Mfalme wa Gheto
Member
- Jul 27, 2012
- 41
- 28
ukifatilia kwa makini kabisa utagundua Kuwa Tanzania ndio nchi pekee ulimwenguni inayosifika kuwa na viongozi ktk eneo nyeti(Serikali) ambao ni majuha kuanzia top hadi bottom. hebu imagine serikali inahaha katengeneza barabara kwa kutumia mabilioni ya kodi za wananchi(then humo humo ktk miradi wanaiba hzo fedha) wakati taarifa inaonyesha uharibifu wa barabara unasababishwa na malori ya mizigo, nini kifanyike hapo ndo utaona ujaha wa viongozi,wanaapply project nying za kijambazi wakati kuna reliable,easy and affordable way ya kuzikarabati reli zetu ili mizigo mizito iwe inapitishwa kwa reli.Leo unaambiwa wamezindua usafiri wa reli ktk mji wa Dar kupunguza foleni! kweli ukistaajabu ya Musa utashangaa ya Firauni hvi mnataka kuwaaminisha watanzania kuwa viunga vyote vya mji wa dar watatumia treni kama njia mbadala ya kuwaondolea usumbufu wa foleni? hv mfano mtu anayetoka mbezi au kimara kwenda kariakoo hiyo reli ina maana gani kwake?haya wa TMK kwenda posta, muhimbli? halafu watu wanaona kuna bonge la jitihadalimefanywa. kweli ni rahisi sana kuongoza Tanzania sababu huhitaji kuwa na akili yeyote zaidi ya ujuha kwani hata wananchi wake wengi wanasumbuliwa na ujuha. ni mtazamo tu wadau