Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba Machi 13, 2026 akizungumza na wananchi wa eneo la Majalila, Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi, amesema Serikali tayari imeshalipa fedha zote za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayoendelea katika maeneo mbalimbali.
"Kila eneo ambapo mradi unatekelezwa Serikali imeshalipa fedha za mradi huo, wale wanaofanya kwenye miradi hiyo, mafundi, vibarua wapate malipo yao, hii habari ya Watu wanafanya kazi wanaendelea kunung'unika huku Serikali ikiwa imeshalipa fedha zote za miradi ya maendeleo halikubaliki, hii inagombanisha Serikali na Wananchi."
"Mkuu wa Mkoa waambie hawa wanaosimamia miradi yote wa waandikie wakandarasi sitaki kusikia wananchi wanadai fedha kwenye mradi ambao Serikali imeshalipa. Kama wapo wanaodaiwa na wengine miradi imeshakamilika wameondoka na fedha za Wananchi, mtume kamanda wa polisi wa mkoa awasiliane na makamanda wenzao wawatafute popote walipo wakamatwe wasiwe huru mpaka watakapolipa fedha ambazo wanadaiwa."
"Kila eneo ambapo mradi unatekelezwa Serikali imeshalipa fedha za mradi huo, wale wanaofanya kwenye miradi hiyo, mafundi, vibarua wapate malipo yao, hii habari ya Watu wanafanya kazi wanaendelea kunung'unika huku Serikali ikiwa imeshalipa fedha zote za miradi ya maendeleo halikubaliki, hii inagombanisha Serikali na Wananchi."
"Mkuu wa Mkoa waambie hawa wanaosimamia miradi yote wa waandikie wakandarasi sitaki kusikia wananchi wanadai fedha kwenye mradi ambao Serikali imeshalipa. Kama wapo wanaodaiwa na wengine miradi imeshakamilika wameondoka na fedha za Wananchi, mtume kamanda wa polisi wa mkoa awasiliane na makamanda wenzao wawatafute popote walipo wakamatwe wasiwe huru mpaka watakapolipa fedha ambazo wanadaiwa."