Mkuu ni bora ungeandika kwamba unahitaji mtu akupe gari uwe unafanyakazi.
Ila suala la bodaboda ulete kwenye gari?
Bodaboda zenyewe siku hizi hakuna anaetaka upuuzi huo.Ingekuwa hivyo haya ma DC yoote kwa miaka yaliyomo njiani yangekuwa mali ya madereva.
Mikataba hiyo ilikuwa inaingiwa na watu wa bodaboda,na wengie ni wenye uelewa mdogo sana wa biashara na kutojiamini.Ndio maana wakawa wanaingia jiti kwa kusema kwamba baada ya muda unamuachia chombo kinakuwa mali yake.
Taxi kwa bei yake na ili ufanye kazi kwa mazingira mazuri ikiwa bado nzima kiasi si chini ya 6m - 7m.
Sasa we niambie deni hadi liishe liishe ni miaka mingapi,si chini ya mitatu,maana hapo kuna misiba,kuharibika na matengenezo kibaoo hasa mwaka wa mwisho.
Ushauri kwangu,badilisha tangazo,.wewe ingia mkataba kama Taxi Driver wa kawaida,kisha baada ya mwaka,unaanza kumtongoza bosi wako akuuzie gari,hapo itakupa akili ya kuweka akiba.Ila kwa mkataba wako huu ni tatizo sana na hakuna anaeweza ku risk kwa pesa nyingi namna hiyo.
Hawa wenye Taxi tu kwa kupeleka hesabu ya siku vurugu mtu,sasa wewe unafikiria itakuwaje.
Ni mtizamo wangu tu kaka.