Mkuu nimesikia kuna nafasi zitatoka hivi karibuni mwezi october kwaajili ya form6 unaweza ukaomba pia, japo zile kwaajili ya ngazi ya shahada ni mpaka January. Kwanini nakushauri uombe hizo zikitoka? Kuzingatia kigezo cha umri, mwisho ni miaka 25 kujiunga na jeshi la wananchi na kwakua tayari umefikisha umri huo mkuu, ukisema usubiri hadi mwakani umri utakua umevuka kiwango hiko. Hivyo ni vyema basi nafasi zitakapotangazwa kwa waliomaliza form 6 hapo october nawe uombe, kwani pia una kigezo cha shahada ambapo ni added advantage.