Naanza kuchukia baadhi ya sera za Magufuli. Hivi tunajenga au tunabomoa?

Davion Delmonte Jr.

JF-Expert Member
Oct 27, 2013
2,149
1,718
Katika nchi maskini kama Tanzania naamini kabisa kiongozi hatakiwi kufanya decision bila kutizama hali halisi ya wananchi. Mfano katika siku za karibuni kumekuwa na maamuzi ambayo kwa kweli ni magumu hasa ukizingatia yanagusa moja kwa moja tabaka la wananchi wa ngazi ya chini.

Mfano tu kuna hili suala la bomoa bomoa ambalo naona kama limeshika kasi. Nisingependa kukosoa kwani kuna sababu stahiki za bomoa bomoa lakini wasiwasi wangu ni kwamba zoezi linaenda katika hali ambayo kwa namna moja inawaacha raia walengwa katika ugumu fulani wa maisha.

Ningetoa Rai yangu kwa Magufuli na watekelezaji sera wake " Hii ni Tanzania na ni moja wapo ya nchi masikini ambayo pia raia wake wengi hawana elimu kwa hiyo basi ingepaswa maamuzi kama haya yawe yanawashirikisha walengwa badala ya kuvamia tu na matingatinga na kuanza kuvunja nyumba za raia"

Mh Rais hii nchi yetu bado changa na huwezi tu ukafuata sheria bila kuangalia uhalisia wa maisha ya wananchi. Hapo tutakuwa hatujengi bali tunabomoa. Naelewa vema azma yako ya kuipatia maendeleo nchi hii lakini kuna sehemu nyingine lazima tuende kwa speed ya ki pwani pwani maana tukienda kwa speed ya ki London London ni wazi utaumiza wengi.

Hata hii hatua ya kubomoa nyumba za watu zenye thamani kubwa na mahoteli kwa dhana kwamba eti wamejenga kwenye viwanja vya wazi hilo nalo nna mashaka nalo maana jenzi zozote zinapata vibali kutoka halmashauri husika. Kwa hiyo kama ni tatizo saa nyingine halipo kwa raia bali kwa watendaji wa serikali wenyewe.

Mi sitaki kuamini kuanza ku deal na bomoa bomoa kwa kipindi hiki kutanufaisha wananchi walio wengi. Nadhani kuna mambo mengi ya kufanya kwa sasa. Hata na hivo bomoa bomoa haikuwa kwenye ilani ya CCM.

Halafu tangu uchaguzi uishe naona harakati za kisiasa na kazi za serikalini ni Dar es salaam tu, ina maana mikoa mingine sio sehemu ya Tanzania? Mara muhimbili hospital mara sijui wap wap.. yaani Dar tu. Tabora nayo ni Tanzania na kuna shida nako kweli kweli..

No offence,, namkubali sana Rais ila kuna mambo yananipa ukakasi na lazima niandike.
 
Mtoa maada hao watu hata kama ni mimi mlengwa ambae natakiwa nyumba yangu ishushwe sawa tu!! Hao watu walishalipwa zama na walipewa maeneo mabwepande hawajaenda kujenga pesa wakazipiga wenye akiri walijenga.. Watu kama hao ndo walalamishi kila siku na wanarudisha nyuma maendeleo.. Kwa hilo kama na wewe umebomolewa kubali yaishe serikali haikurupuki mambo yao yamepangiliwa. Pole kama umekutwa na mkasa ila mkiambiwa kuhama kwa hiari hamtaki!
 
Hivi mipango miji haikuwa na ramani ya kila eneo ili kuzuia watu wasijenge sehemu zisizo husika?
 
