Mbeto alisema matatizo yaliochomoza yana taaswira yac Siasa hivyo ni busara utatuzi wake , ukachwaa mikononi mwa Serikali na wanasiasa huku viongozi wa Dini wakisubiri kushirikishwa itakapohitajika .
Alisema hata inapozuka mizozo au mitafaruku ya Kidini Makanisani kwenye Mahekalu na Misikitini ,Wanasiasa hawana nafasi ya kushiriki katika kufikia utatuzi , ni busara pia kwa viongozi wa Dini kutoingilia Siasa.
"Viongozi wa Serikali hawajachoka kutafuta Suluhu na utatuzi kwa yaliotokeea. Si vyema na wala si ustaarabu Viongozi wa Dini kuwapangia hatma viongozi Serikali lipi la kufanya "Alisema Mbeto .
Akizumgumza kwa utulivu, Katibu huyo Mwenezi , alisema inasikitisha kuona Viongozi wa Dini Kuu , Uislam na Ukristo, wakianza kuzungumzia masuala ya kisiasa ndani ya nyumba za ibada kwa jazba na hamaki .
'Taifa linaoongozwa na Serikali ya Rais , Mkuu wa Nchi mwenye mamlaka kisheria na kikatiba. Hajashindwa kumaliza yaliojitokeza .Ikiwa viongozi wa Dini watahitajika wataitwa kutoa ushauri itakapobidi "Alieleza
Aidha ,alisema kwa namna yoyote ikiwa Viongozi wa Dini wataendelea kutoa matamko yenye hofu na taharuki katika jamii , Taifa linaweza kupitishwa katika Jangwa la hatari nyeusi isioepukika.
"Mwalimu Julius Nyerere amewahi kutamka hadharani Serikali ya Tanzania haina Dini. Wananchi ndiyo wenye imani za Dini .Hivyo si vyema baada ya miaka 60 Dini zijibebesha dhamana za kisiasa ' Alifafanua Mbeto
Chanzo: Habari digital