Aende Kisarawe aniambie kuwa ni uwongo kuwa raia hawakuhamishwa ili mzungu anayelima jathropa apate ardhi. Kuna mkazi mmoja alikuwa akijiendeshea biashara yake ya mkaa pale akipata pato la dola 150 kwa mwezi ( si haba) na baada ya mzungu kuchukua ardhi yake na kumwajiri analipwa sasa dola 50 kwa mwezi. Je, ni maendeleo hayo?