Mwenyekiti wa Kijiji Cha Ilula (CHADEMA) ajiuzulu na kujiunga na CCM

security guard

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
799
603
Mwenyekiti wa Kijiji cha Ilula, Kata ya Hungumalwa Wilayani Kwimba ndugu Hamala Materemki amejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) asubuhi ya leo baada ya hotuba ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana aliyoitoa kwa wananchi baada ya kushiriki mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Hungumalwa.

Mwenyekiti huyu, mwanachama wa CHADEMA amefikia uamuzi huo baada ya kukinai maneno ya kweli yenye ujumbe mzito aliyoyatoa Katibu Mkuu wa CCM kwa wananchi wa eneo hilo, akiwataka waache kuyumbishwa na Upinzani na waamue kwa dhati kujiletea maendeleo kwa kufanya Kazi.

Ndugu Hamala, ameshaandika barua ya kujiuzulu nafasi yake ya Uenyekiti wa Kijiji, kwani amepoteza sifa kwa kuhama Chama alichokuwa anakiwakilisha na hivyo italazimika ufanyike uchaguzi mwingine wa kuunda upya Serikali ya Kijiji, ambapo Ndugu Hamala amesema atagombea tena nafasi hiyo kupitia Chama Cha Mapinduzi.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana yuko Wilayani Kwimba akiendelea na Ziara yake ya Siku kumi katika Mkoa wa Mwanza, ambapo anategemea kumaliza Juni 30, 2015.

CIQPBJCWoAAocEg.jpg
 

Attachments

  • 18.jpg
    18.jpg
    56.4 KB · Views: 988
Naye watamuita msaliti. tehteh bavicha mna mambo, CCM wanaomba Slaa awarudishie kadi yao ambayo hataki kuirudisha.
 
CHADEMA inakufa kibudu baada ya watu wenye akili kuanza kukikimbia,watabaki wenye maslahi wanaofaidika na mfumo kandamizi uliopo.
 
Kinana anafanya jambo moja la hatari kwa amani, usalama na maendeleo ya demokrasia katika nchi hii, anasema katiba mpya sio chochote na haimuhusu mwananchi, pia anasema wananchi wasiwaheshimu viongozi wa upinzani, pia anasema wananchi waachane na siasa.

Ukiaangalia utangundua kuwa ameshawasoma akili wale jamaa wa bush kuwa hapa shule hakuna,hivyo ngoja nijifanye mkombozi!.hii sio haki.

Anajua kule hakuna anayejua kuwa yeye ni mhusika wa ujangili maana kampuni yake ilikamatwa ikisafirisha matani ya meno ya tembo.Kwa takwimu ni kuwa mwaka 2010 pale selous tulikuwa na tembo 150000 lakini mpaka mwaka jana tulibakiwa na tembo 13000 tu.

Huyu ni mtu ambaye ana jibu kuhusu ujagili but kwa kuwa nchi hii ni shamba la bibi na hakuna mwenye haki basi.....nani atamuuliza but siku yaja....tutamuuliza.Alijua kuhusu usafirishaji huo.....ndio maana akiulizwa yeye anasema ohoo ile ni kampuni hivyo yeye hajui.Kwani kampuni haikujui kuwa kuna bar ya kusafirisha meno ya tembo,je management si walitaka assurance yake.

Tanzania ni nchi isiyo na wenyewe yaani kama USA vile...ndio maana karibu warundi 160000 mnawapa uraia,wasomali kibao nao wanapewa uraia.Tumekwisha...

TANGANYIKA ITALINDWA TU KAMA SIO LEO BASI KESO.Ardhi hii ni kwa ajili ya Watanganyika.Ndio maana HAWAKUZALIWA SOMALIA, KENYA, USA, UARABUNI,ETC!

TANGANYIKA KWANZA.....UZAWA KWANZA.
 
CHADEMA inakufa kibudu baada ya watu wenye akili kuanza kukikimbia,watabaki wenye maslahi wanaofaidika na mfumo kandamizi uliopo.

Tatizo lako ni kuwa umechanganyikiwa , Mwenyekiti mmoja wa kijiji anakupa shida hivyo? Zitto alifukuzwa sembuse huyu
 
Mleta uzi umesema jamaa kaamua kujiuzulu nafasi yake baada ya kukinai maneno ya ukweli ya kuambiwa aachane na vyama vya upinzani , eti ccm ndiyo ya kuwaletea maendeleo. Ni vyema kabisa alivyofanya kwani inaelekea uelewa wake ni
mdogo na bado ni rahisi kurubunika.
 
Looh CCM choka mbaya, katibu Mkuu wa Chama Tawala anafunga safari kutoka DSM hadi Hungumalwa Mwanza kumpokea M/kiti wa Kijiji wa CDM?!
 
Uyu ndugu wacha aende, wacha awemzululaji wa kisiasa. Wachukue mjumbe mmoja ashikilie hiyo nafasi.
 
Bwana Gor kitu ambacho hujamalixia ni kuhusu ile gari ys Mbowe yenye alams KUB kukamatwa na magendo tena nje ya nchi ulikuwa mradi wa Mbowe??
Pia ungenielewesha hivi ninyi wakati mnafaulu kuwaingiza CHAGADEMA muda ule pia walikuwa hawana akili? Na mlitumia njia gan baada ya kuwasoma hawana akili na mkaitumia njia hiyo kuwaingiza chama cha Matukio??
Au akili zimeisha hasa baada ya wao kutimia haki yao kikatiba kuhama chama chenu cha Kichaga???
Kunya anye kuku tu akinya bata kaharisha!!!! Mtajibeba mwaka huu...
 
Back
Top Bottom