VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Ile timu ya makada nguli wa chama 32 kumpigia kampeni Dr. Magufuli na Samia S. Hassan imekumbwa na kanyamazongo. Haiko pamoja na haimsaidii Dr. Magufuli kama ilivyotarajia. Hata kilichotokea leo ni aibu hata kukiandika hapa. Natunza heshima ya chama changu.
Mwenyekiti Kikwete,unahitajika kwenye kampeni. Tayari Dr. Magufuli ameshajionesha kuwa anaweza kujisimamia. Tayari amejitangaza vya kutosha. Tayari amesikika ingawa shati wanamshika. Lakini,Mwenyekiti Kikwete yakupasa uingia kampenini. Timiza ahadi yako ya Lumumba kuongoza ngoma ya ushindi. Uko wapi?
Mwenyekiti,wanatimu uliowaamini hawaaminiki. Wanamimina matusi,kashfa zisizo na afya,kejeli za jeuri na maigizo. Wamemfanya hata Dr. Magufuli kuwa tapeli na muigizaji wa kisiasa. Usijitenge Mwenyekiti. Ingia ngomani. Mazuri yako yatambeba huyu. Hali inatisha kwenye kampeni. Si vutizi. Wenzetu watatupiga overtake na teke.
Mwenyekiti Kikwete,tafadhali okoa jahazi na hadhi ya CCM!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
Mwenyekiti Kikwete,unahitajika kwenye kampeni. Tayari Dr. Magufuli ameshajionesha kuwa anaweza kujisimamia. Tayari amejitangaza vya kutosha. Tayari amesikika ingawa shati wanamshika. Lakini,Mwenyekiti Kikwete yakupasa uingia kampenini. Timiza ahadi yako ya Lumumba kuongoza ngoma ya ushindi. Uko wapi?
Mwenyekiti,wanatimu uliowaamini hawaaminiki. Wanamimina matusi,kashfa zisizo na afya,kejeli za jeuri na maigizo. Wamemfanya hata Dr. Magufuli kuwa tapeli na muigizaji wa kisiasa. Usijitenge Mwenyekiti. Ingia ngomani. Mazuri yako yatambeba huyu. Hali inatisha kwenye kampeni. Si vutizi. Wenzetu watatupiga overtake na teke.
Mwenyekiti Kikwete,tafadhali okoa jahazi na hadhi ya CCM!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.