Mimi nina Airtel Home WIFI Router, hii ni router inayotumia line ya Airtel pekee. Mahali ninapoishi hivi sasa hakuna mtandao wa 3G kwa Airtel na hivyo kufanya Router yangu kukosa msaada niliokuwa nauhitaji.
Je naweza nikaibadili ili niweze kutumia line yoyote!?
Airtel home wifi ndo kitu gani?
Sema Manufacturer na Model na sema ukiweka line nyingine inakwambia nini?
Its worthy noting kwamba hapa Modem/router zinatambulika kwa vitu viwili vya maingi nilivovitaja hapo juu.
Na ili ujue inatoka vipi Lock lazima useme ujumbe unaopewa ukiweka line ya kigeni.
Njia Pekee zilizopo za Ku Unlock modem/Router za Bure zinazojulikana nazo ni
1) Iwapo modem/Router IMEI inaanza na 35 na inaomba NCK codes basi utaenda a-zgsm.com utatia IMEI na utapewa hizo codes
2)Iwapo Modem ina Customized Firmware.
Basi hapa lazima na wewe uchangamshe akili kutafuta Firmware iwapo firmware yake haijawai kuwa verified na users wa hapa kwetu,Modem zenye Firmware zinazojulikana ni E173,E153,E303,E3131 na modem mpya za Tigo 3G za 42Mbps if not mistaken ni E3531.
Kama Firmware ya Modem yako haijulikana hapa napo utaongia Cost ya kulipia Hi-Silicon Firmware writer inamilikiwa na DC-Unlocker na watakupa Firmware ambayo ina format ya .dgtk ambayo hauwezi itumia bila kulipia hiyo Tool yao.
3)Modem/router zenye IMEI inayoanza na 86 na zinaomba NCK codes pia lazima ujipange.
4)Modem/Router mpya za ZTE hizo ujanja wake haupati kwingine bila kulipa DC-Unlocker na bei yake sio chini ya 7£
Hivo watu inabidi wawe makini unapoenda kukimbilia kununua Modem/Router Jua kwanza kama inatoka Lock au utakua Umechagua kufunga Ndoa ya kikristo na hicho kifaa cha mtandao wako maana modem nyingine hazina hata walau solution ya kulipia e.g ZTE 6601 ya Halotel