Mtoa maada hao watu hata kama ni mimi mlengwa ambae natakiwa nyumba yangu ishushwe sawa tu!! Hao watu walishalipwa zama na walipewa maeneo mabwepande hawajaenda kujenga pesa wakazipiga wenye akiri walijenga.. Watu kama hao ndo walalamishi kila siku na wanarudisha nyuma maendeleo.. Kwa hilo kama na wewe umebomolewa kubali yaishe serikali haikurupuki mambo yao yamepangiliwa. Pole kama umekutwa na mkasa ila mkiambiwa kuhama kwa hiari hamtaki!
Mkuu usiropoke,mimi ni mhanga na wala sikupata kiwanja wala kulipwa,NO RESEARCH NO RIGHT TO SAY
 
#Vnice ukiongea kitu uwe na kumbukumbu au taarifa sahihi. Waliopewa viwanja mabwepande hawazidi hata 60 na ilikua ni kinondoni Suna tu. Wale wa mkwajuni hakuna kiwanja wala pesa waliyopewa. Pia ufahamu jangwani hawakupewa wanachofanya watendaji wanamdanganya Magufuli kua walipewa lakini uhalisia si kweli. Viwanja wamegawana maafisa wa halamashauri na kiviuza kwa watu wengine. Na ubomoaji hauzingatii sheria wala kanuni ni uhuni tu. Haiwezekani timu inafika eneo la tukio unaanza kuonyesha vunja hii,hii acha. Walipaswa kuja na kuweka alama za nyumba zote ambazo zitavunjwa kwanini hawataki kushirikiana na serikali za mitaa juu ya zoezi lao?Waje na hoja zao juu ya meza na wapime hifadhi za mto ni wapi ili wananchi wajue walipo hawastahili. Pia sheria zote wanazozitumia ni upuuzi mtupu yaani maafisa hawajui kutafsiri sheria. Sheria ni ya 2004 na 1997 kuna watu wapo pale tangu mwaka 70 sheria haiwahusu kabisa lakini haki zao nani atetee? AU mngependa kuona wakazi wa mabondeni wakionyesha kuchoshwa???Ufikie wakati nguvu si suluhisho ya matatizo yetu.Hekima inahitajika kukiendea hili wale ni Watanzania maskini kabisa maana yale mazingira kama una fedha huwezi kuishi huko lakini je wafanyeje?Mnaita maeneo hatarishi sawa mbina serikali imejenga kituo cha mabasi ya kwenda kasi sehemu hatarishi???Je wameacha mita 60?Je wamefanya nini hadi uhatarishi umeondoka?Nani hajui kua jangwani panajaa maji?mratu wa brt upo pale kwenye kingo ya mto. Ukuta ulishawahi kuzolewa na maji. Lakini hekima ukiitumia sehemu moja uangalie na ingine pia. Msiseme watu wa mabondeni kupitia mitandao ya kijamii fikeni mpate kuwasikia je wana hoja za msingi au wanapiga kelele??
 
Kama lengo ni kutekeleza sheria sina la kusema hata mgonjwa wetu angepata angefanya hivyo.

Nitasema zaidi kama kuna ukiukwaji wa sheria, nasubiri.
 
