Nahisi jamaa yangu anatoka na mwanafunzi, nimeshangaa sana

Labda kama i am missing a point in your story ila jamaa kakuchukulia poa, nakujaje kugonge mlupo nyumbani kwako?? Hayo ni madharau, afu kama na wewe ulimkaushia na wewe basi ulizingua, maana kuna vitu vya kuvichukulia poa na kuna vitu si vya kuchukulia poa kabisa
 
Juzi kati jamaa yangu akanipigia, Mshkaji nilisoma naye High school. Tulipotezana kitambo ila hamadi tukakutana town tukabadilishana namba fresh.

Kwa sasa nimehamia kwenye kakibanda kangu ambapo jamaa since naanza ujenzi alikuwa hajawahi kuja though mimi kwake nimewahi kwenda kumtembelea, Jamaa ana wife na watoto 3.

Mimi nimeoa ila wife na dogo wako mkoa mwingine ambako wife kaajiriwa huko. Kwakuwa jamaa hapajui nilipohamia ikabidi nimfuate. Akanielekeza alipo ila haikiwa kwake, fresh nikaenda nikampick jamaa ila hakuwa mwenyewe jamaa alikuwa na kabinti flani kama kadent ka form 5 au 6 hivi.

Sikutaka kujishughulisha kwani pia sikutaka kujua. Ila nilihisi kama ni kadem kake. Baada ya kufika home tukawa na story za hapa na pale akanipongeza kwa ujenzi akatalii vyumbani kuona jinsi mafundi walivyofanya yao.

Basi nikaandaa msosi tukapiga ile fresh kabisa. Kwangu sina umeme ndio niko mbioni kuunganishiwa sasa jamaa akaomba nikamuwekee charge nyumba ya jirani, nikafanya hivyo.

Kurudi nakuta wametoka sebuleni wako chumba cha wageni wanaongea. Daaa kama mtu mzima nikaona isiwe tabu nikatoka zangu nikaenda kwa jirani kula story. Walitumia kama masaa 3 wakiwa wamejifungia.

Hii imekaeje waungwana. Is this fair au ndio kukua kwa science na technolojia
Mkuu nitakuja j2 kukutembelea, nabeba na charge kabisa
 
Sasa what is not fair hapo!!!? Mwanafunzi wa kidato Cha 5 sio mtoto huyo Ni mtu mzima ana Akili zake anajielewa , kinachonishangaza hapo Nini !? Tena huyo rafik ako Ni mstaarabu Sana mpaka umewakuta chumban tayari kakuonesha heshima kidogo hapo , wengine wangekusuprise ungerudi kuchomeka chaji ungewakuta wananjunjana hapohapo kwa sebule yako..... Relax man !!!!

nyinyi ndio dizain ya watu wa Instagram wanaomponda mtoto wa kajala kudate ikiwa she is over 22
Hakuna cha kurelax hapo, its not fair at all! Wasipigane mambo yao huko walikokuwa mpaka wakafanyiane hivyo nyumbani kwa mtu mwingine! Sio sawa kabisa, ukizingatia mtu ndio kwanza anamalizia nyumba yake, ni kweli wanaweza kumwachia mikosi. Wangemwacha aizindue yeye na mkewe na sio wao mtu na kistudent chake!!
 
Nakumbuka wakati naishi zangu gheto Mtoni kwa Azizi Ali, kipindi nakaribia kuchukua jiko, One day kuna rafiki yangu alikuja kunitembelea, jioni nilitoka kidogo kuna mtu nilikwenda kumcheki maeneo ya kwa Kabuma, nikakumbuka kuna kitu nilisahau halafu mchizi yuko gheto.

Ile narudi kufika gheto jamaa yuko ndani na mlango umefungwa gonga sana eboo! Nikaona isiwe tabu nikamsubiria alipomaliza mambo yake na kunifungulia mlango kibinti cha watu kikatoka ndani na kuondoka nikamwambia mshkaji kama urafiki utakufa na ufe......

Nilimuuzia kwa lazima kitanda na godoro lake nikahama kabisa gheto na kuhamia kwengine!

Hela aliyonipa nikaongezea na kununulia vifaa katika gheto jipya!!


Kitanda nilichopanga kukilalia na mke wangu ni haramu kwangu kukilalia mwingine kabla ya mke wangu!
 
seriously pre form one hukumtambua
Hadi castle light alikunywa. Tulifika sehemu kinondoni nikamwagizia chipsi kuku mi nikachukua safari kubwa, mhudumu alivyomuuliza we nikuletee kinywaji gani! Akasema castle light.

Baadae nikasikiaga hadi mtaani kwao alishawahi kukamatwa na mume wa mtu wakati yupo darasa la sita huko mtaa wa Sogodo Kino hapo hapo.
 
Back
Top Bottom