Mtela Mwampamba
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 537
- 347
Katika kumbukumbu zangu wakati najiunga na Chadema, kwa nguvu za ushawishi na hoja kutoka kwa kaka yangu, mwanasiasa makini na mwenye maono thabiti ya kesho yake na kesho ya watanzania walio wengi, kijana wa kanda ya magharibi mwa nchi hii Dr. Zuberi Zitto Ruyagwa, aliniambia kuwa
"..tunajenga chama hiki ili kiwe chama bora kitakacholeta maendeleo ya kweli kwa watanzania, ndugu zetu wamechoshwa na umasikini uliokithiri na hawana namna nyingine yeyote isipokuwa matumaini yao yapo juu yenu nyie vizazi vyao ili kuwakomboa kutoka katika umasikini wao, na njia pekee ni kwa kushiriki na kupata nguvu ya maamuzi na utawala.."
Akaendelea kwa kusema kuwa;
"..Chama chetu (CHADEMA) bado ni chama kichanga na hakina sura ya chama cha siasa, bado tu-wanaharakati, tunao wajibu kama vijana ndani ya chama hiki kuleta mabadiliko kwanza ndani ya Chama chetu kukifanya kuwa chama bora zaidi kitakacholeta matumaini mapya mioyoni mwa watanzania kisha tupate kuungwa mkono zaidi na tuweze kushinda chaguzi na kufanya maamuzi ya kimamlaka kama chama tawala, lakini hatutofika huko bila kuwa na SHABAHA, pamoja na mpango kazi wa kutimiza na kutekeleza shabaha yetu hiyo, sisi wana-chadema hatuna budi tukubali hali yetu ya ndani ya chama na hata nje, halafu tufanye bidii kuibadili hali hiyo ilingane na shabaha yetu.."
Mazungumzo haya tuliyafanya mwaka 2006, takribani miaka miaka tisa (9) iliyopita, nasikitika nikisema kuwa bado chadema ya leo haina shabaha wala muelekeo wa kutimiza shabaha hiyo, nasema na kwa ushahidi uliyo bayana kuwa chadema ya leo ni more worse kuliko ya miaka tisa iliyopita, wakati huo vijana walikuwa na matumaini at least ya kuleta mageuzi chanya ndani ya Chama chenyewe ili kiwe bora na imara kuweza kukitoa CCM madarakani, lakini leo hata hayo MATUMAINI kwa vijana ndani ya Chama yamekwishaondoka achilia mbali matumaini ya kuingia magogoni.
Lakini haya ndio matokeo ya kuruhusu akili ndogo kuongoza akili kubwa, ni jambo lisilowezekana kuwa form six failure yaani mtu aliyepata ZERO form six ajione mwenye maana na atake kudharau mawazo ya wengine wote na afuate mawazo yake pekee, kisha mawazo hayo yalete mafanikio na yazae matunda..HAIWEZEKANI.
Hakuna namna kuwa MAANDAMANO iwe ndio hoja ya siku zote, iwe ndio mfumo na shabaha ya kupima mafanikio ya Chama, yaani siku niliyokuwa nasikiliza mkutano mkuu wa Chama ilikuwa ni kama vile mtu anatania, anasema moja ya mafanikio ya Chama chao ni kuendesha maandamano, tena maandamano yaliyopoteza maisha ya watanzania, eti hayo ndio mafanikio, kama sio akili ndogo ni nini..?
Wakati mwingine ninapokumbuka dhamira, ari na kujitoa kwa dhati kutoka katika mioyo ya wazalendo wa kweli wa nchi hii katika kujaribu kukijenga chama hicho zilipozimwa na manyang'au na wapiga dili wa mjini waliokimbilia siasa kama njia ya "nitoke vipi" ni jambo linalokera na kutia uchungu.
Baada ya kumbukumbu hiyo fupi ya maisha yangu ndani ya Chadema, niseme kuwa nawatakiwa vijana wa Bavicha maandamano yatakayowaachia uchungu wasiousahau katika maisha yao.,kwani wajinga ndio waliwao...!!!
"..tunajenga chama hiki ili kiwe chama bora kitakacholeta maendeleo ya kweli kwa watanzania, ndugu zetu wamechoshwa na umasikini uliokithiri na hawana namna nyingine yeyote isipokuwa matumaini yao yapo juu yenu nyie vizazi vyao ili kuwakomboa kutoka katika umasikini wao, na njia pekee ni kwa kushiriki na kupata nguvu ya maamuzi na utawala.."
Akaendelea kwa kusema kuwa;
"..Chama chetu (CHADEMA) bado ni chama kichanga na hakina sura ya chama cha siasa, bado tu-wanaharakati, tunao wajibu kama vijana ndani ya chama hiki kuleta mabadiliko kwanza ndani ya Chama chetu kukifanya kuwa chama bora zaidi kitakacholeta matumaini mapya mioyoni mwa watanzania kisha tupate kuungwa mkono zaidi na tuweze kushinda chaguzi na kufanya maamuzi ya kimamlaka kama chama tawala, lakini hatutofika huko bila kuwa na SHABAHA, pamoja na mpango kazi wa kutimiza na kutekeleza shabaha yetu hiyo, sisi wana-chadema hatuna budi tukubali hali yetu ya ndani ya chama na hata nje, halafu tufanye bidii kuibadili hali hiyo ilingane na shabaha yetu.."
Mazungumzo haya tuliyafanya mwaka 2006, takribani miaka miaka tisa (9) iliyopita, nasikitika nikisema kuwa bado chadema ya leo haina shabaha wala muelekeo wa kutimiza shabaha hiyo, nasema na kwa ushahidi uliyo bayana kuwa chadema ya leo ni more worse kuliko ya miaka tisa iliyopita, wakati huo vijana walikuwa na matumaini at least ya kuleta mageuzi chanya ndani ya Chama chenyewe ili kiwe bora na imara kuweza kukitoa CCM madarakani, lakini leo hata hayo MATUMAINI kwa vijana ndani ya Chama yamekwishaondoka achilia mbali matumaini ya kuingia magogoni.
Lakini haya ndio matokeo ya kuruhusu akili ndogo kuongoza akili kubwa, ni jambo lisilowezekana kuwa form six failure yaani mtu aliyepata ZERO form six ajione mwenye maana na atake kudharau mawazo ya wengine wote na afuate mawazo yake pekee, kisha mawazo hayo yalete mafanikio na yazae matunda..HAIWEZEKANI.
Hakuna namna kuwa MAANDAMANO iwe ndio hoja ya siku zote, iwe ndio mfumo na shabaha ya kupima mafanikio ya Chama, yaani siku niliyokuwa nasikiliza mkutano mkuu wa Chama ilikuwa ni kama vile mtu anatania, anasema moja ya mafanikio ya Chama chao ni kuendesha maandamano, tena maandamano yaliyopoteza maisha ya watanzania, eti hayo ndio mafanikio, kama sio akili ndogo ni nini..?
Wakati mwingine ninapokumbuka dhamira, ari na kujitoa kwa dhati kutoka katika mioyo ya wazalendo wa kweli wa nchi hii katika kujaribu kukijenga chama hicho zilipozimwa na manyang'au na wapiga dili wa mjini waliokimbilia siasa kama njia ya "nitoke vipi" ni jambo linalokera na kutia uchungu.
Baada ya kumbukumbu hiyo fupi ya maisha yangu ndani ya Chadema, niseme kuwa nawatakiwa vijana wa Bavicha maandamano yatakayowaachia uchungu wasiousahau katika maisha yao.,kwani wajinga ndio waliwao...!!!