TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,914
- 23,079
Ukirejea uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru M. jinsi kampeni za CCM zilivyoendeshwa ilidhihirika kuwa baadhi ya makada wa chama hicho ama kwa kudhamiria au kwa kupitiwa walihujumu umaarufu wa CCM na kusababisha kushindwa kurejesha jimbo hilo. Wafuatiliaji mnalijua hilo.
Hisia zangu ni kiwatuhumu viongozi hao wabunge niliowataja ktk kichwa cha uzi huu zinatokana na namna wanavyozidi kupukutisha imani ya wananchi juu uimara waCCM kuendelea kushika hatamu.
Hisia hizi zinadhibitishwa na namna viongozi hawa wanavyoshindwa kumudu kuendesha vikao vya bunge mara kwa mara. Maelezo juu ya hilo yapo mengi hapa Janvini (JF).
Hivyo nalazimika kuwahisi moja kwa moja viongozi hawa wanashiriki kuihujumu na kuiua kikamilifu CCM ktk siasa za nchi hii.
Yawezekana viongozi hawa wakadhani wanawadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani kutoa michangao yao bungeni kwa imani kuwa hapo wanadhibiti kasi ya vyama vya upinzani kutambulika kwa wananchi wengi, hivyo kufikiri kuwa CCM itaendelea kushika hatamu kwa ukiukwaji huu wa uendeshaji wa vikao vya Bunge.
Kama wanadhani hivyo wamekosea. Wananchi wengi wanafuatilia kwa karibu sana kinachoendelea bungeni na namna viongozi hawa wanavyoendesha vikao huko.
Matukio haya ya kuwadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani wanaoikosoa serikali ya CCM katika mijadala iliyoko bungeni kwa ukali yanawafanya wananchi kuanza kuwahurumia wabunge hawa na hivyo hata wale waliokuwa wanadhani CCM inatenda haki kuanza kuichukia pia.
Mazingira wanayoyatengeneza viongozi hawa wa Bunge katika hali ya sasa ya siasa za Tanzania nidhahiri yanaihujumu CCM.
Nimeliona hilo na imenilazimu niliseme.
Hisia zangu ni kiwatuhumu viongozi hao wabunge niliowataja ktk kichwa cha uzi huu zinatokana na namna wanavyozidi kupukutisha imani ya wananchi juu uimara waCCM kuendelea kushika hatamu.
Hisia hizi zinadhibitishwa na namna viongozi hawa wanavyoshindwa kumudu kuendesha vikao vya bunge mara kwa mara. Maelezo juu ya hilo yapo mengi hapa Janvini (JF).
Hivyo nalazimika kuwahisi moja kwa moja viongozi hawa wanashiriki kuihujumu na kuiua kikamilifu CCM ktk siasa za nchi hii.
Yawezekana viongozi hawa wakadhani wanawadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani kutoa michangao yao bungeni kwa imani kuwa hapo wanadhibiti kasi ya vyama vya upinzani kutambulika kwa wananchi wengi, hivyo kufikiri kuwa CCM itaendelea kushika hatamu kwa ukiukwaji huu wa uendeshaji wa vikao vya Bunge.
Kama wanadhani hivyo wamekosea. Wananchi wengi wanafuatilia kwa karibu sana kinachoendelea bungeni na namna viongozi hawa wanavyoendesha vikao huko.
Matukio haya ya kuwadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani wanaoikosoa serikali ya CCM katika mijadala iliyoko bungeni kwa ukali yanawafanya wananchi kuanza kuwahurumia wabunge hawa na hivyo hata wale waliokuwa wanadhani CCM inatenda haki kuanza kuichukia pia.
Mazingira wanayoyatengeneza viongozi hawa wa Bunge katika hali ya sasa ya siasa za Tanzania nidhahiri yanaihujumu CCM.
Nimeliona hilo na imenilazimu niliseme.