Mwanzo huwa mgumu, kaza mwendo

Mwanzo huwa mgumu, kaza mwendo

Amba Samedi

Senior Member
Joined
Apr 5, 2024
Posts
193
Reaction score
326
Habari wanaJF,

Ni jioni nyingine tena nakuja hapa kumalizia siku hii. Nikiwa hapa, nilipiga picha ya kumbuukumbu za maisha ya hapo nyuma. Nikagundua cycles fulani zinazojirudia rudia. Na cycle (mzunguko) unapoisha, huna budi kuanza tena.

Mwanzo huwa ni mgumu. Maisha sio rahisi baada ya kupoteza vyote. Lakini if this is your case, endelea kusoma. Kuna kitu fulani nimeakuandalia kukutia moyo unapokabiliana na wiki hii mpya.

Nakuletea "the 3Ts You Must Know if You're Starting from Scratch" (Vitu 3 vya kuvifahamu endapo utakuwa unaanza upya).

1. Muda (Time)


Muda sio tu masaa 24—ni namna unavyoutumia. Utahitaji muda wa kujifunza, wa kufikia watu, wa kutoa huduma, na wa kujenga kitu ambacho kitabadilisha maisha yako na ya jamii yako. Utahitaji muda wa kuvumilia ukimya, kusubiri dalili za mvua, na kuendelea hata pale juhudi zako zinapoonekana kugonga mwamba.

Fahamu kuwa Mohammed Dewji (Mo) hakurithi utajiri mkubwa kama wengi wanavyodhani. Alianza na biashara ya familia iliyokuwa ndogo, lakini alitumia muda mwingi kujifunza, kupanua mtandao wake, na kuweka mikakati ya muda mrefu. Leo, anajulikana kama mmoja wa wafanyabiashara wakubwa Afrika (na anaongoza Afrika Mashariki, kwa mujibu wa Forbes List 2024). Lakini ilikuwa ni safari ya muda mrefu—yenye kazi kwelikweli.

"Muda ni mtaji wa maskini mwenye ndoto kubwa."

2. Kipaji (Talent)


Kila mtu ana kitu kimoja anachokifanya vizuri zaidi ya 90% ya watu wanaomzunguka. Hicho ndicho silaha yako. Kitafute. Kikuze. Kikamilishe. Kama hujui talanta yako, waulize wanaokufahamu. Halafu jifunze kitu kipya kinachohusiana na talanta/kipaji chako kila siku, hata kama ni kwa dakika 15 tu. Kipaji hukua. Baada ya mwaka mmoja utakuwa mbele ya asilimia 90 ya watu.

Angalia Nandy—aliyekulia katika mazingira ya kawaida mkoani Moshi. Alijua kuwa ana kipaji cha kuimba, akakikuza kupitia mashindano kama Tecno Own the Stage. Alijitahidi, akaendelea, na leo ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa Afrika Mashariki. Kipaji kilichofanyiwa kazi kiliweka historia. Konde Boy, Joel Nanauka na wengine kama hao ni mifano ya kuichunguza vizuri.

"Kipaji ni zawadi; lakini mafanikio ni kazi."

3. Uaminifu (Trust)

Unapokuwa huna kitu, uaminifu wako ndiyo mtaji wako wa kwanza. Ukiukosa, unaharibu msingi wa kila kitu. Ukikopa, lipa kwa wakati. Ukipewa nafasi, shine. Ukiaminiwa na mtu, usiache doa. Uaminifu unafungua milango ambayo hata pesa haiwezi kufungua.

Wasanii wengi waliofanikiwa walipiga mbio kwa mgongo wa mtu mwingine. Ambaye alikuwa na watu, na access, na platform. Rais Samia hangekuwepo kama mwamba hangemwona na kumpa nafasi. Christiano Ronaldo (CR7) alishine kwa sababu ya rafiki yake aliyemwamini na kumpasia mpira akafunga, na kupata nafasi kujiunga na Lisbon Footbal academy. Trust, my friend, is the currency of starters.

"Uaminifu hujengwa na matendo, si maneno."

Endapo umelazimika kuanza na hakuna kinachoenda, kama kila kitu ni kigumu—shikilia. Mwanzo ni mgumu. Ndivyo ilivyo. Lakini mchakato huo unakutengeneza kuwa mtu ambaye usingekuwa endapo changamoto hazingekuwepo.

Signed,
Amba Jnr.
 
Yote kwa yote pesa ni muhimu
Mtazamo mzuri. Ila watu ni mtaji. Mtu anaweza akakupa pesa. Ukiaminika, utafanya kitu. Jamaa wangu mmoja (mzee wa makamo), alianza biashara kwa Tshs 2,000 mwaka 1984 (thamani ya 300,000 sasa). Bibi mmoja alimwamini na kumpa pesa amtunzie, ili aje kuchukua baada ya wiki 2 kwenda nayo sokoni kuemea vitu.

Badala ya kutunza, alienda Musoma mjini na kununua vitu. Alizungusha mara kadhaa. Mama alipokuja baada ya wiki mbili, alikuwa ashazungusha, akapata faida ya kutosha, na kumrudishia pesa zake zote.

Mwanzo sio tu pesa, ni akili yenye kutumia vizuri muda, talanta na uaminifu.
 
Kitu kikubwa na cha umuhimu ni uwezo wa kutambua fursa na kuzifanyia kazi hayo mengine hayana umihimu sana, kuna watu wana kipaji na waaminifu na wana uvimilivu huko mtaani na wapo pale pale
 
Kitu kikubwa na cha umuhimu ni uwezo wa kutambua fursa na kuzifanyia kazi hayo mengine hayana umihimu sana, kuna watu wana kipaji na waaminifu na wana uvimilivu huko mtaani na wapo pale pale
Uaminifu ni kitu cha umuhimu (lazima),ni maamrisho ya Allah,
Nilishawahi ku nunua kitu lakini ktk pesa yangu ikapungua laki moja dalali aka kubali kuni dhamini hiyo laki moja kutokana na maneno na imani yangu, muda uka fika nika lipa hiyo laki na huyo dalali nika mjulisha (hakuwepo)

Kilicho fuata alikubali kuni dhamini laki 5 tena nika muahidi nita mpa na pesa ya udalali kwa maana sikuwa nayo hapo, na yeye ndiye aliye tumia nguvu zake ku mshawishi muuzaji,
Biashara ika fanyika na nika lipa na dalali nika mpa pesa yake tena kwa siri, wote wali furahi kila mtu kwa wakati wake,

Hadi leo hii jamaa ana niamini sana, jambo la biashara au lolote ndani ya uwezo wake ana nisaidia
 
Habari wanaJF,

Ni jioni nyingine tena nakuja hapa kumalizia siku hii. Nikiwa hapa, nilipiga picha ya kumbuukumbu za maisha ya hapo nyuma. Nikagundua cycles fulani zinazojirudia rudia. Na cycle (mzunguko) unapoisha, huna budi kuanza tena.

Mwanzo huwa ni mgumu. Maisha sio rahisi baada ya kupoteza vyote. Lakini if this is your case, endelea kusoma. Kuna kitu fulani nimeakuandalia kukutia moyo unapokabiliana na wiki hii mpya.

Nakuletea "the 3Ts You Must Know if You're Starting from Scratch" (Vitu 3 vya kuvifahamu endapo utakuwa unaanza upya).

1. Muda (Time)


Muda sio tu masaa 24—ni namna unavyoutumia. Utahitaji muda wa kujifunza, wa kufikia watu, wa kutoa huduma, na wa kujenga kitu ambacho kitabadilisha maisha yako na ya jamii yako. Utahitaji muda wa kuvumilia ukimya, kusubiri dalili za mvua, na kuendelea hata pale juhudi zako zinapoonekana kugonga mwamba.

Fahamu kuwa Mohammed Dewji (Mo) hakurithi utajiri mkubwa kama wengi wanavyodhani. Alianza na biashara ya familia iliyokuwa ndogo, lakini alitumia muda mwingi kujifunza, kupanua mtandao wake, na kuweka mikakati ya muda mrefu. Leo, anajulikana kama mmoja wa wafanyabiashara wakubwa Afrika (na anaongoza Afrika Mashariki, kwa mujibu wa Forbes List 2024). Lakini ilikuwa ni safari ya muda mrefu—yenye kazi kwelikweli.

"Muda ni mtaji wa maskini mwenye ndoto kubwa."

2. Kipaji (Talent)


Kila mtu ana kitu kimoja anachokifanya vizuri zaidi ya 90% ya watu wanaomzunguka. Hicho ndicho silaha yako. Kitafute. Kikuze. Kikamilishe. Kama hujui talanta yako, waulize wanaokufahamu. Halafu jifunze kitu kipya kinachohusiana na talanta/kipaji chako kila siku, hata kama ni kwa dakika 15 tu. Kipaji hukua. Baada ya mwaka mmoja utakuwa mbele ya asilimia 90 ya watu.

Angalia Nandy—aliyekulia katika mazingira ya kawaida mkoani Moshi. Alijua kuwa ana kipaji cha kuimba, akakikuza kupitia mashindano kama Tecno Own the Stage. Alijitahidi, akaendelea, na leo ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa Afrika Mashariki. Kipaji kilichofanyiwa kazi kiliweka historia. Konde Boy, Joel Nanauka na wengine kama hao ni mifano ya kuichunguza vizuri.

"Kipaji ni zawadi; lakini mafanikio ni kazi."

3. Uaminifu (Trust)

Unapokuwa huna kitu, uaminifu wako ndiyo mtaji wako wa kwanza. Ukiukosa, unaharibu msingi wa kila kitu. Ukikopa, lipa kwa wakati. Ukipewa nafasi, shine. Ukiaminiwa na mtu, usiache doa. Uaminifu unafungua milango ambayo hata pesa haiwezi kufungua.