#Vnice ukiongea kitu uwe na kumbukumbu au taarifa sahihi. Waliopewa viwanja mabwepande hawazidi hata 60 na ilikua ni kinondoni Suna tu. Wale wa mkwajuni hakuna kiwanja wala pesa waliyopewa. Pia ufahamu jangwani hawakupewa wanachofanya watendaji wanamdanganya Magufuli kua walipewa lakini uhalisia si kweli. Viwanja wamegawana maafisa wa halamashauri na kiviuza kwa watu wengine. Na ubomoaji hauzingatii sheria wala kanuni ni uhuni tu. Haiwezekani timu inafika eneo la tukio unaanza kuonyesha vunja hii,hii acha. Walipaswa kuja na kuweka alama za nyumba zote ambazo zitavunjwa kwanini hawataki kushirikiana na serikali za mitaa juu ya zoezi lao?Waje na hoja zao juu ya meza na wapime hifadhi za mto ni wapi ili wananchi wajue walipo hawastahili. Pia sheria zote wanazozitumia ni upuuzi mtupu yaani maafisa hawajui kutafsiri sheria. Sheria ni ya 2004 na 1997 kuna watu wapo pale tangu mwaka 70 sheria haiwahusu kabisa lakini haki zao nani atetee? AU mngependa kuona wakazi wa mabondeni wakionyesha kuchoshwa???Ufikie wakati nguvu si suluhisho ya matatizo yetu.Hekima inahitajika kukiendea hili wale ni Watanzania maskini kabisa maana yale mazingira kama una fedha huwezi kuishi huko lakini je wafanyeje?Mnaita maeneo hatarishi sawa mbina serikali imejenga kituo cha mabasi ya kwenda kasi sehemu hatarishi???Je wameacha mita 60?Je wamefanya nini hadi uhatarishi umeondoka?Nani hajui kua jangwani panajaa maji?mratu wa brt upo pale kwenye kingo ya mto. Ukuta ulishawahi kuzolewa na maji. Lakini hekima ukiitumia sehemu moja uangalie na ingine pia. Msiseme watu wa mabondeni kupitia mitandao ya kijamii fikeni mpate kuwasikia je wana hoja za msingi au wanapiga kelele??
Umenena mkuu,kuna majitu ni mabingwa wa kuropoka bila kuwa na taarifa sahihi,hata hao wa suna hawakupewa wote viwanja,
 
Wengi waliobomolewa walijua wanafanya makosa wakati wanajenga, Wengi wao walijipatia haya maeneo ya wazi kwa kulazimisha(Kutoa Rushwa), walithani hii siku ya kubomolewa haitafika karibuni.
 
Watu wanalaumu na kuwakebehi watu wa mabondeni lakini hawajuhi watu hawa wapo katika hali gani.

Ukweli ni kwamba hakuna mtu hata mmoja anayependa kupata matatizo kwa kujitakia.

Na tumekuwa wa kwanza kuwanyoshea vidole kwamba wahame mabondeni tu lakini hatujagusa sababu kuu ya watu kujenga mabondeni, ni sawa na kuua mbu lakini tukiacha masalia ya mbu salama, Hakika mbu watarudi tena.

Na mamlaka husika hawana nia ya kusikiliza na kutatua matatizo labda kwa kujua wao ndio chanzo kikuu cha tatizo au ubabe usiokuwa wa manufaa hebu fikiri nyumba elfu nane zinavunjwa, hivi familia husika zitakaa wapi na hili ndio tatizo kubwa. Je hawa watu watakaa wapi kwa muda huu ambao wanatafuta makazi mapya??, na Je serikali imejiandaa vipi?

Nikirudia kwenye hoja ya msingi ni kwamba watu wanajenga mabondeni kwa sababu zifuatazo:

(I) Hebu tujiulize wakina nani wanapata viwanja mara Halmashauri inapotangaza uuzaji wa viwanja vipya?, Kama ujakuta wanaopata ni watu wale wale, na kwa nini hali hii inajirudia?.

(II) Tujiulize je vipato vya wakazi wengi wa mabondeni vinawawezesha kupata viwanja vinavyouzwa na Halmashauri ya mijini hapa Dar - es - Salaam, Kwa mfano wilaya ya Kinondoni walitoa viwanja Mabwe Pande kama wiki mbili zilizopita, Na vilikuwa vinauzwa Tshs. 12,000.00 kwa mita ya mraba. Kwa mahitaji ya ya uwanja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya kawaida, Mita za mraba 500 ingegharimu Tshs. 6,000,000.00
( Milioni sita). Swali tena wangapi wanaweza kumudu viwanja vya bei hiyo?

(III) Kwa nini kusiwe na utaratibu kwenye Halmashauri ya mgao wa kuuza viwanja kwa zamu. Kama A alipata mgao uliopita na sasa ni zamu ya B kupata kiwanja na A asubiri baadaye?

