NAHISI: Wenyeviti, Naibu Spika na Spika wa Bunge wanaihujumu CCM

TUJITEGEMEE

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
23,914
23,079
Ukirejea uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru M. jinsi kampeni za CCM zilivyoendeshwa ilidhihirika kuwa baadhi ya makada wa chama hicho ama kwa kudhamiria au kwa kupitiwa walihujumu umaarufu wa CCM na kusababisha kushindwa kurejesha jimbo hilo. Wafuatiliaji mnalijua hilo.

Hisia zangu ni kiwatuhumu viongozi hao wabunge niliowataja ktk kichwa cha uzi huu zinatokana na namna wanavyozidi kupukutisha imani ya wananchi juu uimara waCCM kuendelea kushika hatamu.

Hisia hizi zinadhibitishwa na namna viongozi hawa wanavyoshindwa kumudu kuendesha vikao vya bunge mara kwa mara. Maelezo juu ya hilo yapo mengi hapa Janvini (JF).

Hivyo nalazimika kuwahisi moja kwa moja viongozi hawa wanashiriki kuihujumu na kuiua kikamilifu CCM ktk siasa za nchi hii.

Yawezekana viongozi hawa wakadhani wanawadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani kutoa michangao yao bungeni kwa imani kuwa hapo wanadhibiti kasi ya vyama vya upinzani kutambulika kwa wananchi wengi, hivyo kufikiri kuwa CCM itaendelea kushika hatamu kwa ukiukwaji huu wa uendeshaji wa vikao vya Bunge.

Kama wanadhani hivyo wamekosea. Wananchi wengi wanafuatilia kwa karibu sana kinachoendelea bungeni na namna viongozi hawa wanavyoendesha vikao huko.

Matukio haya ya kuwadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani wanaoikosoa serikali ya CCM katika mijadala iliyoko bungeni kwa ukali yanawafanya wananchi kuanza kuwahurumia wabunge hawa na hivyo hata wale waliokuwa wanadhani CCM inatenda haki kuanza kuichukia pia.

Mazingira wanayoyatengeneza viongozi hawa wa Bunge katika hali ya sasa ya siasa za Tanzania nidhahiri yanaihujumu CCM.

Nimeliona hilo na imenilazimu niliseme.
 
bitter truth! Halafu wamekuja na kamsemo eti sikutoi nje! Wapuuzi kweli hawa
 
Ukirejea uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru M. jinsi kampeni za CCM zilivyoendeshwa ilidhihirika kuwa baadhi ya makada wa chama hicho ama kwa kudhamiria au kwa kupitiwa walihujumu umaarufu wa CCM na kusababisha kushindwa kurejesha jimbo hilo. Wafuatiliaji mnalijua hilo.

Hisia zangu ni kiwatuhumu viongozi hao wabunge niliowataja ktk kichwa cha uzi huu zinatokana na namna wanavyozidi kupukutisha imani ya wananchi juu uimara waCCM kuendelea kushika hatamu.Hisia hizi zinadhibitishwa na namna viongozi hawa wanavyoshindwa kumudu kuendesha vikao vya bunge mara kwa mara. Maelezo juu ya hilo yapo mengi hapa Janvini (JF). Hivyo nalazimika kuwahisi moja kwa moja viongozi hawa wanashiriki kuihujumu na kuiua kikamilifu CCM ktk siasa za nchi hii.

Yawezekana viongozi hawa wakadhani wanawadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani kutoa michangao yao bungeni kwa imani kuwa hapo wanadhibiti kasi ya vyama vya upinzani kutambulika kwa wananchi wengi, hivyo kufikiri kuwa CCM itaendelea kushika hatamu kwa ukiukwaji huu wa uendeshaji wa vikao vya Bunge. Kama wanadhani hivyo wamekosea. Wananchi wengi wanafuatilia kwa karibu sana kinachoendelea bungeni na namna viongozi hawa wanavyoendesha vikao huko. Matukio haya ya kuwadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani wanaoikosoa serikali ya CCM katika mijadala iliyoko bungeni kwa ukali yanawafanya wananchi kuanza kuwahurumia wabunge hawa na hivyo hata wale waliokuwa wanadhani CCM inatenda haki kuanza kuichukia pia.

Mazingira wanayoyatengeneza viongozi hawa wa Bunge katika hali ya sasa ya siasa za Tanzania nidhahiri yanaihujumu CCM.

Nimeliona hilo na imenilazimu niliseme.

Kwa hiyo? Watu wengine vipi, kila mwenye hisia aki post hisia zake hapa JF nafikiri Server ya JF itajaa. Ushauri wa bure ukiwa na hisia discuss na mke wako
 
Hakuna cha wenyeviti, naibu spika wala cha spika wa bunge kuihujumu CCM, CCM inajihujumu yenyewe kwa ahadi zisizotekelezeka na kwa kuwatelekeza waTanzania huku wakubwa wakiendelea kunemeka kwa mikataba mibovu na kutumia vyombo vya dola kukandamiza demokrasia
 
Akili ndogo kuongoza akili iliyokubwa...mambo hayaendi. Ni sawa na kulazilisha maji ya mto yapande mlimani.
 
