Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,346
- 9,881
Kwa heshima nawasalimia wana jukwaa la Jamii forum!
Wakati akifunga mkutano wa 8 wa CCM, tarehe 13/11/ 2012 Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, alisema" Nataka mfahamu ndugu zangu tukiishi kwa kutegemea jeshi la polisi kufanikisha mambo yetu, tutakwisha na tutakwisha kweli". Hiyo ilikuwa ni takribani miaka 9 iliyopita. Kipindi kile kilikuwa ni mwanzo wa mwisho (The beginning of the end) wa CCM. Nchi ndo kwanza ilikuwa imetoka kwenye uchaguzi ambao Mh Kikwete alitoka kupambana na Dr. Slaa. Kikwete ambae muhula wake wa kwanza ambao alikuwa ameshinda kwa wastani wa 80% ya kura zote za uchaguzi, uchaguzi wa pili uliompambanisha na Dr. Slaa alishinda takribani 60% za "mashaka", upinzani ukiwa na nguvu sana, nchi ilianza kuona matumizi makubwa sana ya dola. Wapinzani wakipigwa, kuvunjwa na kukamatwa kila siku... CCM ikaanza kujificha kwenye kichaka cha polisi.
Miaka mitatu baada ya Kikwete kutoa kauli hiyo, nchi iliingia tena kwenye uchaguzi, safari hii CCM wakimsimamisha Magufuli, bahati mbaya huyu hakuona aibu kabisa CCM kutegemea polisi katika kufanya shuguli za kisiasa. Mikutano ya kisiasa ikapigwa marufuku, wapinzani wakapigwa risasi hadharani, wengine wakavunjwa miguu, wengine wakapewa kesi za uhujumu uchumi na wengine wakapewa kesi za mauaji. Tanzania ikawa police state. Kukawa hakuna tena siasa, ikawa nchi inaendeshwa kidikteta. CCM wakaipenda hiyo, maana wakawa wanashinda chaguzi kwa kupita "bila kupingwa". CCM ikajisahau na kuacha kufanya siasa na kunadi ambayo serikali ya chama Chao imeweza kuyatelekeza, chama kikawa kinategemea dola kiwaziwazi. Hadi kupelekea katibu mkuu wake akasema " Tutatumia dola kubaki madarakani" bila aibu na kwa kujiamini kabisa ( That was the middle of the end). Mwalimu wa siasa wa chuo kikuu uwezo wake wa kufikiria ukaishia hapo, akasahau kuwa siasa ni ushawishi.
Utawala wa awamu ya 6 umeingia nao wanaendeleza makosa yaleyale ya kutegemea dola. Mbaya zaidi, CCM ya sasa hivi haina watu wenye mvuto kabisa katika uongozi wake, zamani CCM ilikuwa ina viongozi wanaojua siasa hasa, hata kama ni za uongo ( propaganda), watu kama Kingunge Ngombale Mwiru, John Malecela, Abrahaman Kinana, Jakaya Kikwete, Edward Lowassa nk... angalau walikuwa wanajua siasa na wana ushawishi katika nchi.
Lakin wanasiasa waliopo sasaiv CCM hawana ushawishi wala hawajulikani kwa wananchi, hata ukiamua kufanya utafiti mdogo tu ukauliza wananchi huko mtaani nani ni Katibu mkuu wa sasa wa CCM, hakuna anaejua, wala naibu wake, hakuna anaejua wala kujali..( the end of the end). Hata ukitafakari ni kiongozi gani aliyopo CCM sasaiv ana mvuto kwa wananchi na ana uwezo wa kupambana na Tundu Lissu kwenye uchaguzi wa 2025 kama kutakuwa na uchaguzi huru na wa haki na akashinda.. unaona hakuna. Tutegemee matumizi makubwa sana ya nguvu za dola kuliko kipindi chochote toka nchi ipate uhuru ili CCM ibaki madarakani.
Chama Cha Siasa kinapofikia mahali hakina "touch" na wananchi kinakwisha, Chama Cha wakulima na wafanyakazi inapofikia kiongozi wake anawaambia "wale wasioweza kulipia gharama za choo wabaki na mavi yao nyumbani" ... Kiongozi wa Chama anawananga na "anawaringishia" walala hoi kuwa hawajui "utamu" wa kupanda V 8 lenye kiyoyozi kinakwisha, Chama ambacho viongozi wa serikali yake wanaambia kwa madharau wenyenchi kuwa kama hawataki tozo mpya inayowaumiza "wahamie Burundi"...kinakuwa kimefika mwisho wa mwisho. Namna pekee wanayoweza kuendelea kubaki madarakani ni kwa kutumia mabavu ya dola. Na historia inaonyesha siku zote wananchi huwa wana uwezo wa kuishinda dola..hata kama itapita muda gani. Mwisho wa CCM umefika. It's a matter of time..
