Mzanzibari ni nani?

Mzanzibari ni nani?

Mtu yeyote Mtanzania ana haki Zote zanzibar, ile ili uwe na Kadi ZAN-ID japo uwe umeishi miaka 5 Zanzibar, kwa sasa Wachaga, Wasukumu, Wamasa, Wageni na makabila mengi ya Tanzania washachukua

Hata waje wote watanganyika kuchukua zan-id ukweli utabaki tu hakuna mzanzibar mkristo.
 
Hivi visiwa ni shida tupu. Kuna kiongozi kutoka Zanzibar aliwahi kuwaambia Wazanzibar kuwa 'vichwa/akili kama samaki'. Hiyo kauli naikumbuka,aliyesema nimemsahau.

Amaan Abeid Karume. Rais Mstaaf wa Znz aliitoa kuwambia ccm kizota Dodoma.
 
kila siku tunasikia "wazanzibari" wanadai hiki na kile, hususani kwenye katiba mpya, je wazanzibari ni kina nani hasa? Tuzingatie mifano kama: Rais ali hasan mwinyi kazaliwa bagamoyo lakini ni mzanzibari, Dr shein mzaliwa wa pemba ni mzanzibari, Mmasai, mchaga au "mbara" yoyote atayehamia zanzibar na kukaa miaka kadhaa naye anapewa uzanzibari (kama rais mwinyi).
Hivi mpemba aliyezaliwa bara na kukulia bara anaweza kuwa mzanzibari automatically tu kwa sababu babu yake alizaliwa zanzibar? au yeye atakuwa mbara?
Na je mbara aliyehamia zanzibar akawa mzanzibari (kisheria), akirudi bara na kuzaa watoto, hawa "wanyamwezi" nao watakuwa wazanzibari vile vile? Naomba tusaidiane.

Mwinyi sio mzanzibar, hujakosea amekulia tu zanzibar. Mzanzibar ni yule ambae amezaliwa zanzibar au nje ya zanzibar ispokuwa wazee wazanzibari.
 
Aggrey Morris Ambrose eti nae ni Mzenji wakati kazaliwa Songea mkoani Ruvum
 
kila siku tunasikia "wazanzibari" wanadai hiki na kile, hususani kwenye katiba mpya, je wazanzibari ni kina nani hasa? Tuzingatie mifano kama: Rais ali hasan mwinyi kazaliwa bagamoyo lakini ni mzanzibari, Dr shein mzaliwa wa pemba ni mzanzibari, Mmasai, mchaga au "mbara" yoyote atayehamia zanzibar na kukaa miaka kadhaa naye anapewa uzanzibari (kama rais mwinyi).
Hivi mpemba aliyezaliwa bara na kukulia bara anaweza kuwa mzanzibari automatically tu kwa sababu babu yake alizaliwa zanzibar? au yeye atakuwa mbara?
Na je mbara aliyehamia zanzibar akawa mzanzibari (kisheria), akirudi bara na kuzaa watoto, hawa "wanyamwezi" nao watakuwa wazanzibari vile vile? Naomba tusaidiane.

Wakubwa Shkamooni na Wadogo Habar zenu.



Ubaguzi ama wa rangi, dini, kabila au hata jinsia (Gender) ni tatizo kubwa katika sehemu nyingi ulimwenguni. Tatizo hili huanza taratibu kwa kupandikiza mbegu fulani katika jamii na baadae huota mizizi isiyon'goleka.

Kubagua kundi moja kutokana na kundi jengine ndani ya jamii moja ni dhambi isiyovumilika hata kidogo kwa vile inapoachwa kuendelea madhara yake ni makubwa mno mfano mzuri ni mauaji ya Burundi na Rwanda mwaka 1994

Kuzungumzia nani Mzanzibari si jambo baya ikiwa lengo lake ni kuweka historia juu ya jamii unavyobadilika kulingana na wakati lakini inapofika mahali ikawa kwamba lengo ni kueleza kwamba kundi fulani ndio lina haki kwa vile ndio asilia na fulani halina kwa vile sio asili hapo itakuwa mzungumzaji halengi kuelimisha bali kujenga chuki baina yetu. Mzanzibari ni Mzanzibari iwe asili ni Ngazija, Tumbatu, India, Somali, Oman au Tanganyika.

Tunalazimika kuondokana na mawazo kwamba kundi moja ni bora zaidi au lina haki zaidi ya kundi jengine kwa namna yoyote ile ndipo tutaweza kuondokana na ubaguzi wa rangi, kabila, dini au jinsia (Gender)

Tusighadhibike sana anapotokea mbaguzi na kuandika mawazo yake, kwani naye ana haki sawa na wengine katika kutoa mawazo (Freedom of Expression) ila tunawajibika kumjibu tena kwa kutumia diplomasia ya hali ya juu, kwani ikiwa anaeleta ubaguzi ni mwenye akili timamu basi huenda ataelemika kwa njia hiyo.

