Mwiguru Nchemba ni zaidi ya Lowasa

Hon M Nchemba hakuzungumzia ubabaishaji wa NEC, angehimiza NEC kuhakikisha kila raia stahiki anapata haki ktk zoezi la BVR.
Hon EL nae pia hakuzungumzia NEC kuhakikisha wananchi wote kuandikishwa ktk BVR.

Ningefurahi kuwasikia hawa Politicians toka CCM kutoa kauli ktk hilo la BVR.
Bila uandikishwaji wanategemea nn ktk Gen Elc?
 
Kwakweli amenishawishi kwa hoja na ajenda zake. Wasirra na Lowassa hawajanikuna kama yeye. Tatizo ni mfumo wa chama anachotokamo sijui kama watampa dhamana ayasimamie.
 
Inanipa shida rais wa tz "his excellency honorable Mwigulu Nchemba". Dah!mbona ngumu kumeza...
 
Kama nikiambiwa nivote president from ccm naweza kusema Mwigulu. Tangu mchangato wa katiba huyu jamaa amebadilika sana. Amekuwa upande wa wananchi sana na kujenga hoja nzito zenye ukweli bila kujali mapungufu yaliko kwenye chama chake. Ana vission nzuri na uzalendo na he grow from the povety family na cjasikia kama ana kashfa za kifisadi.
 
Mwigulu ni mgombea pekee ambae ameweza kukemea RUSHWA HADHARANI,HUYU ATATUVUSHA WATANZANIA,CCM mteueni MWIGULU apeperushe bendera ya CCM

Tunaimani naye.... till now huyu ndo mtangaza nia aliyenigusa 🎵🎵🎵🎵🎵🎵🎶🎶🎶🎶🎶🎶🎶🎶🎶🎶✌✌✌✌✌✌
 
nikiri kuwa mimi ni mwana-ccm niliyehama chama kwakutupa kadi kapuni baada ya kuona chama kimetekwa na mafisadi. Wapo wengi sana wanamna hiyo ninaowajua.

Pia nikiri kuwa mimi ni miongoni mwa watu waliotokea kumchukia mwiguru nchemba alipojitoa ufahamu na kusemekana kupanga mipango ovu juu ya vyama pinzani vya ccm hasa hasa chadema.

Kwasiku za karibuni, mwiguru amekuwa akijipambanua kwahoja nzito na zenye mashiko kwa umma. Hata hivyo, nimekuwa nikiendelea kuwa na mashaka.

Leo nikisikiliza hotuba yake na kuilinganisha na ya lowasa, nchemba ameendelea kuwa na hoja za mashiko kama kweli zikitekelezwa. Hoja kama za 1. Makao makuu kuhamia dodoma; 2. Mbinu za kuinua viwanda vya ndani 3. Mbinu za kuongeza ajira; 4. Kurekebisha mifumo ya ajira kwenye utumishi ya umma;

walio wengi wetu tulimsikia jana mh. Ngoyae lowasa; ambaye inasemekana watanzania wengi matumaini yao yako kwake (!!??). Binafsi sikupata ramani kamili na njia mbadala atakazotumia kuufikisha umma wa watanzania kwenye nchi ya uchumi wa kati. Angalau nimeiona kwa mwigulu nchemba.

Napenda kujifunza kutoka kwa wenzangu.

Nawasilisha

kumbe kadi umeitupa =>kapuni

basi ipo day utaichukua.. Maana umeihifadhi...


Ungeichoma au kurudisha.... Tungejua kweli umehama
 
Hadi Team Mamvi wametulia hawathubutu kuleta vurugu ... kweli kimeeleweka leo.

Binafsi Huyu bwana nimemsikiliza tangu mwanzo, amekuwa makini sana tofauti na wagombea wengine. Mfano, ameepuka kufanya upuuzi uliofanywa na wenzake, ambapo Lowasa alimkosoa na kumkejeli Kikwete, na Wasira alitumia muda mwingi kumkosoa Lowasa na kumkejeli. Tusisahau hawa wote ni chama kimoja, hoja ndio kitu cha msingi.

Nimekoshwa sana na jinsi anavyochambua hoja, anajua kinachoendelea ndani ya serikali, anajua vikwazo vya kutatua, anajua mbinu na bila shaka hizi mbinu ziko jikoni tayari ila hakukuwa na uthubutu. Hapa ni hoja, nia, na uthubutu.

Huyu bwana historia yake funika mbovu, sidhani kuna atakaemsogelea maana historia hii inawagusa wapiga kura wengi wakiwemo akina mama na vijana.
 
Back
Top Bottom