- Thread starter
- #21
[QUOTE=Yakuonea;4019268]
Beti nilimtumia, kumpa yeye nasaha
Hekima nikajazia, aepuke ya karaha
Awache kung'ang'ania, ajenge yake staha
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
Beti zangu hakujibu, sijui hata kwa nini
Labda ni zake ghadhabu, kwa vile bado kuwini
Au kashikwa aibu, binti kutomthamini
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
Na hataki shaurika, eti mrembo ni wake
siku nazo zakatika, aishi kivyake vyake
uzee utamfika, bila hata ya mwenzake
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)
KIJIJINI TONGOLEANI
[/QUOTE]
Nzi kufia dondani!
Nzi kufia dondani, msemo waujulia?
Narudi kwako mtani, wahenga kukumbushia
Mapenzi ni upofuni, kupenda kweli wajua?
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Ni mengi umeyahoji, na hapo nikajulia
Ki mapenzi si mwnyeji, mtani nimegundua
Hunacho pia kipaji, mapenzi kufahamia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Zaidi ya maradufu, kwa kina kuelezea
Nahisi wewe kipofu, mapenzi kujionea
Umpendaye hukifu, kwa dhati nakuminyia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Kigumu kwako ni kipi, mtani ninashangaa
Mgongo kweli simpi, spidi naongezea
Ladhaye yashinda pipi, mapenzi nasubiria
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Tano zilizo kamili, ni beti namalizia
Bibie nina mjali, hakuna afanania
Ya kwanza, siyo ya pili, nambari ashikilia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Kijana Bin M'bichi
Beti nilimtumia, kumpa yeye nasaha
Hekima nikajazia, aepuke ya karaha
Awache kung'ang'ania, ajenge yake staha
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
Beti zangu hakujibu, sijui hata kwa nini
Labda ni zake ghadhabu, kwa vile bado kuwini
Au kashikwa aibu, binti kutomthamini
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
Na hataki shaurika, eti mrembo ni wake
siku nazo zakatika, aishi kivyake vyake
uzee utamfika, bila hata ya mwenzake
CHOVEKI ANISHANGAZA, KWA PENZI KUNG'ANG'ANIA
SINDANO MWANA WA GANZI (SMG)
KIJIJINI TONGOLEANI
[/QUOTE]
Nzi kufia dondani!
Nzi kufia dondani, msemo waujulia?
Narudi kwako mtani, wahenga kukumbushia
Mapenzi ni upofuni, kupenda kweli wajua?
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Ni mengi umeyahoji, na hapo nikajulia
Ki mapenzi si mwnyeji, mtani nimegundua
Hunacho pia kipaji, mapenzi kufahamia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Zaidi ya maradufu, kwa kina kuelezea
Nahisi wewe kipofu, mapenzi kujionea
Umpendaye hukifu, kwa dhati nakuminyia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Kigumu kwako ni kipi, mtani ninashangaa
Mgongo kweli simpi, spidi naongezea
Ladhaye yashinda pipi, mapenzi nasubiria
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Tano zilizo kamili, ni beti namalizia
Bibie nina mjali, hakuna afanania
Ya kwanza, siyo ya pili, nambari ashikilia
Halali nakujulia, nzi kufia dondani!
Kijana Bin M'bichi