Mzee Kikwete, leo ndiyo leo; msituangushe

Mzee Kikwete, leo ndiyo leo; msituangushe

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
34,776
Reaction score
46,050
Mh. Rais mstaafu Jakaya Kikwette tunayo matumaini makubwa kwenu kuwa ule muda ambao taifa hili limeusubiri mno hatimaye umewadia.

Ni wazi kuwa kila mtu katika nchi hii angalipendelea tuishi sote kwa usawa na haki. Utashi wa viongozi wa juu katika kufanikisha hayo ni jambo la muhimu sana.

Kufanya maamuzi magumu yatakayorejesha imani ya wananchi kwa nchi yao itakuwa jambo la msingi mno kwa sasa labda kuliko jambo lolote lile.

Pana watu wakiwamo watia nia wengi waliojaribu kuutaka urais na kura kuwa hazikutosha hali nafasi ni moja wakiwamo akina:

1. Asha Rose Migiro
2. Mzee Mwandosya
3. Bernard Membe
4. Mizengo Pinda
5. Frederick Sumaye
6. Edward Lowassa
7. Abdulhaman Kinana
8. Philip Mangula
9. Anna Mghwira
10. Dkt. Slaa
11. Dkt. Nchimbi
12. Nk nk

Watu ambao hawakuwamo ndani ya establishment ya sasa au wale waliokuwa na maoni tofauti kuhusiana na establishment ya sasa kwa hakika wangetufaa sana.

JK tupeni raha kwa kuandaa mustakabala mwema utakaotuletea mwanzo mpya.
 
Tunataka atakae shikilia pale alipoishia magufuri, tulisha zoea kuchapa kazi tulisha zoea kulipa kodi, teyar tunajua sisi ni matajiri na vijana wamejityuni kukaa na kuchapa kazi hivyo hatutaki kurudi nyuma tunahitaji atakae tupeleka mbele zaidi na Sio kurudi nyuma
 
Baada ya kumaliza kusoma nimejikuta nimekasirika Sana kuona upeo wako wa hali ya chini hivi na nyumbani unategemewa Kama kibaba
emoji848.png
emoji34.png
 
Tunataka atakae shikilia pale alipoishia magufuri, tulisha zoea kuchapa kazi tulisha zoea kulipa kodi, teyar tunajua sisi ni matajiri na vijana wamejityuni kukaa na kuchapa kazi hivyo hatutaki kurudi nyuma tunahitaji atakae tupeleka mbele zaidi na Sio kurudi nyuma

Tunataka mwanzo mpya. Utakaotambua nchi ni yetu sote. Utakaotambua tuna janga la Corona. Utakaotambua katiba mpya ni agenda yetu muhimu.

Mwanzo utakaotambua maendeleo ya watu nayo ni muhimu tena zaidi ya maendeleo ya vitu.
 
Naamini Raisi samia nikiongozi shupavu sana ataleta makamu wa Raisi mchap kazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom