"Na sauti ifanye ringtone..."

"Na sauti ifanye ringtone..."

Vodka

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
906
Reaction score
96
Siku moja mchaga alikwenda soko la mbuzi,vingunguti na kununua mbuzi. Kabla ya kumchinja mbuzi yule kabla ya kitoweo,akamuachia maagizo mchinjaji na mpishi;
"Ukisha mchija kwanya damu tengeneza kisurio,Nyama nusu ipikie pilau na nyingine itie kwenye jokofu,kichwa kichemshe tupate supu na miguu miguu tengeneza mchuzi chukuchuku.Ngozi usiitupe tutafanya msala kwani Tarimo anaitaka kununua ili kutowa posa si unajua anataka kuoa huko Tanga..Utumbo usafishe na utunze kwa ajili ya kupikia ndizi jioni na mifupa itakayo patikana pia.Na hakikisha baada ya kula mifupa tutawauzia wenye mbwa,kinyesi kihifadhi kwani tumejipatia mbolea ya bustani". Mpishi naye akauliza ".Hutaki na sauti ya mbuzi tuifanye 'ring tone' kwenye simu yako?" Jamaa akajibu "Sikujua kama unaakili namna hiyo massawe,fanya ivyo basi".
 
Je unaweza ukampangia mbuzi namna hiyo?
 
Kama ni bajeti hii sasa ni vunja rekodi duuuu,subiri waje wahusika kina mangi waone
 
Man who fight with wife all day get no piece at night.

Lakini mbona lakini sifa hizi za Kipare, kwanini unasema mchaga wakati unajua mchaga si bahiri kihivyo?
 
Man who fight with wife all day get no piece at night.
Lakini mbona lakini sifa hizi za Kipare, kwanini unasema mchaga wakati unajua mchaga si bahiri kihivyo?
polee kumbe imeku touch!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom