Mwigulu Nchemba, hongera kwa kazi nzuri

analysti

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
731
614
Mara baada ya uteuzi wako, nimekuwa nikifuatilia utendaji kazi wako Muheshimiwa M.Nchemba. Hakika kazi unayoifanya Katika wizara ya Kilimo, mifugo na uvuvi ni kazi ambayo hakika inaweza kutufikisha mahala ambapo kweli kilimo kitakuwa ni uti wa mgongo ulio imara kwa uchumi wetu hapa Tanzania.

Tanzania ni nchi iliyo katika nafasi za mbele kabisa kwa wingi wa Ng'ombe na mifugo mingine hapa duniani, lakini yet ni nchi ambayo sekta hii inachangia kiasi kidogo sana ktk pato la taifa. Hatua ulizozichukua kwa watendaji wa NARCO ni hatua zinazostahili pongezi, kwani NARCO kama ingekuwa imara, na kama ingeongozwa kiuadilifu, hakika taifa letu hivi sasa lisingeitazama secta ya Mifugo kama ilivyokuwa ikitazamwa.

NARCO imekuwa ni kichaka cha watu kujitajirisha, ukifuatilia kwa undani utagundua zaidi ya asilimia 90 ya hao watu uliowasimamisha, wanamiliki ranchi zao binafsi ambazo zimepatikana kwa kuiba mifugo kutoka ranchi wanazoziongoza. Ilikuwa ni desturi wanasiasa kuenda kwenye hizi ranchi na kupewa zawadi za ng'ombe ili waweze kufumbia macho wizi unaotendeka katika mashamba haya.

Muheshimiwa Mwigulu Nchemba, nina hakika kuwa hata wewe walikuwa wameshakupangia kukupatia ng'ombe kadhaa ili kusudi uache waendelee na unyang'anyi wao wa Mali ya Umma, lakini kutokana na uadilifu wako, na msukumo wenye nguvu na mwangwi usiokifani unaotokana na MAGUFULI EFFECT, hakika umeweza kuwatambulisha ya kwamba wizi wa mali ya umma si wakati wake sasa. HONGERA SANA.

Muheshimiwa Mwigulu, naomba sasa uangalie utendaji kazi wa maafisa ugani na maafisa mifugo katika ngazi mbali mbali hapa nchini. Muheshimiwa, hawa watu kama wakitenda kazi ipasvyo, ndio wenye uwezo wa kuibadilisha sekta hii ya kilimo na mifugo kuwa yenye tija kwa wakulima/wafugaji wenyewe na taifa kwa ujumla, na hii itafanikiwa zaidi katika wakati huu ambao nia ya kisiasa ipo dhahiri ila utendaji umeendelea kubaki ule ule wa kasi ya konokono na wizi uliozoeleka. Hali hii ikiachwa iendelee kuwa hivi, pasipo kuwakumbusha majukumu yao, na kuwasimamia watekeleze majukumu yao kwa weledi, hawa maafisa ugani, mifugo, na kilimo hakika watakwamisha juhudi zote uzifanyazo Muheshimiwa.

Mwisho kabisa nakupa pongezi za dhati, na nakuomba ukaze kamba kwani safari bado ni ndefu.
 
Last edited by a moderator:
Tunataka mipango mkakati ya kunusuru kilimo, kukuza sekta ya mifugo na kufanya uvuvi kuwa wa kisasa zaidi na sio ziara za kushtukiza na kufukuzana kazi kisha kusifiana huku mambo yakibaki kuwa vilevile
 
Huyu alisifiwa sana kwa matamko na vitisho alipokuwa wizara yabfedha lakini wote tuliona ukwepaji kodi ukizidi kushamiri chini yake!
 
Aliyekuambia hakuna mipango ni nani, nakuhakikishia, Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye mipango mizuri kweli kimaandishi. Mipango mikakati ilishakuwepo mingi sana, lakini yote imefail kutokana na usimamizi mbovu na kukosekana kwa uzalendo kwa watendaji wakuu. Anachokifanya Muheshimiwa Waziri ni kurejesha nidhamu na uwajibikaji kazini, hofu ya mali ya umma, haya yakishapatikana, hatuhitaji mikakati kutoka mbinguni, hata mikakati iliyopo sasa inatosha kutupeleka katika hatua ya mbele kimaendeleo ktk sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
 
Promo nyingine hizi..

Hana hata miezi 6 kwenye wizara mmeanza kusifia

Aliyekuambia hakuna mipango ni nani, nakuhakikishia, Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye mipango mizuri kweli kimaandishi. Mipango mikakati ilishakuwepo mingi sana, lakini yote imefail kutokana na usimamizi mbovu na kukosekana kwa uzalendo kwa watendaji wakuu. Anachokifanya Muheshimiwa Waziri ni kurejesha nidhamu na uwajibikaji kazini, hofu ya mali ya umma, haya yakishapatikana, hatuhitaji mikakati kutoka mbinguni, hata mikakati iliyopo sasa inatosha kutupeleka katika hatua ya mbele kimaendeleo ktk sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
 
benki ya kilimo toka ianzishwe haijamnufaisha mkulima, pessa wanazotoa wanakopesha saccos matokeo yake zinaliwa huko huko kwenye saccos haziwafikii wakulima, haya ndio mambo muhimu ya kudeal nayo sio kufanya ziara vingunguti sijui machinjioni, hivi mkulima wa tunduru songea hizo ziara za vingunguti zinamsaidia nini?
 
Duh! watendaji awamu hii lazima waipate fresh. Mi naona watumishi wote waliokuwepo awamu ya NNE wapigwe chini tuanze afresh maana inaonekana wote ni majipu tu ili viongozi wetu sasa waanze kusimamia miongozo ya utendaji badala ya kila siku kuwaza majipu atayapata sehemu gani atumbue aonekane anaenda na kasi ya awamu ya TANO.
 
Back
Top Bottom