(IV) Kwa nini maafisa ardhi wanahodhi viwanja lukuki na sio kwa nia ya kujenga bali baadaye wauze kwa bei ya juu na kuinyima serikali mapato?, Kiwanja cha milioni saba kinauzwa baadaye kwa milioni kumi na tano, lakini serikalini inarekodiwa imepokea Tshs. Milioni saba.

Sasa katika hali kama hii unategemea mwananchi wa kawaida ataweza kumudu kununua kiwanja kilichopimwa na serikali.
 
Nimesoma nusu ya maandishi uloyoandika naona niandike na kukujuza kuwa nchi nayo inasheria kama mtu unafanya kitu kwa kudharau sheria au kutokufata utaratibu na miaka nenda rudi wengi wao wanajua walikosea na wakaweka ugumu wa pesa kuhonga na wengine ugumu wa kudharau maana mengi yalikuwa hayafuatiliwi na sasa kwa hapa kazi tu wengi wanashukuru

Kama umeguswa na unataka nchi iende kiolela kama zamani basi ni bora kukaa kimya

Wengi hamna shukurani kwani wengi nao walio dhurumiwa mengiiii wote wakiandika kama wewe nchi itaenda wapi

Sheria ni sheria na mipango ya miji ipo sema ndio kudharau na kuweka ubishi.

Wenginwatakumbwa na mengi kila kona sio bomoa bomoa hivyo wakisamehewa wa bomoa nomoa na wengine nao wasamehewe na nchi iwe ya kuyoa msamaha kama vile kuonea huruma hiyo hapana

Naona bado naandika namaliza mengi hadi nisije yakoroga
 
Katika nchi maskini kama Tanzania naamini kabisa kiongozi hatakiwi kufanya decision bila kutizama hali halisi ya wananchi. Mfano katika siku za karibuni kumekuwa na maamuzi ambayo kwa kweli ni magumu hasa ukizingatia yanagusa moja kwa moja tabaka la wananchi wa ngazi ya chini.

Mfano tu kuna hili suala la bomoa bomoa ambalo naona kama limeshika kasi. Nisingependa kukosoa kwani kuna sababu stahiki za bomoa bomoa lakini wasiwasi wangu ni kwamba zoezi linaenda katika hali ambayo kwa namna moja inawaacha raia walengwa katika ugumu fulani wa maisha.

Ningetoa Rai yangu kwa Magufuli na watekelezaji sera wake " Hii ni Tanzania na ni moja wapo ya nchi masikini ambayo pia raia wake wengi hawana elimu kwa hiyo basi ingepaswa maamuzi kama haya yawe yanawashirikisha walengwa badala ya kuvamia tu na matingatinga na kuanza kuvunja nyumba za raia"

Mh Rais hii nchi yetu bado changa na huwezi tu ukafuata sheria bila kuangalia uhalisia wa maisha ya wananchi. Hapo tutakuwa hatujengi bali tunabomoa. Naelewa vema azma yako ya kuipatia maendeleo nchi hii lakini kuna sehemu nyingine lazima tuende kwa speed ya ki pwani pwani maana tukienda kwa speed ya ki London London ni wazi utaumiza wengi.

Hata hii hatua ya kubomoa nyumba za watu zenye thamani kubwa na mahoteli kwa dhana kwamba eti wamejenga kwenye viwanja vya wazi hilo nalo nna mashaka nalo maana jenzi zozote zinapata vibali kutoka halmashauri husika. Kwa hiyo kama ni tatizo saa nyingine halipo kwa raia bali kwa watendaji wa serikali wenyewe.

Mi sitaki kuamini kuanza ku deal na bomoa bomoa kwa kipindi hiki kutanufaisha wananchi walio wengi. Nadhani kuna mambo mengi ya kufanya kwa sasa. Hata na hivo bomoa bomoa haikuwa kwenye ilani ya CCM.

Halafu tangu uchaguzi uishe naona harakati za kisiasa na kazi za serikalini ni Dar es salaam tu, ina maana mikoa mingine sio sehemu ya Tanzania? Mara muhimbili hospital mara sijui wap wap.. yaani Dar tu. Tabora nayo ni Tanzania na kuna shida nako kweli kweli..

