mambo ya nyakati
Senior Member
- Aug 24, 2022
- 115
- 144
Ushauri,
Juzi nipo na mpenzi wangu tumekaa tunapata kinywaji, harakati za hapa na pale nikahisi jambo kwenye simu yake. Kumpokonya simu, simu ikaleta password kila file, ila mwanzo haikuwa na password kwenye mafile.
katika ugomvi wa hapa na pale akasusa, kaacha simu yake akaondoka kwao, me nikashindwa kusoma kila kitu, na mimi nikarudi home kulala.
Asubuhi nikapata wazo niitoe lain yake niweke kwangu, mara baada yakuweka simu namba ngeni inapigwa, nikakata. Kukataa meseji imeingia, kwanini unakata simu, unazingua, uko wapi? Mimi nikajibu tuma message niko sehemu mbaya. Hajajibu message akawa anapiga nikakata, kukata hajajibu message tena. Kakaa kimya, kucheki jina usajili, Xwake walioachana.
Baadae kaja home kuongea anasema anamsumbuaga tu, hakuna lolote, kuomba msamaha yakaisha yakapita.
Leo kaniita sehemu tumekaa tunainjoy nikahisi jambo, nikakaza nipe simu yako tuone kama ile namba bado inakucheki kakataa katakata, akaondoka kulala kaniacha sehemu saa 6 usiku peke yangu.
Nafikiria sana, katika maisha yangu niliapa sitokuja kupenda tena. Najikuta nimeingia cha kike tena. Nifanyeje wakuu niwe mkatili? Kwanini narudia makosa ya kupenda penda watoto wa watu?
Kwanini mimi isee?!
Juzi nipo na mpenzi wangu tumekaa tunapata kinywaji, harakati za hapa na pale nikahisi jambo kwenye simu yake. Kumpokonya simu, simu ikaleta password kila file, ila mwanzo haikuwa na password kwenye mafile.
katika ugomvi wa hapa na pale akasusa, kaacha simu yake akaondoka kwao, me nikashindwa kusoma kila kitu, na mimi nikarudi home kulala.
Asubuhi nikapata wazo niitoe lain yake niweke kwangu, mara baada yakuweka simu namba ngeni inapigwa, nikakata. Kukataa meseji imeingia, kwanini unakata simu, unazingua, uko wapi? Mimi nikajibu tuma message niko sehemu mbaya. Hajajibu message akawa anapiga nikakata, kukata hajajibu message tena. Kakaa kimya, kucheki jina usajili, Xwake walioachana.
Baadae kaja home kuongea anasema anamsumbuaga tu, hakuna lolote, kuomba msamaha yakaisha yakapita.
Leo kaniita sehemu tumekaa tunainjoy nikahisi jambo, nikakaza nipe simu yako tuone kama ile namba bado inakucheki kakataa katakata, akaondoka kulala kaniacha sehemu saa 6 usiku peke yangu.
Nafikiria sana, katika maisha yangu niliapa sitokuja kupenda tena. Najikuta nimeingia cha kike tena. Nifanyeje wakuu niwe mkatili? Kwanini narudia makosa ya kupenda penda watoto wa watu?
Kwanini mimi isee?!