Mwizi wa viatu msikitini Mtwara akiona cha moto

Mwizi wa viatu msikitini Mtwara akiona cha moto

mangonjoli

Senior Member
Joined
Aug 29, 2012
Posts
154
Reaction score
110
Ijumaa ya leo Tarehe 4/10/2019 mwizi inayesemekana mzoefu wa wizi misikitini ilimkuta Arobaini yake baada ya kudakwa na waumini mkoani Mtwara katika msikiti mkubwa wa Sokoni.maeneo ya Soko kuu mtwara mjini.

Mwizi huyo aliyekamatwa na waumini waliomshtukia mapema akiwa katika harakati akiwa kashalivaa dundo ambalo sio lake. Alipobanwa alianza kubabaika na kuanza kukimbia ndipo alipokamatwa na waumini na kumpa kashikashi kidogo kabla ya kumuingiza ndani ya msikiti kwa usalama wake kabla ya Difenda ya polisi kufika eneo la tukio na kumchukua.

Mmoja wa Vijana waliomkamata alisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiibiwa mpaka kuamua kuweka mtego uliofyatuka ijumaa ya leo Nimekuwekea video ya Tukio hapo chini . Hivyo viatu alivyovishika ndio inasemekana alivyoviiba
 

Attachments

  • VID_20191004_133544.mp4
    45.4 MB
Probably itakuwa fundisho kwa wezi wrote was viatu misikitini..
 
ngoja nmsomee albadili awe anatembea kwa miguu
 
Mmoja wa Vijana waliomkamata alisema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakiibiwa mpaka kuamua kuweka mtego uliofyatuka ijumaa ya leo
siku zote hizo mwizi anaiba wanahangaika kumkakmata kwanini hawakumsomea alibadili??
 
Alalibadil zingine huwa hazikamati kwa vijana wa ntwara.
Ila albadr za Pangani Tanga zinafanya kweli. Wakikaa wenyewe wakianza kisomo cha kufru. Kondoo au mbuzi anaiva kama aliyebanikwa ilhali amesimama. Sasa wewe mlengwa ikifikia hapo utakua hutamaniki. Hawawezi kumfanyia mwizi wa viatu maana na wenyewe wanajua inamadhara. Ila ukiwakwaza wakisema watamwaga mboga. Omba msamaha fasta.
 
Albadri danganya toto. Utakuta anaekutishia nayo anakunywa konyagi, nyama tamu na mteja wa gesti bubu
albadir(ahlul badr) ni uchawi,wazee wataalam wa hizo mambo wametangulia mbele za haki,vijana si wajuzi,zamani huibi msikitini,kuna maquma waliiba msikitini songea miaka ya nyuma sana,walipigwa chuma wakazama topeni na saa walizoiba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom