Nachechemea

B.O.G

Senior Member
Feb 17, 2011
144
40
(Machozi yananitoka) Kijana mmoja ambaye ana ulemavu wa miguu ameamu kujitafutia riziki yake kwa kujiajili. Huwa anauza biscuts, karanga na vitu vingine vingine kama matoi ya watoto wadogo. na eneo lake la biashara ni sehemu ya kivukoni ambapo abilia wa ferry huwa wanasubiria.ndugu msomaji huyu mtu mguu wake mmoja ni mrefu kuliko mwingine hinyo anatembea kwa tabu lakini juwa akai chini bali hutembea pande moja mpaka nyingine pasipo kumbugudhi mtu yoyote (ukimuona utamuonea huruma na utatamani hata ununue kitu chochote kwake na umwambie tafadhari keep chenji) . hapa kivukoni na tanzania nzima kwa ujumla kuna watu wengi sana wenye uhafadhali kwake lakini hawajitumi kufanya chochote ili wajitegemee na huishia kuomba omba.
Leo kijana huyo akiwa anaingia sehemu yake ya kazi mlinzi wapale ferry akamsukuma na kuanza kumtoa nje kwamaba haruhusiwi kufanayia biashara sehumu ile ya kivuko. katika purukushani za hapa na pale yule mlinzi akanza kumpiga kwa jeuri , abilia walio kuwa eneo latukio waka mvaa yule mlinzi ili wampe kipondo ila kwa bahati nzuri akawa amewaponyoka na kumbia kwa asikari polisi. baada ya mda wakaja askari polisi wawili wakike na wakiume pamoja na yule mlinzi wakamfuata yule kilema wakawa wanaongea naye na kuanza kumtoa nje. wananchi tena waka chachama ikawa ni mzozo mkubwa pale ndani hatimaye yule askari wa kiume akaondoka na yule kilema . akawa amebaki askari wakike anaongea na watu. mda wote huo nilikuwa nime simama sehumu nangalia picha ila nika sikia asikari huyo akiseam kuwa "KISHERIA HARUHUSIWI MTU YEYOTE KUFANYA BIASHARA HUMU NDANI YA SEHUMU YA KIVUKO" hapo ndipo na mie jaziba yangu ilipo panda na kumfata yule askari na kumwuliza kama haruhusiwi kufanya humu ndani "HAYA MATANGAZO YA AIRTEL YANA FANYA NINI HUMU NDANI" nikajibiwa kuwa hilo sijui na mwana mama akasepa.
na watu wengine wakauliza pia kwamba kile kibanda cha biashara kilichoko humo ndani kwa nini kisifungwe.
Wana janvi hayo ndiyo nilio shuhudia leo na kama kuna mtu pia alikuwepo laba ana lakuongezea ama kuna sehemu anaona nimekosea ntafurahi kurekebishwa. Mungu ibariki Tanzania
 
siyoni tatizo lolote la askari kumzuia kibaya pale ni kumpiga,hivi tukiruhusu biashara ifanyike kila mahali unadhani huu umaskini utaisha? watz tujifunze kuheshimu sheria,awe mlemavu awe nani
 
huoni shida yeye kukatazwa ni sawa, bali mie shida ninayo iona ni nani kawapa hawa Nova Media kibali cha kufanya biashara ya matangazo sehemu ambayo siyo sahii.
 
akiseam kuwa"KISHERIA HARUHUSIWI MTU YEYOTE KUFANYA BIASHARA HUMU NDANI YA SEHUMU YA KIVUKO" hapo ndipo na mie jaziba yangu ilipo panda na kumfata yule askari na kumwuliza kama haruhusiwi kufanya humu ndani "HAYA MATANGAZO YA AIRTEL YANA FANYA NINI HUMU NDANI".

Kunatofauti kati ya kuafanya biashara na kutangaza biashara.
 
akiseam kuwa"KISHERIA HARUHUSIWI MTU YEYOTE KUFANYA BIASHARA HUMU NDANI YA SEHUMU YA KIVUKO" hapo ndipo na mie jaziba yangu ilipo panda na kumfata yule askari na kumwuliza kama haruhusiwi kufanya humu ndani "HAYA MATANGAZO YA AIRTEL YANA FANYA NINI HUMU NDANI".

Kunatofauti kati ya kuafanya biashara na kutangaza biashara.

ni kweli mheshimiwa , ila yale matangazo yana sehemu mbili mtangazaji mfano Airtell na mmiliki wa vyombo vya kutangazia kama vile Tv zinazo tupigia kelele kwenye kivuko na Big screan ambayo ipo eneo lamagogoni na kigamboni kwenye sehemu ya kusubiria kivuko.
sasa the point ni kwamba yule Nover medi hawa watu anao watangazia wanamlipa yaani Airtell ,PPF na kadhalika. na maana halisi ya biashara ni kuto huduma ama bidhaa kwa mtu au kikundi cha watu ili wakupatie pesa. Je huyu nova Media Halipwi na Hawa watu wake anao watangazia kwanza mbali na kwamba anafanya biashara sehemu ya kivuko na kwenye kivuko chenyewe kwakweli matangazo yao ni moja ya noise pollussion.
 
yaani nina hasira na maaskari wa kibongo aaagrrrriii yanatumia miguvu badala ya akili ndo maana wanasema yamefeli yakakimbilia upolice,very stupid.
 
Back
Top Bottom