Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
M/kiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Tanzania akiwa anaingia kwenye kikao cha NEC ya tarehe 11 June, whitehouse Dodoma na kushuhudia maajabu akatamka "HAIJAPATA KUTOKEA"
Waacheni watanzania wapigwe na butwaa, waacheni wajae kwenye mikutano yake wakimshangaa kwani HAIJAPATA KUTOKEA ktk historia ya Tanzania na Afrika.
Ni vigumu sana kwa MYAHUDI kuswalisha katika msikiti wa WAISLAMU, kama ilivyokuwa kwa KIONGOZI wa CUF kuisimamia ILANI ya TLP, lakini wapo wayahudi kadhaa wamewahi kufanya hivyo.
Kwa kawaida watu hununua wanasiasa, wakawatumia kwa maslahi yao, kuwasemea ajenda zao, nasema ni kawaida kwa sababu inatokea siku zote na tumeyashuhudia yakitokea, hivyo kwangu ama kwetu ni kawaida wanasiasa kununuliwa.
Lakini katika historia ya Tanzania na Afrika ni MZEE WA KIBO pekee, ndio aliyeweka historia ya kununua CHAMA CHA SIASA kizima kizima, na hakuishia hapo akanunua na MUUNGANO wa vyama vya siasa ili asimame kama mgombea, na amefanikiwa.....nasema kama alivyosema JAKAYA, haijapata kutokea.
Historia hii ya kipekee ilitanguliwa na mtu mmoja tu, anaitwa GIOVANNI LEONE, ambaye alikuwa Kiongozi wa Chama cha Wakristo cha Italy ( DEMOCRAZIA CRISTIANA ama CHRISTIAN DEMOCRACY) ambaye HAKUWAHI kuwa mkristo., lakini aliweka historia ya kuwa kiongozi wa Wakristo ambaye hakuwa Mkristo.
Bwana huyu aliingia madarakani kama WAZIRI MKUU- tarehe 21 June 1963 na kujiuzulu miezi sita baadae tarehe 4 December 1963 kwa kashfa ya Ufisadi.
Mwaka 1968, aliingia tena madarakani baada ya kununua MUUNGANO WA VYAMA VYA UPINZANI ITALY ulioitwa THE PENTAPARTITO ambao uliundwa na vyama vitano kikiwemo PSI, PSDI, PRI, PLI na DC.
LAKINI kama wasemavyo waswahili jasiri haachi asili, Bwana LEONE alidumu madarakani kwa miezi sita tena kwa maana kuanzia tarehe 24 June - 22 Dec 1968 pale ambapo BUNGE lilimuondoa kutokana na matumizi mabaya ya nafasi yake kama Waziri Mkuu wa Italy.
Ni kama GIOVANNI LEONE, EDWARD NGOYAI LOWASSA ameamua kufuata nyazo zake, kitabia na mwenendo wake kisiasa. Itakuwa vigumu kwa LOWASSA kufuata misingi hasiyoijua ya UKAWA, na vigumu kutekeleza ILANI hasiyoijua wala kushiriki kuiandaa na itakuwa vigumu kwake KUAMINI ktk UKAWA ama CHADEMA kwani kwake Chama hicho ni Mama wa Kambo.
Mimi ninabaki na mshangao kama vile watanzania wenzangu wanavyoendelea kumshangaa LOWASSA...HAIJAPATA KUTOKEA kada kindaki ndaki wa CCM kuwa JEMEDARI wa wapinzani...ONLY IN TANZANIA.
Waacheni watanzania wapigwe na butwaa, waacheni wajae kwenye mikutano yake wakimshangaa kwani HAIJAPATA KUTOKEA ktk historia ya Tanzania na Afrika.
Ni vigumu sana kwa MYAHUDI kuswalisha katika msikiti wa WAISLAMU, kama ilivyokuwa kwa KIONGOZI wa CUF kuisimamia ILANI ya TLP, lakini wapo wayahudi kadhaa wamewahi kufanya hivyo.
Kwa kawaida watu hununua wanasiasa, wakawatumia kwa maslahi yao, kuwasemea ajenda zao, nasema ni kawaida kwa sababu inatokea siku zote na tumeyashuhudia yakitokea, hivyo kwangu ama kwetu ni kawaida wanasiasa kununuliwa.
Lakini katika historia ya Tanzania na Afrika ni MZEE WA KIBO pekee, ndio aliyeweka historia ya kununua CHAMA CHA SIASA kizima kizima, na hakuishia hapo akanunua na MUUNGANO wa vyama vya siasa ili asimame kama mgombea, na amefanikiwa.....nasema kama alivyosema JAKAYA, haijapata kutokea.
Historia hii ya kipekee ilitanguliwa na mtu mmoja tu, anaitwa GIOVANNI LEONE, ambaye alikuwa Kiongozi wa Chama cha Wakristo cha Italy ( DEMOCRAZIA CRISTIANA ama CHRISTIAN DEMOCRACY) ambaye HAKUWAHI kuwa mkristo., lakini aliweka historia ya kuwa kiongozi wa Wakristo ambaye hakuwa Mkristo.
Bwana huyu aliingia madarakani kama WAZIRI MKUU- tarehe 21 June 1963 na kujiuzulu miezi sita baadae tarehe 4 December 1963 kwa kashfa ya Ufisadi.
Mwaka 1968, aliingia tena madarakani baada ya kununua MUUNGANO WA VYAMA VYA UPINZANI ITALY ulioitwa THE PENTAPARTITO ambao uliundwa na vyama vitano kikiwemo PSI, PSDI, PRI, PLI na DC.
LAKINI kama wasemavyo waswahili jasiri haachi asili, Bwana LEONE alidumu madarakani kwa miezi sita tena kwa maana kuanzia tarehe 24 June - 22 Dec 1968 pale ambapo BUNGE lilimuondoa kutokana na matumizi mabaya ya nafasi yake kama Waziri Mkuu wa Italy.
Ni kama GIOVANNI LEONE, EDWARD NGOYAI LOWASSA ameamua kufuata nyazo zake, kitabia na mwenendo wake kisiasa. Itakuwa vigumu kwa LOWASSA kufuata misingi hasiyoijua ya UKAWA, na vigumu kutekeleza ILANI hasiyoijua wala kushiriki kuiandaa na itakuwa vigumu kwake KUAMINI ktk UKAWA ama CHADEMA kwani kwake Chama hicho ni Mama wa Kambo.
Mimi ninabaki na mshangao kama vile watanzania wenzangu wanavyoendelea kumshangaa LOWASSA...HAIJAPATA KUTOKEA kada kindaki ndaki wa CCM kuwa JEMEDARI wa wapinzani...ONLY IN TANZANIA.