Mwigulu amwonya spika Anne Makinda

Mwigulu amwonya spika Anne Makinda

Ukijua maana ya budget utajua kuwa hii hoja ya mwigulu haina mshiko. Hii hela ilishawekwa kwenye budget na budget ikapitishwa kwa hiyo kwa muda huu ni ku-spend. Kusema kuwa spika asitoe hela ya michezo ni hoja iliyochelewa ulikuwa wapi wakati budget inapitishwa. Sometimes huwa hawasomi vitu na kuelewa vinapitishwa wakiwa wanasinzia wakati wa implementation ndo wanangamua makosa na kuanza kelele. Mfano mzuri ni kodi ya sim cards.

Umechemka kijana haina mana kupitishwa kwa bajeti pesa zitumike ovyo na hawara dubai zitumike kwa zilivyokusudiwa zile sio rudhuku kama utazitumia kwenda USA na Israil kwenda kuzurura na mke wa mtu
 
Wafanye kwa Gharama zao Hakuna Posho ya Kupakatana, wamepewa Fedha za kwenda kutumikia Wananchi mkitaka kusaliti ndoa zenu nje ya Nchi tumieni Fedha zenu hakuna ataelalamika. Mtu anajaribiwa kupewa KUB anashindwa kuwa Muadilifu akipewa u Mizengo Pinda si itakuwa Usaliti kama wa Yuda?

Muangalie tatizo lamatumizi sambamba na bajeti inayokuwa ipo. Ukweli ni kuwa wabunge hupitisha bajeti ambayo sio realistic. Wapinzani huwa wakiihoji ila wao CCM kwa kutumia wingi, kanuni pendelevu na usio utumikiaji wa spika na wasaidizi kwa wananchi. Utasia, ipiteeee.... Kinachofuata ni matumizi yasiyo na tija kwa wananchi. Mojawapo ni safari za wabunge. Ni kweli hazina msaada wote kwa walala hoi huku vijijini? Utasikia bajeti kubwa ya stationaries, posho, chai, soda, tamasha, ukarabati, magari, majumba, nk. Kama CCM wanaweka pesa ya kutumbua japo huwa kuna angalizo la wapinzani. Je hao wakiamua kuzitumbua CCM waanze kutema mate bungeni? Mwigulu asilalamike. Tatizo ni bajeti tumbua ya CCM!
 
Hapa issue ni nidhamu ya matumizi sio kuzuia matumizi. Kama hakuna nidhamu hata kama matumizi ni halali pesa itachakachuliwa tu. Tatizo la bunge kwa sasa ni nidhamu ya matumizi ya pesa na sio budget
 
Mwigulu Nchemba ni mnafiki kama kweli anauchungu na fedha za nchi hii afuatilie pesa za Epa,pesa za Rada na zaidi utekelezwaji wa maazimio ya bunge kamati ya mwakyembe sakata la Richmond/Dowans
Dodoma. Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwigulu Nchemba, amemwonya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuacha kutumia vibaya fedha za Serikali kwa kuwapa posho wabunge kwa ajili ya kwenda kwenye michezo nje ya nchi.

Nchemba ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akichangia Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa bidhaa ya mwaka 2013 iliyowasilishwa na Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salumu.

Mkuya katika maelezo yake alisema kuwa kodi hiyo imefutwa kwa laini za simu kwa mtu mmoja mmoja na badala yake imeongezwa katika kodi kutoka asilimia 14.5 hadi asilimia 17.

Katika mchango wake, mbunge huyo alionya kuwa kumekuwa na tabia ya kutumia vibaya fedha za umma jambo alilosema linaanzia ndani ya bunge.

“Naomba tukubaliane katika kubana matumizi, na hivyo ninakuomba Mheshimiwa Spika tuanze na ofisi yako achana na kutoa fedha kwa kuwapa wabunge kwa ajili ya kwenda Dubai kwa burudani,”alisema Nchemba.

Alisema umefika wakati ambao Serikali inatakiwa kufanya uamuzi wa kutumia fedha katika mambo muhimu ambayo yanaigusa jamii kuliko mambo ambayo hayana maana. Kwa upande mwingine aliwalaumu watendaji kuwa wameiangusha Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kushindwa kutoa ushauri na usimamizi mzuri katika makusanyo ya kodi.

Kwa upande wake Mbunge wa kuteuliwa James Mbatia aliinyooshea vidole Serikali kuwa ndiyo iliyovuruga mchakato mzima wa makusanyo ya kodi ambayo muswada wake ulishapitishwa.

Mbatia alitoa sababu kuwa ndani ya Serikali wamekuwa wakiamua mambo lakini kwenye utekelezaji wake wanagawanyika.

source : Mwananchi Jumapili :
 
Dah, kodi imeongezeka kutoka 14.5% to 17%. Kwa vigezo vipi? Mbona ni sawa na kuvuka dibwi la maji ukazama kwenye mto!
Kwa maisha yapi ya kupandisha kodi?
Viongozi wakiona magari yanazidi kuwa mengi barabarani wanafikiri maisha ya walalahoi yameboreka.
Katika mfumuko huu wa bei, kushuka thamani ya shilingi ya Tanzania, kuongezeka kodi na uingizaji bidhaa bandia nchi. Kweli kabisa Kuna ubora wa maisha hapo!!!. Enyi wabunge mwogopeni hata Mungu.
 
Serikali inayoongozwa na CCM ni dhaifu sana na viongozi wake ni dhaifu sana, huwezi kupitisha budget harafu uanze kuilalamikia (Mwigulu ni naibu Katibu mkuu wa CCM na ni Mbunge alipitisha budget kifungu kwa kifungu sasa hivi amesahau anamlalamikia Makinda) Shangaa!! Acha watu waponde raha, Gari mmewapa (KUB) na Pesa mmewapa kwa nini wasitumie? Na posho chukueni mpaka hapo serikali dhaifu itakapopata akili ya kubana matumizi ya posho zisizokuwa za lazima.
 
Hasomi alama za NYAKATI alivizia mwisho wa bunge aache gumzo ya Mbowe kwenye vyombo vya habari. kumbe operesheni TOKOMEZA in wipe out Uzushi wake kwa MBOWE.
 
Mwingulu anataka akapewe raha na Mbowe.. Mnafiki mkubwa tena.

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Mwigulu kama ungejua na kutekeleza majukumu yako kama mb usingeyasema haya sasa ulipaswa uzuie wakati wa kupitisha bajeti lakini wakati wa bajeti ulialia kuitikia ndiyooooooo sasa unapiga makelele
 
Angeishauri serikali ifute sherehe za mbio za kutembeza Mwenge Tz nzima., maradhi, uhasharati na kila aina ya balaa ndo mbali jasho la maskini la walipa kodi Tanzania nzima
 
Shonza, mara wake za watu Igunga ...kwa CCM haya ni mambo ya kawaida kabisa maana hata Samwel Sitta alitimuliwa baada ya kufaniwa na mke wa mtu alipokuwa mkuu wa mkoa wa Iringa...
 
Mwigulu yuko sahihi,Ofisi ya spika na spika hawaogopi na hawaheshimu pesa za walipa kodi.NA SIO KILA ANALOSEMA MWIGULU LAZIMA WATU WAMPINGE HUMU JF,HAIKUBALIKI.BIG UP MWIGULU!
 
Back
Top Bottom