Moana
Senior Member
- Jan 18, 2021
- 103
- 137
Aisee
Nalipwa 1.9M lakini ukiniangalia maisha yangu utacheka
Lakini katikati tu ya mwez nmeishiwa!!
- Sina gari
- Sina nyumba
- Kiwanja ninacho
- Sivai vizuri
- Sili vizuri
- Sipigi bata
Yaani najikuta hela inanitoka kwenye mazngira ya ajab ajab!! Sisemi inatoweka kama zile za chuma ulete NO but nikipata mshahara tu vishida na visababu vya kutumia hela vijatokea kusikojulikana!!
Mfano jana nimechelewa kuamka kwenda kazini ikabidi na kulikuwa na ugeni!! Na mimi ofisini ni mtu muhimu sana so ikabidi nikodi boda hadi kazini 13,000
Nilipofika nimesahau flash na ilikua na document muhimu ikabidi nirudi kwenda kurudi 26000
Bado sijala
Bado sijarudi jioni
Actually tuvitu twingi twingi tunasababisha hela itumike ili mradi iishe tu.
Nawaza kazi ikiisha ntaishije
Kuna shida gani hapa
We unaonaje? Share experience
Tengeneza list uwe unacheck kabla hujatoka home nini unatakiwa kwenda nacho afu tenga hela ambayo iwe isiwe lazima iende saving.. usiambie watu mshahara wako maana kuna ndugu wanalia shida mwisho wa mwez hata kama hakuna shida sababu anajua unapokea pesa nyingi