Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa Ndugu Nimka Lameck leo tarehe 21/10/2018 ametembelea uchaguzi wa chipukizi unaoendelea katika wilaya za Kinondoni, Ubungo na Temeke ambapo amepata fursa ya kuzungumza na wajumbe wa mkutano mkuu katika wilaya hizo.
Akizungumza na wajumbe hao kwa nyakati tofauti Ndg Nimka amewataka wachague viongozi kutokana na sifa na uwezo wa kuwawakilisha na kuwasemea changamoto zinazowakabili watoto. Pia alikemea vikali suala la rushwa katika uchaguzi huo
"Naomba tumuunge mkono Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais wa Tanzania katika kuipiga vita Rushwa kwa kutokubali kushawishiwa kwa vitu ili kumchagua kiongozi atakayetuongoza. Wote watakaobainika kuwashawishi kwa vitu tutawachukulia hatua kali kwa mujibu wa taratibu za Chama ili kulinda maadili yetu."
#KulindaNaKujengaUjamaa
#TukutaneKazini
Akizungumza na wajumbe hao kwa nyakati tofauti Ndg Nimka amewataka wachague viongozi kutokana na sifa na uwezo wa kuwawakilisha na kuwasemea changamoto zinazowakabili watoto. Pia alikemea vikali suala la rushwa katika uchaguzi huo
"Naomba tumuunge mkono Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais wa Tanzania katika kuipiga vita Rushwa kwa kutokubali kushawishiwa kwa vitu ili kumchagua kiongozi atakayetuongoza. Wote watakaobainika kuwashawishi kwa vitu tutawachukulia hatua kali kwa mujibu wa taratibu za Chama ili kulinda maadili yetu."
#KulindaNaKujengaUjamaa
#TukutaneKazini