GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Kibamba, Ernest Mgawe akamatwa kwa tuhuma za kuhamasisha Maandamano na Fujo Vituo vya Mwendokasi

GE2025 Mwenyekiti wa CHADEMA Kibamba, Ernest Mgawe akamatwa kwa tuhuma za kuhamasisha Maandamano na Fujo Vituo vya Mwendokasi

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
1759405819154.jpeg

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jimbo la Kibamba, Dar es Salaam Ernest Mgawe anashikiliwa na Jeshi la Polisi ikielezwa kuwa anatuhumiwa kutenda makosa mawili (2) ambayo ni kuhamasisha maandamano, na kuhamasisha watu kufanya fujo kwenye vituo na magari ya mwendokasi

Taarifa iliyotolewa leo Oktoba 02.2025 na Wakili wake Dickson Matata imeeleza kuwa baada ya Mgawe kukamatwa jana, Oktoba 01.2025 mteja wake alipelekwa kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay, ambapo akiwa kituoni hapo aliandika maelezo

Soma zaidi > Kamanda Muliro: Watatu wakamata kwa kuharibu Mabasi ya Mwendokasi, wengine wasakwa katika fujo Magomeni

Wakili Matata, anasema ilipofika majira ya Saa 06:30 usiku maafisa wa Jeshi la Polisi wakiambatana na mtuhumiwa na Wakili wake walielekea nyumbani kwa mtuhumiwa Kibamba kwa ajili ya kufanya upekuzi katika makazi yake

"Muda huu Saa 11:21 alfajiri ndio tumetoka Kibamba na kufika Oysterbay Police baada ya kumaliza zoezi la upekuzi ambalo (Polisi) hawajapata kitu chochote kinachohusiana na tuhuma zinazomkabili" -Wakili Matata

Katika maelezo yake, Wakili Matata amebainisha kuwa zoezi hilo lilikuwa linasimamiwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Gogoni ASP Yahaya M. Omary aliyekuwa anatekeleza maelekezo ya RCO wa Kinondoni

Kuhusu suala la dhamana ya mteja wake, wakati anaandika taarifa hiyo alfajiri ya leo Wakili huyo alitoa wito wa subira, huku akiahidi kuendelea kufuatilia mchakato huo wa dhamana siku ya leo

Chanzo Jambo TV
 
Wakuu,

Si nilisema jana, jinsi media chache zilivyoripoti hii ngoma inaenda inatafuta wa kuangushiwa na chances are wataedna kuwaangushia zigo CHADEMA :BearLaugh: :KEKWlaugh: CHADEMA ambao wamezuiwa kufanya shughuli zote za kisiasa!

Polisi, serikali na CCM wamekuwa that predictable. Yaani mnafanya wananchi wajinga, kwamba hawaoni kinachotokea! Baada ya kuchukua jana kama funzo na kurekebisha yaliyotokea ndio mnazidi kutia petroli kwenye moto!

Kweli sikio la kufa halisikii dawa, tuko na nyie hadi Gen Z watekeleze jambo lao kikamilifu!:elmoFire::elmoFire::elmoFire:

Kalamu
 
Jeshi imejaa Vilaza.
Kamanda Willy na vijana wako wa Upelelezi hapo Kijiweni ( Gogoni ).
Ni upelelezi gani mtakuja mshika mtu na ushahidi wa wazi ?.

Kijiwe Cha Kufosi Uzushi.
 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jimbo la Kibamba, Dar es Salaam Ernest Mgawe anashikiliwa na Jeshi la Polisi ikielezwa kuwa anatuhumiwa kutenda makosa mawili (2) ambayo ni kuhamasisha maandamano, na kuhamasisha watu kufanya fujo kwenye vituo na magari ya mwendokasi

Taarifa iliyotolewa leo Oktoba 02.2025 na Wakili wake Dickson Matata imeeleza kuwa baada ya Mgawe kukamatwa jana, Oktoba 01.2025 mteja wake alipelekwa kwenye Kituo cha Polisi Oysterbay, ambapo akiwa kituoni hapo aliandika maelezo

Wakili Matata, anasema ilipofika majira ya Saa 06:30 usiku maafisa wa Jeshi la Polisi wakiambatana na mtuhumiwa na Wakili wake walielekea nyumbani kwa mtuhumiwa Kibamba kwa ajili ya kufanya upekuzi katika makazi yake

"Muda huu Saa 11:21 alfajiri ndio tumetoka Kibamba na kufika Oysterbay Police baada ya kumaliza zoezi la upekuzi ambalo (Polisi) hawajapata kitu chochote kinachohusiana na tuhuma zinazomkabili" -Wakili Matata

Katika maelezo yake, Wakili Matata amebainisha kuwa zoezi hilo lilikuwa linasimamiwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Gogoni ASP Yahaya M. Omary aliyekuwa anatekeleza maelekezo ya RCO wa Kinondoni

Kuhusu suala la dhamana ya mteja wake, wakati anaandika taarifa hiyo alfajiri ya leo Wakili huyo alitoa wito wa subira, huku akiahidi kuendelea kufuatilia mchakato huo wa dhamana siku ya leo

Chanzo Jambo TV
Anahusika nn huyo mwenyekiti? Alikuwepo usiku kwenye mahangaiko ya usafiri?
Aisee ccm acheni ujinga huu kwnn hamjifunzi?
 
Watu wameona huduma mbovu wameamua kupaza sauti, wao wanaona kua chadwma ndo wanatuma watu kufanya vurugu huko tuendako ni kubaya sana
 
Unajitahidi brother, kama haupo kwenye payroll bhasi waone jitihada zako na wakupe kiti pahala flani.
Huyu jamaa anajiita mama halafu inadaiwa ni wa jinsia ya kiume, kuna namna ana walakini. Jinsia aliyojipatia na aina ya uwasilishaji wake lazima atakuwa bwabwa.
 
Halafu huyu bwana ni kama amewahi kuwa diwani wa kibamba kuanzia 2015
 
Wakuu,

Si nilisema jana, jinsi media chache zilivyoripoti hii ngoma inaenda inatafuta wa kuangushiwa na chances are wataedna kuwaangushia zigo CHADEMA :BearLaugh: :KEKWlaugh: CHADEMA ambao wamezuiwa kufanya shughuli zote za kisiasa!

Polisi, serikali na CCM wamekuwa that predictable. Yaani mnafanya wananchi wajinga, kwamba hawaoni kinachotokea! Baada ya kuchukua jana kama funzo na kurekebisha yaliyotokea ndio mnazidi kutia petroli kwenye moto!

Kweli sikio la kufa halisikii dawa, tuko na nyie hadi Gen Z watekeleze jambo lao kikamilifu!:elmoFire::elmoFire::elmoFire:

Kalamu


CCM wanatafuta culprits tu. By 29th October watawafunga just ya viongozi wa Chadema ingawa wanewazuia kufanya siasa.
 
Yaani wanataka kusema hizo gari ni za CCM hivyo wanaopanda ni wote wanaCCM na CHADEMA ndio wamezishambulia?

Mnaoishi hiyo route na mpo humu mtujuze je nyie wote ni CCM?

Najua hii ni move pia wanaisuka kumkamata Heche hadi igizo lao la uchaguzi lipite wakiwa na zile stori zao za taarifa za kiintelijensia juu ya matishio ya kuharibu miundombinu na kudhuru viongozi wa CCM
 
Hapo kunamtu anatafutiwa kesi nchi yangu inapoelekea sio kuzuri kabisa
 
Back
Top Bottom