Mwigulu kama Kikwete

Mwigulu kama Kikwete

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Nilikerwa na uuzwaji wa nyumba za serikali uliofanywa na Mkapa. Mwaka 2005 nilimchagua Rais Kikwete kwakuwa na yeye alionesha dalili za kukerwa pia na uuzwaji wa nyumba zile. Lakini hadi leo anamaliza urais wake nyumba hazijarudishwa. Mwaka 2015 nimekerwa tena na wizi wa escrow, wakati huu tena Mwigulu anaonyesha dalili za wazi za kukerwa na wizi huu na ametangaza nia ya kugombea urais 2015. Mh. Mwigulu anataka kutuaminisha kuwa kama akiwa rais atayakamata majizi yote ya mali za umma. Safari hii sitaki kuamini tena kama mtu mmoja anaweza kufanikisha jambo ambalo halimo kwenye katiba ya nchi na ambalo ni kinyume na mfumo wa chama chake cha siasa. Sera ya kukamata majizi lazima iwe kwenye katiba na iwe ni sera ya chama sio utashi wa mgombea mmoja mmoja. Ndio maana Kikwete kashindwa kuzirudisha nyumba za serikali hata kama alipenda kwakuwa sio sera ya chama chake. Hata Mwigulu akiwa rais hataweza kukamata majizi kwakuwa sio sera ya chama chake, hivyo hatapata uungwaji mkono ndani ya chama chake kutekeleza kile anachokiamini na kutuahidi. Hivyo basi, nguruwe pita sina mkuki mie mwaka huu, style ile ya 2005 ya Kikwete sintainunua tena 2015.
 
Achana na CCM, hawana jipya tena!
Wananchi wasipoyaona mabadiliko ndani ya CCM, watayatafuta nje ya CCM.
By Mwalimu Nyerere.

Tumeanza kuuona utabiri huo wa Mwalimu ukianza kutimia, kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.

Utabiri huo wa Mwalimu utazidi kutimia, kwenye upigaji kura za maoni, za katiba pendekezwa ya Sisiem, iliyoandikwa chini ya usimamizi wa mzee wa 'Escrow'
Andrew Chenge a.k.a mzee wa vijisenti, ambapo kura hizo zitapigwa tarehe 28/4/2015.

Utabiri huo wa Mwalimu utakamilika kutimia kwake, kwenye uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.
 
Wananchi wasipoyaona mabadiliko ndani ya CCM, watayatafuta nje ya CCM.
By Mwalimu Nyerere.

Tumeanza kuuona utabiri huo wa Mwalimu ukianza kutimia, kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni.

Utabiri huo wa Mwalimu utazidi kutimia, kwenye upigaji kura za maoni, za katiba pendekezwa ya Sisiem, iliyoandikwa chini ya usimamizi wa mzee wa vijisenti, ambapo kura hizo zitapigwa tarehe 28/4/2015.

Utabiri huo wa Mwalimu utakamilika kutimia kwake, kwenye uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu.
Chini ya mwizi chenge na wala sio Mzee
 
Una maana gani kuhusu hiyo kauli?
Hapo nilikuwa na maana kuwa, ukiangalia umri wa JK, ukiulinganisha na unri wa Nchemba, inawezekana kabisa kiumri JK akawa babayake Mwigulu Lameck.
 
Sioni matumaini CCM. Mabadiliko ni lazima. Hayakwepeki.
 
Mtu akiendelea kuiamini CCM atakua na matatizo ya akili, huwezi kukubali kuwa disappointed kila siku na mtu huyo huyo na wewe unaendelea kuchekelea tu
 
uadilifu wa mtu ndio tuuangalie wananchi wenzangu hata kama tunabadili chama kwa kutaka tunayofikiri yatakuwa bado uwezekanp wa kuyakosa upo kutokana na uadilifu wa kiongozi mwenyewe. kwasababu hakuna chama chenye sera mbovu ukitaka kujua hilo tafuta au angalia sera hata za TLP utagundua hili hivyo tufananishe wagombea kwa uadilifu na misimamo yao nasio kukaa tunasema hatuchagui sisiem .hata hiyo ccm ikipata kiongozi mwenye msimamo hakuna mchafu atakaebaki ssem.hatakama mgombea wake ni bora hatumchagui kwa kuwa n chma kile tusifungwe kimaamuzi
 
uadilifu wa mtu ndio tuuangalie wananchi wenzangu hata kama tunabadili chama kwa kutaka tunayofikiri yatakuwa bado uwezekanp wa kuyakosa upo kutokana na uadilifu wa kiongozi mwenyewe. kwasababu hakuna chama chenye sera mbovu ukitaka kujua hilo tafuta au angalia sera hata za TLP utagundua hili hivyo tufananishe wagombea kwa uadilifu na misimamo yao nasio kukaa tunasema hatuchagui sisiem .hata hiyo ccm ikipata kiongozi mwenye msimamo hakuna mchafu atakaebaki ssem.hatakama mgombea wake ni bora hatumchagui kwa kuwa n chma kile tusifungwe kimaamuzi