Tunapoghadhibika na kuanza kumshambulia mwandishi badala ya kujibu maandishi hapo ndipo nidhamu ya kielimu (Academic discipline) inapotea na hivyo kupoteza dhana nzima ya kuelimishana.

Uislamu ndio njia bora ya kuondokana na haya kwa vile umepiga vita wazi wazi mambo yote yanayopelekea kwenye ubaguzi. M/Mungu mwenyewe anatueleza sababu ya msingi ya kuwatofautisha wanadamu kimaumbile na ni yupi ni mbora mbele yake katika Qur-an kama ifuatavyo :-

"Enyi watu! Hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamme (mmoja, Adam) na mwanamke (mmoja, Hawa). Na tukakufanyeni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika anaeheshimiwa sana miongoni mwenu mbele ya M/Mungu ni yule amchae M/Mungu zaidi . Kwa hakika M/Mungu ni mjuzi na mwenye habari" (49.13)

Kwa hiyo kupoteza muda kujadili ni nani Mzanzibari hasa au asilia au mwenye haki fulani kuliko mwingine ni jambo ambalo kimsingi halina faida yoyote kwa Wananeti wa JF na Watanzania wote kwa ujumla.

Ewe Mola wetu tupe uwezo wa kuchambua kiyakinifu. Amin.
 
mke wangu anamimba nataka aende akajifungulie zanzibar;
je mtoto akizaliwa atakuwa mzanzibar????

atajifungulia bandarini inshaallah kabla hajaingia botini kuelekea nchi yetu ya ahadi
 
Wakubwa Shkamooni na Wadogo Habar zenu.



Ubaguzi ama wa rangi, dini, kabila au hata jinsia (Gender) ni tatizo kubwa katika sehemu nyingi ulimwenguni. Tatizo hili huanza taratibu kwa kupandikiza mbegu fulani katika jamii na baadae huota mizizi isiyon'goleka.

Kubagua kundi moja kutokana na kundi jengine ndani ya jamii moja ni dhambi isiyovumilika hata kidogo kwa vile inapoachwa kuendelea madhara yake ni makubwa mno mfano mzuri ni mauaji ya Burundi na Rwanda mwaka 1994

Kuzungumzia nani Mzanzibari si jambo baya ikiwa lengo lake ni kuweka historia juu ya jamii unavyobadilika kulingana na wakati lakini inapofika mahali ikawa kwamba lengo ni kueleza kwamba kundi fulani ndio lina haki kwa vile ndio asilia na fulani halina kwa vile sio asili hapo itakuwa mzungumzaji halengi kuelimisha bali kujenga chuki baina yetu. Mzanzibari ni Mzanzibari iwe asili ni Ngazija, Tumbatu, India, Somali, Oman au Tanganyika.

Tunalazimika kuondokana na mawazo kwamba kundi moja ni bora zaidi au lina haki zaidi ya kundi jengine kwa namna yoyote ile ndipo tutaweza kuondokana na ubaguzi wa rangi, kabila, dini au jinsia (Gender)

Tusighadhibike sana anapotokea mbaguzi na kuandika mawazo yake, kwani naye ana haki sawa na wengine katika kutoa mawazo (Freedom of Expression) ila tunawajibika kumjibu tena kwa kutumia diplomasia ya hali ya juu, kwani ikiwa anaeleta ubaguzi ni mwenye akili timamu basi huenda ataelemika kwa njia hiyo.

Tunapoghadhibika na kuanza kumshambulia mwandishi badala ya kujibu maandishi hapo ndipo nidhamu ya kielimu (Academic discipline) inapotea na hivyo kupoteza dhana nzima ya kuelimishana.

Uislamu ndio njia bora ya kuondokana na haya kwa vile umepiga vita wazi wazi mambo yote yanayopelekea kwenye ubaguzi. M/Mungu mwenyewe anatueleza sababu ya msingi ya kuwatofautisha wanadamu kimaumbile na ni yupi ni mbora mbele yake katika Qur-an kama ifuatavyo :-

"Enyi watu! Hakika tumekuumbeni (nyote) kwa (yule) mwanamme (mmoja, Adam) na mwanamke (mmoja, Hawa). Na tukakufanyeni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika anaeheshimiwa sana miongoni mwenu mbele ya M/Mungu ni yule amchae M/Mungu zaidi . Kwa hakika M/Mungu ni mjuzi na mwenye habari" (49.13)

Kwa hiyo kupoteza muda kujadili ni nani Mzanzibari hasa au asilia au mwenye haki fulani kuliko mwingine ni jambo ambalo kimsingi halina faida yoyote kwa Wananeti wa JF na Watanzania wote kwa ujumla.

Ewe Mola wetu tupe uwezo wa kuchambua kiyakinifu. Amin.

Asante sana kwa ustaarabu wako, ni mara chache sana watu wanaongea kwa utaratibu kama wewe kwenye mijadala hii ya zanzibar.
Swali langu lisikutie hofu, lengo hapa si ubaguzi. Lengo langu ni kutafuta uhalali wa mtu kuwa mzanzibari baada ya miaka 50 ya muungano. Hoja yangu ni kuwa uzanzibari kamili ulikufa kama ambavyo utanganyika ulikufa. Hivyo leo hii hakuna mtu mwenye haki ya kujiita "mzanzibari" akimaanisha raia wa zanzibar.
 