Wakati akifunga mkutano wa 8 wa CCM, tarehe 13/11/ 2012 Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, alisema" Nataka mfahamu ndugu zangu tukiishi kwa kutegemea jeshi la polisi kufanikisha mambo yetu, tutakwisha na tutakwisha kweli". Hiyo ilikuwa ni takribani miaka 9 iliyopita. Kipindi kile kilikuwa ni mwanzo wa mwisho (The beginning of the end) wa CCM. Nchi ndo kwanza ilikuwa imetoka kwenye uchaguzi ambao Mh Kikwete alitoka kupambana na Dr. Slaa. Kikwete ambae muhula wake wa kwanza ambao alikuwa ameshinda kwa wastani wa 80% ya kura zote za uchaguzi, uchaguzi wa pili uliompambanisha na Dr. Slaa alishinda takribani 60% za "mashaka", upinzani ukiwa na nguvu sana, nchi ilianza kuona matumizi makubwa sana ya dola. Wapinzani wakipigwa, kuvunjwa na kukamatwa kila siku... CCM ikaanza kujificha kwenye kichaka cha polisi.
Miaka mitatu baada ya Kikwete kutoa kauli hiyo, nchi iliingia tena kwenye uchaguzi, safari hii CCM wakimsimamisha Magufuli, bahati mbaya huyu hakuona aibu kabisa CCM kutegemea polisi katika kufanya shuguli za kisiasa. Mikutano ya kisiasa ikapigwa marufuku, wapinzani wakapigwa risasi hadharani, wengine wakavunjwa miguu, wengine wakapewa kesi za uhujumu uchumi na wengine wakapewa kesi za mauaji. Tanzania ikawa police state. Kukawa hakuna tena siasa, ikawa nchi inaendeshwa kidikteta. CCM wakaipenda hiyo, maana wakawa wanashinda chaguzi kwa kupita "bila kupingwa". CCM ikajisahau na kuacha kufanya siasa na kunadi ambayo serikali ya chama Chao imeweza kuyatelekeza, chama kikawa kinategemea dola kiwaziwazi. Hadi kupelekea katibu mkuu wake akasema " Tutatumia dola kubaki madarakani" bila aibu na kwa kujiamini kabisa ( That was the middle of the end). Mwalimu wa siasa wa chuo kikuu uwezo wake wa kufikiria ukaishia hapo, akasahau kuwa siasa ni ushawishi.
Utawala wa awamu ya 6 umeingia nao wanaendeleza makosa yaleyale ya kutegemea dola. Mbaya zaidi, CCM ya sasa hivi haina watu wenye mvuto kabisa katika uongozi wake, zamani CCM ilikuwa ina viongozi wanaojua siasa hasa, hata kama ni za uongo ( propaganda), watu kama Kingunge Ngombale Mwiru, John Malecela, Abrahaman Kinana, Jakaya Kikwete, Edward Lowassa nk... angalau walikuwa wanajua siasa na wana ushawishi katika nchi.
Lakin wanasiasa waliopo sasaiv CCM hawana ushawishi wala hawajulikani kwa wananchi, hata ukiamua kufanya utafiti mdogo tu ukauliza wananchi huko mtaani nani ni Katibu mkuu wa sasa wa CCM, hakuna anaejua, wala naibu wake, hakuna anaejua wala kujali..( the end of the end). Hata ukitafakari ni kiongozi gani aliyopo CCM sasaiv ana mvuto kwa wananchi na ana uwezo wa kupambana na Tundu Lissu kwenye uchaguzi wa 2025 kama kutakuwa na uchaguzi huru na wa haki na akashinda.. unaona hakuna. Tutegemee matumizi makubwa sana ya nguvu za dola kuliko kipindi chochote toka nchi ipate uhuru ili CCM ibaki madarakani.
Chama Cha Siasa kinapofikia mahali hakina "touch" na wananchi kinakwisha, Chama Cha wakulima na wafanyakazi inapofikia kiongozi wake anawaambia "wale wasioweza kulipia gharama za choo wabaki na mavi yao nyumbani" ... Kiongozi wa Chama anawananga na "anawaringishia" walala hoi kuwa hawajui "utamu" wa kupanda V 8 lenye kiyoyozi kinakwisha, Chama ambacho viongozi wa serikali yake wanaambia kwa madharau wenyenchi kuwa kama hawataki tozo mpya inayowaumiza "wahamie Burundi"...kinakuwa kimefika mwisho wa mwisho. Namna pekee wanayoweza kuendelea kubaki madarakani ni kwa kutumia mabavu ya dola. Na historia inaonyesha siku zote wananchi huwa wana uwezo wa kuishinda dola..hata kama itapita muda gani. Mwisho wa CCM umefika. It's a matter of time..