Mwogope sana Binadamu akifikia mwisho kufikiri maana ni sawa na mfu.Hao uliowataja wamafika mwisho wa kufikiri.
 
Bahati mbaya sana viongozi hawa wakifanikiwa kuizamisha CCM 2015 kwa matendo yao haya, watakuwa wamesababisha chama kitakachopata nafasi ya kuongoza nchi hii katika uchaguzi wa mwaka huo, kuwa na chama kikubwa cha upinzani legelege ambacho hakiwezi kumudu shughuli ya kuikosoa serikali kwa namna viongozi wake walio wengi kushidwa kujenga hoja huku wakiendekeza ushabiki wa kisiasa katika masuala ya msingi yanayowagusa wananchi moja kwa moja.
 
Naona na Mh.Lukuvi kajiunga na hawa jamaa kuiua CCM.

Yaani Mh. Lukuvi anataka tuamini kuwa anawahurumia sana CDM wasije wakaadhibiwa kwa kuzungumzia jambo ambalo liko mahakamani kweli? Nadhani sheria inaelekeza ni adhabu gani utapata kwa kuingilia mwenendo wa kesi kwa kuijadili nje ya mahakama. Sina hakika kama CDM wanaweza kukosa weledi juu ya jambo.
 
Hakuna spika atakayeweza kumfikia sitta, ndugui na makinda hamna kitu ni mipasho tu!

Kweli kabisa mkuu,Sitta alikuwa anaijenga ccm na kuonyesha kuwa hakuna kupendelea,sasa hawa vilaza wanakiua chama chao bila kujua ili wasifiwe na JK ambaye anelekea kustaafu.
Mungu tuepushe na hawa wapenda posho walioko madarakani.!!
 
CCM is a walking dead man. Sio kwamba wanaihujuma BALI NDIYO UWEZO WA KUFIKIRI UMEFIKIA MWISHO!

1. Spika na Naibu Spika kupindisha kanuni za bunge ..... Wanaihujumu CCM
2. Blunder ya TISS kumteka na kumtesa Dr. Ulimboka ...... Wanaihujumu CCM
3. Blunder ya Kova kutuletea mtekaji wa "kuchongwa" wa Ulimboka ...... Wanaihujumua CCM
4. Matusi ya Lusinde, Nchemba, Mkapa Arumeru ...... Wanaihujumu CCM
5. AG Werema kubaliki mswaada wa mabadiliko ya katiba mbovu ...... Anaihujumu CCM
6. Mgawo wa Umeme usiokwisha .......... TANESCO inaihujumu CCM
7. Bilioni 300 zilizofichwa USWISS na vigogo na wafanyabiashara wa Tanzania .......... Wanaihujumu CCM
8. Mgogoro wa madaktari na serikali ............. Madaktari wanaihujumu CCM

CCM wamefikia mwisho wa KUFIKIRI hakuna anayewahujumu bali wanajihujumu wenyewe.
 
never seen such incompetent ppo like the ones you've mentioned in the history of our parliament.
 
Loh ! hii hatari, Werema naye kaingia kwenye msafara wa kuizamisha CCM pia. Kauli ya .... sana hii ametoa.

Mimi nilijua tu kuwa kitendo cha CCM kushindwa kumkaripia 'Mh' Lusinde kwa maneno yake ya aibu/kujiabisha yeye na chama chake wakati wa uchaguzi wa mbunge Arumeru M., basi CCM ilikuwa imegundua njia mpya ya kujizika kwa kuanzisha Chuo Kikuu kipya cha cha kufundisha propaganda ya maneno ya aibu/kujiabisha huku wahitimu wa kwanza wa chuo hicho wakiwa makada wake wakuu.

Hisia zangu nadhani zaelekea kuwa sahihi.
 
Sasa ni rahisi kutabiri nikitugani Naibu Spika ataweza kutoa majibu gani pindi anapoomwa mwongozo na mbunge kutoka kambi ya upinzani.

Rejea shughuli ya bunge leo, jinsi alivyojibu mwongozo wa Mh. Mkosamali na Mh.Lissu. Naibu spika kakiuka kanuni dhahiri inayotaka nusu ya idadi ya wabunge kuwa nusu ndani ya bunge wakati wa kupitisha bajeti.

Poleni sana wapenda uwepo wa CCM.
 
Sasa ni rahisi kutabiri nikitugani Mh.Ndungai ataweza kutoa majibu gani pindi anapoomwa mwongozo na mbunge kutoka kambi ya upinzani.