No offence,, namkubali sana Rais ila kuna mambo yananipa ukakasi na lazima niandike.


kama bomoa bomoa iko kinyume na sheria au iko kisheria lakini atekelezaji wanatenda isivyo, basi hoja yako ina mashiko lakini kama ni kinyume kwamba wafanyacho ndicho kinachostahili kufanywa kwa kuwa kina matokeo bora kwa taifa, hatupaswi kule sympathy kwa kigezo cha wanaohusika ni masikini au nchi hii bado ni masiki, au watu waliuziwa viwanja na halmashauri; hiyo si hoja ya kujenga. tumefika hapa tulipo kwa huruma na uzembe wa namna hiyo.
 
Katika nchi maskini kama Tanzania naamini kabisa kiongozi hatakiwi kufanya decision bila kutizama hali halisi ya wananchi. Mfano katika siku za karibuni kumekuwa na maamuzi ambayo kwa kweli ni magumu hasa ukizingatia yanagusa moja kwa moja tabaka la wananchi wa ngazi ya chini.

Mfano tu kuna hili suala la bomoa bomoa ambalo naona kama limeshika kasi. Nisingependa kukosoa kwani kuna sababu stahiki za bomoa bomoa lakini wasiwasi wangu ni kwamba zoezi linaenda katika hali ambayo kwa namna moja inawaacha raia walengwa katika ugumu fulani wa maisha.

Ningetoa Rai yangu kwa Magufuli na watekelezaji sera wake " Hii ni Tanzania na ni moja wapo ya nchi masikini ambayo pia raia wake wengi hawana elimu kwa hiyo basi ingepaswa maamuzi kama haya yawe yanawashirikisha walengwa badala ya kuvamia tu na matingatinga na kuanza kuvunja nyumba za raia"

Mh Rais hii nchi yetu bado changa na huwezi tu ukafuata sheria bila kuangalia uhalisia wa maisha ya wananchi. Hapo tutakuwa hatujengi bali tunabomoa. Naelewa vema azma yako ya kuipatia maendeleo nchi hii lakini kuna sehemu nyingine lazima tuende kwa speed ya ki pwani pwani maana tukienda kwa speed ya ki London London ni wazi utaumiza wengi.

Hata hii hatua ya kubomoa nyumba za watu zenye thamani kubwa na mahoteli kwa dhana kwamba eti wamejenga kwenye viwanja vya wazi hilo nalo nna mashaka nalo maana jenzi zozote zinapata vibali kutoka halmashauri husika. Kwa hiyo kama ni tatizo saa nyingine halipo kwa raia bali kwa watendaji wa serikali wenyewe.

Mi sitaki kuamini kuanza ku deal na bomoa bomoa kwa kipindi hiki kutanufaisha wananchi walio wengi. Nadhani kuna mambo mengi ya kufanya kwa sasa. Hata na hivo bomoa bomoa haikuwa kwenye ilani ya CCM.

Halafu tangu uchaguzi uishe naona harakati za kisiasa na kazi za serikalini ni Dar es salaam tu, ina maana mikoa mingine sio sehemu ya Tanzania? Mara muhimbili hospital mara sijui wap wap.. yaani Dar tu. Tabora nayo ni Tanzania na kuna shida nako kweli kweli..

No offence,, namkubali sana Rais ila kuna mambo yananipa ukakasi na lazima niandike.
Amri ya kubomoa haijaanza kutolewa na Magufuli , Rais mpendwa JK alipotembelea mafuriko ya Dar alitoa amri ya Nyumba zote zilizojaa maji kubomolewa.


Hizo Nyumba ni lazima zibomolewe tu no way ,ukitaka kuona hilo subiri mvua inyeshe uone watu Wa Mabondeni wanavyosombwa na mafuriko.



NB. Nyinyi chagadema mtupishe tufanye kazi.
 
