Kipenzi Changu
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 57,913
- 133,926
Muhubiri wa Kanisa la Arise and Shine International, Boniface Mwamposa amesema Watanzania wanapaswa kubadilisha mtindo wa maisha na kuachana na uvivu unaowafanya kupoteza muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii badala ya kujikita katika maendeleo.
Akihubiri Jumapili kanisani Mwamposa amesema Taifa linakumbwa na changamoto ya Watu wengi kupenda umbea na hadithi badala ya kufanya kazi kwa bidii. “Tanzania ni Taifa pekee ambapo hata Mfanyakazi wa ndani anachukua mshahara kuweka bando ili kufuatilia umbea mitandaoni. Watu wanashangaa kwa nini Wawekezaji hawawaajiri wazawa ni kwa sababu wengi hawana nidhamu ya kazi,” amesema.
Mwamposa ameeleza kuwa Mtu yeyote mwenye maono anatafuta Mfanyakazi anayejituma bila kusimamiwa kila mara lakini Watanzania wengi wanahitaji kufuatiliwa kila wakati ambapo amesema hali hiyo inasababisha baadhi ya Watu kuajiri Wageni kwa sababu wanaona wana nidhamu na ufanisi mkubwa kazini. “Mtu mwenye maono anataka Mfanyakazi anayejituma lakini ukiweka Mtanzania kazini unakuwa mtumwa wa kumfuatilia,” amesema.
Pia ameitaka Serikali kuwekeza kwenye mitandao ya kijamii ya kizalendo inayojenga ufahamu wa Watu badala ya kuharibu. “Mitandao ni zaidi ya bangi, na Tanzania ni miongoni mwa Nchi zinazoongoza kwa matumizi ya mitandao ya kijamii lakini si kwa mambo ya maana bali umbea na uvivu. Tukibaki hivi, barabara tunazojenga zitaendeshwa na Wageni kwa sababu vichwa vya Watanzania vinaharibiwa na mitandao,” amesema Mwamposa
Akihubiri Jumapili kanisani Mwamposa amesema Taifa linakumbwa na changamoto ya Watu wengi kupenda umbea na hadithi badala ya kufanya kazi kwa bidii. “Tanzania ni Taifa pekee ambapo hata Mfanyakazi wa ndani anachukua mshahara kuweka bando ili kufuatilia umbea mitandaoni. Watu wanashangaa kwa nini Wawekezaji hawawaajiri wazawa ni kwa sababu wengi hawana nidhamu ya kazi,” amesema.
Mwamposa ameeleza kuwa Mtu yeyote mwenye maono anatafuta Mfanyakazi anayejituma bila kusimamiwa kila mara lakini Watanzania wengi wanahitaji kufuatiliwa kila wakati ambapo amesema hali hiyo inasababisha baadhi ya Watu kuajiri Wageni kwa sababu wanaona wana nidhamu na ufanisi mkubwa kazini. “Mtu mwenye maono anataka Mfanyakazi anayejituma lakini ukiweka Mtanzania kazini unakuwa mtumwa wa kumfuatilia,” amesema.
Pia ameitaka Serikali kuwekeza kwenye mitandao ya kijamii ya kizalendo inayojenga ufahamu wa Watu badala ya kuharibu. “Mitandao ni zaidi ya bangi, na Tanzania ni miongoni mwa Nchi zinazoongoza kwa matumizi ya mitandao ya kijamii lakini si kwa mambo ya maana bali umbea na uvivu. Tukibaki hivi, barabara tunazojenga zitaendeshwa na Wageni kwa sababu vichwa vya Watanzania vinaharibiwa na mitandao,” amesema Mwamposa