Lejea shughuli ya bunge leo, jinsi alivyojibu mwongozo wa Mh. Mkosamali na Mh.Lissu. Naibu spika kakiuka kanuni dhahiri inayotaka nusu ya idadi ya wabunge kuwa nusu ndani ya bunge wakati wa kupitisha bajeti.

Poleni sana wapenda uwepo wa CCM.
yote kwa yote nawe unaefatilia BUNGE pole sana,,,,,,
 
miaka 50 ahadi zile zile chama kile ,watu wale wale wanabadilshana tu toto baba , mama ,imani itatoka wapi ,pengine ashuke malaika tu.
 
Ukirejea uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru M. jinsi kampeni za CCM zilivyoendeshwa ilidhihirika kuwa baadhi ya makada wa chama hicho ama kwa kudhamiria au kwa kupitiwa walihujumu umaarufu wa CCM na kusababisha kushindwa kurejesha jimbo hilo. Wafuatiliaji mnalijua hilo.

Hisia zangu ni kiwatuhumu viongozi hao wabunge niliowataja ktk kichwa cha uzi huu zinatokana na namna wanavyozidi kupukutisha imani ya wananchi juu uimara waCCM kuendelea kushika hatamu.Hisia hizi zinadhibitishwa na namna viongozi hawa wanavyoshindwa kumudu kuendesha vikao vya bunge mara kwa mara. Maelezo juu ya hilo yapo mengi hapa Janvini (JF). Hivyo nalazimika kuwahisi moja kwa moja viongozi hawa wanashiriki kuihujumu na kuiua kikamilifu CCM ktk siasa za nchi hii.

Yawezekana viongozi hawa wakadhani wanawadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani kutoa michangao yao bungeni kwa imani kuwa hapo wanadhibiti kasi ya vyama vya upinzani kutambulika kwa wananchi wengi, hivyo kufikiri kuwa CCM itaendelea kushika hatamu kwa ukiukwaji huu wa uendeshaji wa vikao vya Bunge. Kama wanadhani hivyo wamekosea. Wananchi wengi wanafuatilia kwa karibu sana kinachoendelea bungeni na namna viongozi hawa wanavyoendesha vikao huko. Matukio haya ya kuwadhibiti wabunge wa vyama vya upinzani wanaoikosoa serikali ya CCM katika mijadala iliyoko bungeni kwa ukali yanawafanya wananchi kuanza kuwahurumia wabunge hawa na hivyo hata wale waliokuwa wanadhani CCM inatenda haki kuanza kuichukia pia.

Mazingira wanayoyatengeneza viongozi hawa wa Bunge katika hali ya sasa ya siasa za Tanzania nidhahiri yanaihujumu CCM.

Nimeliona hilo na imenilazimu niliseme.

Jana Ndugai kaingizwa mjini na Lisu bila kujua. Unapoonekana unaitetea Zanzibar halafu kiongozi wa juu serkali ya Muungano anapinga inaamsha hisia mbaya za Wazanzibari dhidi ya muungano ambao sasa ndio kidonda cha CCM. Hivyo Maskini Ndugai alidhani anadhibiti kumbe anatoboa tundu.
 
CCM is a walking dead man. Sio kwamba wanaihujuma BALI NDIYO UWEZO WA KUFIKIRI UMEFIKIA MWISHO!

1. Spika na Naibu Spika kupindisha kanuni za bunge ..... Wanaihujumu CCM
2. Blunder ya TISS kumteka na kumtesa Dr. Ulimboka ...... Wanaihujumu CCM
3. Blunder ya Kova kutuletea mtekaji wa "kuchongwa" wa Ulimboka ...... Wanaihujumua CCM
4. Matusi ya Lusinde, Nchemba, Mkapa Arumeru ...... Wanaihujumu CCM
5. AG Werema kubaliki mswaada wa mabadiliko ya katiba mbovu ...... Anaihujumu CCM
6. Mgawo wa Umeme usiokwisha .......... TANESCO inaihujumu CCM
7. Bilioni 300 zilizofichwa USWISS na vigogo na wafanyabiashara wa Tanzania .......... Wanaihujumu CCM
8. Mgogoro wa madaktari na serikali ............. Madaktari wanaihujumu CCM

CCM wamefikia mwisho wa KUFIKIRI hakuna anayewahujumu bali wanajihujumu wenyewe.

Tetesi za mgomo wa walimu ni hujuma kwa CCm
Shida za wazanzibari kwa muugano ni hujuma kwa CCm
 
Kwa kweli haya mambo yanasikitisha sana, sidhni kama ni kuihujumu ccm bali huu ni udhihirisho wa uwezo wa watu binafsi maana sasa tunaona gap kubwa kabisa kati ya Mzee Sitta na waliopo sasa, kwa mazingira haya wa kulaumiwa ni ccm wenyewe maana ndivyo walivyoamua kuchagua na hakuna anayewahujumu.
 
Back
Top Bottom