Ni mtu mmoja tu katika histoaria ya ccm ambaye aliweza kujenga hoja against chama chake na kufanikiwa kubadisha mwelekeo wake!!Ni mwalimu peke yake aliyeweza kuwashawishi ccm kuwa kukataa kuwepo kwa vyama vingi ilikuwa ni kupitwa na wakati hivyo ingawa kura zilionesha wengi wa wananchi walitaka siasa za chama kimoja ziendelee ccm ilikuwa haina budi kwenda na wakati na kugeuza mwelekeo wa siasa nchini kwa kukubali vyama vingi vya siasa. Sioni kiongozi hata mmoja ndani ya chama hicho mwenye ushawishi huo hivi sasa wote ni wahafidhina wanaoongozwa na filosofia ya " KUONGOZWA NA UTARATIBU WALIOJIWEKEA KAMA CHAMA" wa kutohoji mambo magumu! Mweneyekiti wao wa sasa ndio disaster kabisa; angalia jinsi alivyobadili msimamo wake juu ya katiba kuhusu mabadiko nchini baada ya yeye mwenyewe kuwaaasa wanachama wake kuwa wangejiandaa kisaikolojia juu ya mabadiliko, after receiving the first draft of the constitution!!
 
Nilikerwa na uuzwaji Wa nyumba za serikali uliofanywa na Mkapa. Mwaka 2005 nilimchagua Rais Kikwete kwakuwa na yeye alionesha dalili za kukerwa Pia na uuzwaji Wa nyumba zile. Lakini hadi Leo anamaliza urais nyumba hajazirudishwa. Mwaka 2015 nimekerwa tena na wizi wa escrow, wakati huu tena Mwigulu anaonyesha dalili za wazi za kukerwa na wizi huu na ametangaza nia ya kugombea urais 2015. Mh. Mwigulu anataka kutuamisha kuwa Kama akiwa rais atayakamata majizi yote ya mali za umma. Safari hii sitaki kuamini Tena Kama mtu mmoja anaweza kufanikisha jambo kinyume na mfumo Wa chama chake. Sera ya kukamata majizi lazima iwe sera ya chama sio mgombea mmoja mmoja. Ndio maana Kikwete kashindwa kuzirudisha nyumba za serikali kwakuwa sio sera ya chama chake. Hâta Mwigulu hataweza kukamata majizi kwakuwa hatapata uungwaji mkono ndani ya chama chake. Hivyo nguruwe pita sina mkuki mie, style ile ya 2005 sintainunua tena

Itakula kwako kama 2005. Sera yenye maana inatakiwa iwemo kwenye KATIBA ya nchi ili mtu kutoka chama chochote abanwe nayo na hata kama ni mgombea binafsi. Hiyo sera ya chama ni propaganda za kuwapopoa wananchi walio hoi kufikiri. Sera kuwa ya kikatiba imekataliwa na ccm kwa kufuta maadili ya viongozi
 
uadilifu wa mtu ndio tuuangalie wananchi wenzangu hata kama tunabadili chama kwa kutaka tunayofikiri yatakuwa bado uwezekanp wa kuyakosa upo kutokana na uadilifu wa kiongozi mwenyewe. kwasababu hakuna chama chenye sera mbovu ukitaka kujua hilo tafuta au angalia sera hata za TLP utagundua hili hivyo tufananishe wagombea kwa uadilifu na misimamo yao nasio kukaa tunasema hatuchagui sisiem .hata hiyo ccm ikipata kiongozi mwenye msimamo hakuna mchafu atakaebaki ssem.hatakama mgombea wake ni bora hatumchagui kwa kuwa n chma kile tusifungwe kimaamuzi

Wako watu wanatuambia "chagua chama usichague mgombea" na hakuna mtu maarufu kushinda chama. Kwa slogan hizi hakutakuwa na mgombea safi au mbaya ndani ya chama ila kutakuwa na vyama safi na vibaya. Hata Mwigulu aombe kura tu kama mtu mwingine wa kawaida na sio kujiita Sokoine maana kinachofanya vizuri au vibaya ni chama sio mtu.
 
As long as your a product of corrupt system.extra ability is needed to won against that system.sijaona mtu kutoka ccm atakaye weza hi.
 
Hivi, kuna watu zaidi ya wale wa Lumumba bado wanahangaika na CCM ..........................!!!!
 
Sioni matumaini CCM. Mabadiliko ni lazima. Hayakwepeki.

Nyenzo za mabadiliko zipo wapi? Nijuavyo mimi mabadiliko yanaanzia kwenye kujiandikisha, kupiga kura, kusimamia kura, kulinda kura, kutangaza mshindi na kumuapisha. Je, nyenzo hizo muhimu kwa mabadiliko zipo nchini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom