Mwigamba hatahama CHADEMA kirahisi!

Mwigamba hatahama CHADEMA kirahisi!

Akina mwigamba wapo wengi wasio na idadi ndani ya chadema, wataibuka kila kukicha kwakuwa wana ya moyoni yasioweza kuzimwa kwa kuwashughulikia kimabavu ila tu kushughulikia yale wanayosimamia.
 
Upo sahihi sana mkuu TUPA TUPA nimekubaliana na huu mtazamo wako mfupi.
 
Sijaona updates za news conference ya Mwigamba ili niweze kufanya hitimisho.

Tafadhali mwenye taarifa kamili atuwekee humu, ule uzi mwingine uliishia njiani.
 
Tupatupa , ccm ikitimiza ahadi zake ama ikikamilisha ilani yake ya 2010 - 2015 nakupa nyumba yangu ya urithi mtaa wa nyamwezi - kariakoo !
 
akaungane na kina mwampamba na shoza.....
hana vision ndio maana yaliowakuta wale madiwani na yanayoendelea kwa shibuda kwake sio simo.
he iz very chip.we dnt need him anymore.
 
Mzee 2pa 2pa much respect, mwambie Sadifa aache matusi hapo lumumba
Siku moderators watakapoamua kuzikusanya hizi multiple ID na kuziunganisha na verified ID utashangaa wale unaodhani wapo abroad kumbe wapo Ukonga wanaendesha bodaboda
 
Hata kama cdm wakifanikiwa kum-contain mwigamba, kama hawata zingatia matumizi bora ya ruzuku hasa kupeleka pesa kwenye kanda basi wataibuka akina mwi-GAMBA wengi mara kwa mara. Cdm lazima ijue namna ya kupoza njaa za makamanda wake.

Kamanda sisi makamanda hatuna njaa, tunaendelea kulisongesha kama kawaida!
 
Ni kweli. CHADEMA inamuhitaji sana Mwigamba. But sio kama mwenyekiti wa mkoa... bali mwanachama hai kama Tuko...

Mwigamba kama mtanzania yeyote chadema inamhitaji kutupia kura yake moja kwenye sanduku la kura akaichagua chadema
 
Last edited by a moderator:
Hata kama cdm wakifanikiwa kum-contain mwigamba, kama hawata zingatia matumizi bora ya ruzuku hasa kupeleka pesa kwenye kanda basi wataibuka akina mwi-GAMBA wengi mara kwa mara. Cdm lazima ijue namna ya kupoza njaa za makamanda wake.

Hiyo ruzuku ni ndogo mno! Tatizo ni relative poverty ni kubwa mno. Kiukweli bila kuwa na certain basic needs wengi hukata tamaa haraka na kuamua kushusha silaha chini na ku surrender!

Mine or mine sijui tutalimaliza hili vipi.... Pengine tukisemezana na kubadilishana mawazo tutaweza saidia.
 
Siku moderators watakapoamua kuzikusanya hizi multiple ID na kuziunganisha na verified ID utashangaa wale unaodhani wapo abroad kumbe wapo Ukonga wanaendesha bodaboda

Na siku hiyo wanaJF ndipo watakapozijuwa vyema true colour za Mzito Kabwela huyu. Tumeanza kumjuwa leo Jason bourne, hakuna atakaesalia.
 
Kamanda sisi makamanda hatuna njaa, tunaendelea kulisongesha kama kawaida!
Kamanda najua siyo makamanda wote wana njaa, ila kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo utanikubalia kuwa chokochoko nyingi ndani ya cdm chanzo chake ni njaa. mara utasikia kiongozi fulani wa Bavicha kapokea hongo kutoka kwa shibuda, mara mwigulu kamurubuni yule, mara mwigamba analalamika makao makuu hawajapeleka pesa kwenye kanda n.k. Njaa ndo zinafanya kuibuka kwa mitandaa ya viongozi fulani waandamizi ndani ya chama. mwenye njaa hana miiko.
 
Hata kama cdm wakifanikiwa kum-contain mwigamba, kama hawata zingatia matumizi bora ya ruzuku hasa kupeleka pesa kwenye kanda basi wataibuka akina mwi-GAMBA wengi mara kwa mara. Cdm lazima ijue namna ya kupoza njaa za makamanda wake.

Kamanda sisi makamanda hatuna njaa, tunaendelea kulisongesha kama kawaida!
 
Ninachojua mwigamba aliachiwa kesi peke yake hadi leo anateseka nayo.
 
Hivi katika akili ya kawaida tu utajisikiaje ukijakugunduwa mkeo amekuanzishia thread MMU kwa kutumia fak
e ID kwamba mume wangu hanifikishi kileleni?

Wakati mnalala kitanda kimoja na hajawai kukwambia udhaifu wako?

teh teh teh teh inachekesha sn ila kula like mkuu natumia simu ya mchina
 
yawezekana kaahidiwa kufutiwa kesi ama atapewa adhabu ndogo akifanya alichokifanya maana hata kibanda nae tulishangaa kumtukuza katibu mkuu wa ccm mara tukashanga amehamia kwa Bashe, yapo mahusiano flulani hapa tujipe nafasi ya kufikiri maana matendo yao yamefanana saana Kibanda na Mwigamba.
 
Mkuu Bramo, amenisihi kutoa maoni yangu juu ya utofauti uliopo kati ya Juliana Shonza, Mtela Mwampamba na Samson Mwigamba (wakiwa CHADEMA). Najaribu tu kusikika hapa:

Juliana Shonza na Mtela Mwampamba(vijana) sasa ni makada wenzetu wa CCM. Mwigamba bado yu CHADEMA. Makada hawa wanaweza kutofautishwa hata wakiwa CHADEMA.

Kwanza, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba walikuwa BAVICHA wakati Mwigamba alikuwa Mwenyekiti wa mkoa Arusha. Hapa pana jambo zito. BAVICHA ni kiwanda cha CHADEMA kutengeneza makamanda imara wa chama na viongozi wanaofuata. Hivyobasi, BAVICHA ni sehemu adimu na adhimu. Si sehemu ya mchezo.

Vijana husika walikuwa humo.Tena mmoja alikuwa Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa (Shonza). Mwigamba yeye ameshaiva na kuivika.Katika hali ya kawaida,hata katika familia zetu,onyo kali mno hupewa kijana mdogo kuliko mtu mzima hata kwa kosa moja. Hii ni kwasababu, kijana bado ana muda mrefu wa kujifunza na kujirekebisha. Akirudia tena,adhabu kali hufuata. Ndivyo ilivyokuwa.

Pili, Juliana Shonza Mtela Mwampamba na Mwigamba wote walikiuka Katiba na Kanuni za chama. Na wote walisimamishwa. Lakini vijana waliendeleza kiburi. Walidai mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuwa wao bado wako BAVICHA na 'hakuna' wa kuwatisha. Shonza alikuwa akisema "Mimi bado Makamu Mwenyekiti BAVICHA Taifa' hata baada ya kusimamishwa.Kiburi kikubwa.Walistahili 'kuletwa' CCM. Mwigamba yeye ameshaongea na waandishi wa habari jana na amemaliza yake ya moyoni.

Tatu, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba walionesha kuwa kufukuzwa kwao ni baraka na nauli tosha kwenda CCM. Wakawahi Dodoma kupokelewa na kupiga picha na Mwenyekiti wetu wa chama-Rais Kikwete. Tena kulikuwa na Kamati Kuu yote pale Dodoma. Makini yeyote ataona haraka kuwa mchezo ulipangwa na kupangika.Hitimisho laweza kuwa vijana hawa walikuwa CHADEMA wakiiwakilisha CCM. Maybe. Mkulima maskini yeye hajahama wala kufukuzwa chama bado.Na hawezi kufanya hivyo kirahisi.

Nne, vijana hawa wakati wanaingia kwenye sintofahamu na CHADEMA walikuwa bado hawana ajira. Lakini Mwigamba alikuwa na ajira yake. Ya uandishi wa habari. Vijana hawa walikuwa wakilelewa na CHADEMA kwa kila kitu. Ingwa wote hawa wana shahada za kwanza za Ualimu na Utawala, Mwigamba yuko katika nafasi nzuri.Yeye angalau alishakuwa Mwalimu na Mhasibu mahali kabla ya kuja CHADEMA. Vijana wote walikuwa bado.

Lakini, wote watatu sasa wanajutia maamuzi yao ya kukimbia vikao rasmi na kukimbilia mitandao. Amini nawaambia, vijana wawili: Juliana Shonza na Mtela Mwampamba hawana maisha ya uhuru na raha kama waliyokuwa nayo CHADEMA. Pale CHADEMA walikuwa wana usemi na nafasi. Hapa CCM hawana. Kuna vijana kama wao hapa waliwakuta na nafasi zao. Wageni hawa lazima wawe wapole. Kimsingi, wako 'limited' sana. Mwigamba bado anadunda ndani ya CHADEMA.Amesimamishwa tu.
Juliana Shonza na Mtela Mwampamba ni vijana wazuri kichama lakini wanaendesheka kirahisi. Yawezekana ni kutokana na kuhitaji makubwa haraka. Lakini, bado wana muda wa kutosha kujirekebisha. Wanaweza kuaminika chama chochote cha siasa nchini na kuendeleza mapambano yao ya kisiasa. Kwanza wakubali kuwa wao wanaongozwa na Katiba na Kanuni za vyama vyao.Viongozi wao wapo tu kuwasimamia na kuzisimamia Katiba na Kanuni husika. Basi.

Kwenye siasa lolote linawezekana. Ipo siku, yaweza kuwepo kweli ndugu zangu, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba wakarejea CHADEMA na Mwigamba akahama CHADEMA. Siasa hazitabiriki!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam



 
Nasema hivi kiongozi aliemaliza muda wa uongozi anahaki ya kugombea na kuchaguliwa tena mradi awe anatimiza mashariti katika cheo kimoja hii iko kwenye ibara moja ya toleo la 2004 mwaka 2006 tulifanya renovation mwaka huo huo tulikubaliana kubadilisha baadhi ya vipengele mimi nilikuwa katibu wa wilaya na hiki kipengele hatukiozungumzia juzi wakati napitia katiba nikitaka kujua kwanini mbowe na zitto wanagombana nikaona hiki kipengelee hakipo, nikasema kwanini hatukuambiwa wajumbe wakati kinaondolewa...MBOWE, ARFI - bara, MOHAMEDI ISSA - zanzibar, DR SLAA, Naibu katibu mkuu MOHAMEDI YUSUF- zanzibar, ZITTO –Bar hawa mimi ndiyo nawapinga kuendelea kugombea.....

Bahati mbaya sina katiba ya CDM toleo la 2004. Lakini Mwigamba angetusaidia kama angeitaja hiyo IBARA na kutuwekea quotation yake. Lakini kusema ilikuwa kwenye toleo 2004 na kuacha hiyo statement ina hang hewani inaleta maswali mengi kuliko majibu.

Mwigamba tunaomba utueleze hicho kipengele kilikuwa IBARA gani ya KTIBA 2004?. Na pia iwekee nukuu yake hapa ili uweze kuaminika.
 
kitendo cha kukichafua chama kwenye mitandao umefika muda akawapikie chai wakina nape kama mtela mwampamba na wengine,pia nautakia kila la kheri uongozi wa juu wa chadema hakuna kulala mpaka kinaeleweka.
 
Back
Top Bottom