Nafasi ya Kazi: "Delivery Driver"

Nafasi ya Kazi: "Delivery Driver"

hbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2011
Posts
678
Reaction score
298
Habari, msishangae kurudia hili tangazo. Mtu aliyekua amepatikana mwanzo amepata dharura binafsi na kushindwa kuanza kazi hivyo imetulazimu kutafuta mtu mwingine.


Kuhusu P2P Delivery Company:
Tunatoa huduma ya kusafirisha nyaraka na vifurushi ndani ya jiji la Dar es salaam.

Tunahitaji "Delivery Driver" atakayekua anafanya kazi ya kusafirisha vifurushi vya wateja kutoka sehem moja kwenda sehem nyingine ndani ya Dar es salaam.

Vigezo:
  • Uwe na leseni halali, kama hauna na unweza kuendesha pikipiki vizuri unaweza kuwasiliana nasi pia tukazungumza namna ya kukutafutia leseni. Ila kipaumbele kitatolewa kwa wale wenye leseni tayari.
  • Uwe na uwezo wa kuhudumia wateja, ikiwa ni pamoja na nidhamu na kauli nzuri kwa wateja.
  • Uwe na uwezo wa kuwasiliana kwa ufasaha.
  • Mwenyeji wa jiji la Dar es salaam na anayejua maeneo vizuri.
  • Uwezo wa kufanya kazi bila kusimamiwa.
  • Uwezo wa kubeba bidhaa za gharama na ambazo zinaweza kuvunjika kwa urahisi.
  • Mwenye nidhamu na uwezo wa kufanya kazi na watu wengine.
  • Asiwe na rekodi za uhalifu au makosa ya jinai.

Kama unakidhi vigezo hapo juu, tafadhali tuma ujumbe kwenda namba 0658123748 ukijibu maswali yafuatayo.

  • JINA LAKO KAMILI.
  • UMRI WAKO na MAHALI UNAPOISHI.
  • JIBU NDIYO kama unayo LESENI na HAPANA kama hauna leseni.
  • KIWANGO UNACHOTEGEMEA KULIPWA KWA WIKI au KWA MWEZI.
Baada ya kujibu maswali hayo juu, utajulishwa utaratibu utakaofuata.
Angalizo: Mafuta na gharama za ufundi wa chombo cha usafiri utagharamiwa na ofisi.
 
Kazi ya ofisi mlitaka mafuta na gharama za ufundi inapotokea hitilafu ziwe za kwake?
Inashangaza kama si kustaajabisha.
 
Kazi ya ofisi mlitaka mafuta na gharama za ufundi inapotokea hitilafu ziwe za kwake?
Inashangaza kama si kustaajabisha.
Hatujataka iwe hivyo, bali tumetanabaisha kwa kuwa watu wamekua wakiuliza hilo swali.
 
Asanteni wale wote waliotuma meseji zao kwa ajili ya kuomba kazi, mtusamehe hatukuweza kumjibu kila mtu. Pia kuna wengine tuliwaita kwa ajili ya usahili wakashindwa kufika na hawakutoa sababu zozote. Nafasi imeshajazwa tayari na mtu ataanza kazi jumatatu ijayo.

Hivi punde tutawajulisha tena pale tutakapohitaji mtu mwingine, asanteni kwa ushirikiano wenu mliouonesha.
 
NDIO...!!
Mkuu nashukuru kwa tangazo na naomba hiyo kazi naamini ntaifanya kwa ustadi wa hali ya juu,
ELIMU
Kidato cha nne nmemaliza mwaka 2014
Elimu ya udereva wa magari na leseni class D
UZOEFU
Nimefanya kazi kwenye makampuni binafsi mengi ila makampuni mawili ambayo ni Aramex na Freight Forwarders nilifanya kama mtoa huduma kwa wateja. Kwa hiyo nna uzoefu wa kutosha wa kufanya kazi na wateja.
Nna uzoefu wa kuendesha gari ndogo na pick-up, pikipiki na bajaji na zote nna leseni nazo
Mshahara
Mkuu mshahara ntapenda kama ukinilipa kwa wiki 105,000/= pamoja na allowance za mawasiliano na kazi hatarishi.
 
NDIO...!!
Mkuu nashukuru kwa tangazo na naomba hiyo kazi naamini ntaifanya kwa ustadi wa hali ya juu,
ELIMU
Kidato cha nne nmemaliza mwaka 2014
Elimu ya udereva wa magari na leseni class D
UZOEFU
Nimefanya kazi kwenye makampuni binafsi mengi ila makampuni mawili ambayo ni Aramex na Freight Forwarders nilifanya kama mtoa huduma kwa wateja. Kwa hiyo nna uzoefu wa kutosha wa kufanya kazi na wateja.
Nna uzoefu wa kuendesha gari ndogo na pick-up, pikipiki na bajaji na zote nna leseni nazo
Mshahara
Mkuu mshahara ntapenda kama ukinilipa kwa wiki 105,000/= pamoja na allowance za mawasiliano na kazi hatarishi.

eti kazi hatarishi, hapo najua unaongelea kiangushi aka pikipiki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom