbe lingine tena uwe nayo mawili

Ulifanikiwa kunyonya mkuu?
Asante kwa ushauri, bado sijachonya mkuu ila hali ni tete sana aisee limejaa kweli kweli hera ndo tatizo.
 
Back
Top Bottom