Mwinyi sio mzanzibar, hujakosea amekulia tu zanzibar. Mzanzibar ni yule ambae amezaliwa zanzibar au nje ya zanzibar ispokuwa wazee wazanzibari.

lakini amekaa zanzibar miaka zaidi ya kumi, huyo si mzanzibari kisheria.
 
Asante sana kwa ustaarabu wako, ni mara chache sana watu wanaongea kwa utaratibu kama wewe kwenye mijadala hii ya zanzibar.
Swali langu lisikutie hofu, lengo hapa si ubaguzi. Lengo langu ni kutafuta uhalali wa mtu kuwa mzanzibari baada ya miaka 50 ya muungano. Hoja yangu ni kuwa uzanzibari kamili ulikufa kama ambavyo utanganyika ulikufa. Hivyo leo hii hakuna mtu mwenye haki ya kujiita "mzanzibari" akimaanisha raia wa zanzibar.

Mzanzibar ni MTU yoyote.ambae wazazi wake au yeye mwenyewe alikuwepo Zanzibar kabla ya Mapinduzi 1964.
 
Mzanzibar ni MTU yoyote.ambae wazazi wake au yeye mwenyewe alikuwepo Zanzibar kabla ya Mapinduzi 1964.

lakini sheria si inaruhusu kwa wasio na masharti hayo kupata uzanzibari huu wa ukazi wa miaka kadhaa?
 
Mzazibari maana yake ni mtu mlalamikaji, maneno mengiii, kila saa anajiona anaonewa na asie na msimamo!

Just read your post Have -to tell you that you are very sick,more annoyed,at being filed under,no further action
 
Asante sana kwa ustaarabu wako, ni mara chache sana watu wanaongea kwa utaratibu kama wewe kwenye mijadala hii ya zanzibar.
Swali langu lisikutie hofu, lengo hapa si ubaguzi. Lengo langu ni kutafuta uhalali wa mtu kuwa mzanzibari baada ya miaka 50 ya muungano. Hoja yangu ni kuwa uzanzibari kamili ulikufa kama ambavyo utanganyika ulikufa. Hivyo leo hii hakuna mtu mwenye haki ya kujiita "mzanzibari" akimaanisha raia wa zanzibar.
"kwa hiari au lazima? tatizo sisi waZanzibari hatupo tayari kuupoteza utaifa wetu ulioukuwepo na ambao tunaupigania sasa. kwetu sisi uZanzibari unakuja mwanzo kuliko uTanzania, (Tanzania = Tanganyika0. Najisikia kichefuchefu sana passport yangu imebeba jina la Tanzania ... japo mara nyingi kwa kila nimuoneshae hujifariji kwa kumsisitiza aangalie "issued by PCO ZANZIBAR". wakati Karume anaungana na Nyerere waZanzibari wazee wetu walikuwa na kadi zao za uraia ... leo ati tuna :ZanID.. ambayo CCM wanaitumia kuwapa mamluki kuwasaidia kwenye kupiga kura! ...
 
"kwa hiari au lazima? tatizo sisi waZanzibari hatupo tayari kuupoteza utaifa wetu ulioukuwepo na ambao tunaupigania sasa. kwetu sisi uZanzibari unakuja mwanzo kuliko uTanzania, (Tanzania = Tanganyika0. Najisikia kichefuchefu sana passport yangu imebeba jina la Tanzania ... japo mara nyingi kwa kila nimuoneshae hujifariji kwa kumsisitiza aangalie "issued by PCO ZANZIBAR". wakati Karume anaungana na Nyerere waZanzibari wazee wetu walikuwa na kadi zao za uraia ... leo ati tuna :ZanID.. ambayo CCM wanaitumia kuwapa mamluki kuwasaidia kwenye kupiga kura! ...

kwa hiyo kimsingi tumekubaliana kuwa taifa la zanzibar halipo tena.
 
kila siku tunasikia "wazanzibari" wanadai hiki na kile, hususani kwenye katiba mpya, je wazanzibari ni kina nani hasa? Tuzingatie mifano kama: Rais ali hasan mwinyi kazaliwa bagamoyo lakini ni mzanzibari, Dr shein mzaliwa wa pemba ni mzanzibari, Mmasai, mchaga au "mbara" yoyote atayehamia zanzibar na kukaa miaka kadhaa naye anapewa uzanzibari (kama rais mwinyi).
Hivi mpemba aliyezaliwa bara na kukulia bara anaweza kuwa mzanzibari automatically tu kwa sababu babu yake alizaliwa zanzibar? au yeye atakuwa mbara?
Na je mbara aliyehamia zanzibar akawa mzanzibari (kisheria), akirudi bara na kuzaa watoto, hawa "wanyamwezi" nao watakuwa wazanzibari vile vile? Naomba tusaidiane.

mzanzibari ni pandu ameir kificho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom