GE2025 Mwenyekiti wa TEF, Balile: Kampeni za mwaka huu zina hoja zaidi

GE2025 Mwenyekiti wa TEF, Balile: Kampeni za mwaka huu zina hoja zaidi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Deodatus Balile, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) amedai kuwa Kampeni za uchaguzi huu wa Oktoba 29, 2025 zimejaa hoja;

"Nimeshuhudia kampeni za miaka mingi lakini kampeni za mwaka huu zina hoja zaidi lakini mazingira yamebadilika watu wana Smart phone na bahati mbaya hizi (simu) hazituonyeshi uchochoroni zinatuonyesha katikati ya Mji.

"Mtu akiona London pale katikati na New York pale katikati. Akaona Johannesburg katikati anasahau kwamba ukitoka kilometa kumi kuna shida sehemu nyingine kwahiyo watu wanataka kuishi maisha ya smartphone.

"Nimeona kuna mwingine anasema kampeni zimekuwa kama shopping list kwamba atafanya hivi au vile. Nikasema inawezekana kuna shida mahali kwamba watu hawajui kwamba hiki ndio kipindi cha kutoa ahadi ambazo tutakubana nazo baada ya kushinda uchaguzi kwamba aliahidi atajenga barabara ya Kitunda iko wapi?

"Sasa alipoahidi mtu anasema aeleze utekelezaji! Hiki ni kipindi halisi na sahihi kwa ajili ya kuahidi"

Soma > Mwenyekiti wa TEF, Balile: Watu mtandaoni wanajizima data au sijui hamnazo? Tanzania kuna maendeleo hadi vjijini
 
Kama huyu ndio mwenyekiti TEF, hao wanaoongozwa na huyu wakoje.
Kuna sheikh mmoja kasema, kama umepewa bahasha tulia, usipende kila mtu ajue udhaifu wako.
 
Hii nchi hata sijui shule tumejenga za nn Tuna wasomi wa hovyo zaidi hata ya hovyo yenyewe ... Dah kama huyo ni kiongozi wa taasisi ndo anatoa boko km hilo je huku chini 😭
 
Bila shaka huyu Balle ni punguani mnafiki, asiye na uwezo wa kumudu maisha yake, hivyo anaamini kwa kuwa chawa mnafiki huenda itamsaidia kupata unafuu wa maisha.

Mapunguani kama hawa, ni kuwapuuza tu.
 
nakumbuka cartoon ya masoud kipanya ikiwaonyesha waandishi wa habari kama toilet paper
 
Back
Top Bottom