Hiyo deni keeps on growing. The budget is in shillings but the cost is in dollars! The shilling depreciated by 60 shilling againat the dollar in a month. If they to import usd 10m worth of drugs theybhave already lost 600m in purchasing power! Who bares the consequences? Us the wananchi!
If it wasent for the IPTL issue and speculation we would had experienced a lower cost of living.
Another example of poor government policy: fuel peices for nov have only dropped by 0.66% ! Whilw global price in oct alone dropped by more than 10 percent! What is the biggest contributor? Depreciation od the shilling!
Mtoto wa mfugaji na naibu Waziri wa Fedha, mh Mwigulu Nchemba kupitia kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV amethibitisha kuwa yeye ni kiongozi mwenye maono thabiti juu ya nchi yetu ya Tanzania, akizungumzia masuala mbalimbali ya kitaifa kama Ajira kwa Vijana, Mikopo kwa wanafunzi wa elimu Juu, Ufufuaji wa viwanda, Maslahi ya Wakulima na Wafanyakazi, mh Mwigulu ametoa taswira mpya yenye matumaini mapya kuelekea nchi ya kipato cha kati.
Ajira kwa Vijana.
Akiongea kwa kuonesha uhalisia kabisa wa tatizo la ajira kwa vijana hasa waliomaliza vyuo. Mwigulu amesema serikali inaendelea kutengeneza ajira mpya maana karibu ofisi zote za umma zinalalamika kutokuwa na ufanisi mdogo kwa sababu ya uhaba wa watumishi hivyo ameagiza either wizara zitangaze ajira au watoe attachment na vijana waweze kulipwa nauli na fedha za kujikimu kuliko kuwaacha vijana wakiwa mtaani wanazurura na hili linaanza kwa ya December japo ameomba vijana watakaopata nafasi hizo wawe na moyo wa Uzalendo wa kutumikia taifa. Maana wafanyakazi wengi wanafanyakazi kwa mazoea
Mikopo Ya Elimu Juu
Hakika kiongozi bora ni yule anayejua maisha na changamoto za wananchi wake kwa hili mh Mwigulu ametuonesha kwa Vitendo akisisitiza kuwa bila yeye kupewa mkopo basi ndoto yake ingeishia f6 hivyo kwa kufahamu changamoto ya mwanafunzi kukosa mkopo amesisitiza kuwa kila pesa atakayoiokoa ataenda kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Mfano zaidi bilion 87 zilizookolewa zimepelekwa bodi ya mikopo kwa ajili ya elimu ya juu.
Ufufuaji wa Viwanda
Akizungumzia kwa uchungu mzito mh Mwigulu amesema hapingani na sera ya ubinafsishaji bali ni ujanjaujanja unaofanywa na wawekezaji wenye mtazamo wa kama ni wahujumu uchumi maana kuna wengine toka wanunue hayo mashirika tena kwa bei ya kuhamasisha uwekezaji (Sio Market Value) ya mashirika lakini bado wameshindwa kulipa madeni na pia kuendeleza uzalishaji ili kutoa fursa za ajira kwa vijana zaidi ya kukopea fedha kwenye taasisi za fedha kama benki nk
Mwigulu tayari amemwagiza TR (Treasure Register) wa hazina awakumbushe wote wanaodaiwa walipe madeni yao na waanze uzalishaji mara moja tofauti na hapo serikali itachukua mashirika yote yaliobinafsishwa na hayapo katika uzalishaji kwani serikali inakosa kodi na pia Ajira kwa wananchi wake.
Maslahi ya Wakulima na Wafanyakazi
Pia mh Mwigulu aliendelea kugusia makundi mbalimbali ya jamii yetu na akazungumzia maslahi ya wakulima na akawapongeza kwa kuzalisha mazao mengi hadi tumepita lengo la taifa, serikali imekuwa ikiwatafutia masoko katika nchi za Congo na Sudan Kusini lakini kutokana na changamoto ya Ebola na machafuko huko Sudan impala imekuwa ni migumu lakini ametoa kibali na sasa wananchi wanaweza kuuza mazao yao nje ya nchi.
Pia upo mchakato unaoendelea wizarani katika kuhakikisha wafanyakazi walau mishahara yao inaboreshwa ili kuweza kukabiliana na changamoto na gharama za maisha ya sasa.
Mabadiliko ni Vitendo
Tuache Kufanya mambo kwa Mazoea
Tunaye Mwigulu Rais Aliyependekezwa 2015
Tunakuunga mkono Mwigulu