Watu wanalaumu na kuwakebehi watu wa mabondeni lakini hawajuhi watu hawa wapo katika hali gani.

Ukweli ni kwamba hakuna mtu hata mmoja anayependa kupata matatizo kwa kujitakia.

Na tumekuwa wa kwanza kuwanyoshea vidole kwamba wahame mabondeni tu lakini hatujagusa sababu kuu ya watu kujenga mabondeni, ni sawa na kuua mbu lakini tukiacha masalia ya mbu salama, Hakika mbu watarudi tena.

Na mamlaka husika hawana nia ya kusikiliza na kutatua matatizo labda kwa kujua wao ndio chanzo kikuu cha tatizo au ubabe usiokuwa wa manufaa hebu fikiri nyumba elfu nane zinavunjwa, hivi familia husika zitakaa wapi na hili ndio tatizo kubwa. Je hawa watu watakaa wapi kwa muda huu ambao wanatafuta makazi mapya??, na Je serikali imejiandaa vipi?

Nikirudia kwenye hoja ya msingi ni kwamba watu wanajenga mabondeni kwa sababu zifuatazo:

(I) Hebu tujiulize wakina nani wanapata viwanja mara Halmashauri inapotangaza uuzaji wa viwanja vipya?, Kama ujakuta wanaopata ni watu wale wale, na kwa nini hali hii inajirudia?.

(II) Tujiulize je vipato vya wakazi wengi wa mabondeni vinawawezesha kupata viwanja vinavyouzwa na Halmashauri ya mijini hapa Dar - es - Salaam, Kwa mfano wilaya ya Kinondoni walitoa viwanja Mabwe Pande kama wiki mbili zilizopita, Na vilikuwa vinauzwa Tshs. 12,000.00 kwa mita ya mraba. Kwa mahitaji ya ya uwanja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya kawaida, Mita za mraba 500 ingegharimu Tshs. 6,000,000.00
( Milioni sita). Swali tena wangapi wanaweza kumudu viwanja vya bei hiyo?

(III) Kwa nini kusiwe na utaratibu kwenye Halmashauri ya mgao wa kuuza viwanja kwa zamu. Kama A alipata mgao uliopita na sasa ni zamu ya B kupata kiwanja na A asubiri baadaye?

(IV) Kwa nini maafisa ardhi wanahodhi viwanja lukuki na sio kwa nia ya kujenga bali baadaye wauze kwa bei ya juu na kuinyima serikali mapato?, Kiwanja cha milioni saba kinauzwa baadaye kwa milioni kumi na tano, lakini serikalini inarekodiwa imepokea Tshs. Milioni saba.

Sasa katika hali kama hii unategemea mwananchi wa kawaida ataweza kumudu kununua kiwanja kilichopimwa na serikali.


Huwa Hauoni watu Wa mabondeni wanavyokufa na mafuriko .



Watu Wa jangwani wakisombwa na mafuriko wewe ndio Wa kwanza kulaumu serikali.


Chadema mlishashindwa kaeni pembeni wanaume wafanye kazi
 
Last edited by a moderator:
Pimbi wewe,

Huwa Hauoni watu Wa mabondeni wanavyokufa na mafuriko .



Watu Wa jangwani wakisombwa na mafuriko wewe ndio Wa kwanza kulaumu serikali.


Chadema mlishashindwa kaeni pembeni wanaume wafanye kazi
Watu wa ajabu sana hao, na kweli mafuriko yakija wanaanza ilaumu serikali. Hivi hata kwa macho tu mtu huwezi kuona kwamba hapo unapojenga ni bonde/njia ya maji??!!
Akili zetu Waafrika ni mbovu kabisa. Shwain
 
Watu wa ajabu sana hao, na kweli mafuriko yakija wanaanza ilaumu serikali. Hivi hata kwa macho tu mtu huwezi kuona kwamba hapo unapojenga ni bonde/njia ya maji??!!
Akili zetu Waafrika ni mbovu kabisa. Shwain
 
Back
Top Bottom