Wasanii wengi waliofanikiwa walipiga mbio kwa mgongo wa mtu mwingine. Ambaye alikuwa na watu, na access, na platform. Rais Samia hangekuwepo kama mwamba hangemwona na kumpa nafasi. Christiano Ronaldo (CR7) alishine kwa sababu ya rafiki yake aliyemwamini na kumpasia mpira akafunga, na kupata nafasi kujiunga na Lisbon Footbal academy. Trust, my friend, is the currency of starters.

"Uaminifu hujengwa na matendo, si maneno."

Endapo umelazimika kuanza na hakuna kinachoenda, kama kila kitu ni kigumu—shikilia. Mwanzo ni mgumu. Ndivyo ilivyo. Lakini mchakato huo unakutengeneza kuwa mtu ambaye usingekuwa endapo changamoto hazingekuwepo.

Signed,
Amba Jnr.
Unasema mo akurithi utajili mkubwa?? Broo dola milioni 20 hivi unaionaje kwani???............ndogo eehh??
 
Habari wanaJF,

Ni jioni nyingine tena nakuja hapa kumalizia siku hii. Nikiwa hapa, nilipiga picha ya kumbuukumbu za maisha ya hapo nyuma. Nikagundua cycles fulani zinazojirudia rudia. Na cycle (mzunguko) unapoisha, huna budi kuanza tena.

Mwanzo huwa ni mgumu. Maisha sio rahisi baada ya kupoteza vyote. Lakini if this is your case, endelea kusoma. Kuna kitu fulani nimeakuandalia kukutia moyo unapokabiliana na wiki hii mpya.

Nakuletea "the 3Ts You Must Know if You're Starting from Scratch" (Vitu 3 vya kuvifahamu endapo utakuwa unaanza upya).

1. Muda (Time)


Muda sio tu masaa 24—ni namna unavyoutumia. Utahitaji muda wa kujifunza, wa kufikia watu, wa kutoa huduma, na wa kujenga kitu ambacho kitabadilisha maisha yako na ya jamii yako. Utahitaji muda wa kuvumilia ukimya, kusubiri dalili za mvua, na kuendelea hata pale juhudi zako zinapoonekana kugonga mwamba.

Fahamu kuwa Mohammed Dewji (Mo) hakurithi utajiri mkubwa kama wengi wanavyodhani. Alianza na biashara ya familia iliyokuwa ndogo, lakini alitumia muda mwingi kujifunza, kupanua mtandao wake, na kuweka mikakati ya muda mrefu. Leo, anajulikana kama mmoja wa wafanyabiashara wakubwa Afrika (na anaongoza Afrika Mashariki, kwa mujibu wa Forbes List 2024). Lakini ilikuwa ni safari ya muda mrefu—yenye kazi kwelikweli.

"Muda ni mtaji wa maskini mwenye ndoto kubwa."

2. Kipaji (Talent)


Kila mtu ana kitu kimoja anachokifanya vizuri zaidi ya 90% ya watu wanaomzunguka. Hicho ndicho silaha yako. Kitafute. Kikuze. Kikamilishe. Kama hujui talanta yako, waulize wanaokufahamu. Halafu jifunze kitu kipya kinachohusiana na talanta/kipaji chako kila siku, hata kama ni kwa dakika 15 tu. Kipaji hukua. Baada ya mwaka mmoja utakuwa mbele ya asilimia 90 ya watu.

Angalia Nandy—aliyekulia katika mazingira ya kawaida mkoani Moshi. Alijua kuwa ana kipaji cha kuimba, akakikuza kupitia mashindano kama Tecno Own the Stage. Alijitahidi, akaendelea, na leo ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa Afrika Mashariki. Kipaji kilichofanyiwa kazi kiliweka historia. Konde Boy, Joel Nanauka na wengine kama hao ni mifano ya kuichunguza vizuri.

"Kipaji ni zawadi; lakini mafanikio ni kazi."

3. Uaminifu (Trust)

Unapokuwa huna kitu, uaminifu wako ndiyo mtaji wako wa kwanza. Ukiukosa, unaharibu msingi wa kila kitu. Ukikopa, lipa kwa wakati. Ukipewa nafasi, shine. Ukiaminiwa na mtu, usiache doa. Uaminifu unafungua milango ambayo hata pesa haiwezi kufungua.

Wasanii wengi waliofanikiwa walipiga mbio kwa mgongo wa mtu mwingine. Ambaye alikuwa na watu, na access, na platform. Rais Samia hangekuwepo kama mwamba hangemwona na kumpa nafasi. Christiano Ronaldo (CR7) alishine kwa sababu ya rafiki yake aliyemwamini na kumpasia mpira akafunga, na kupata nafasi kujiunga na Lisbon Footbal academy. Trust, my friend, is the currency of starters.

"Uaminifu hujengwa na matendo, si maneno."

Endapo umelazimika kuanza na hakuna kinachoenda, kama kila kitu ni kigumu—shikilia. Mwanzo ni mgumu. Ndivyo ilivyo. Lakini mchakato huo unakutengeneza kuwa mtu ambaye usingekuwa endapo changamoto hazingekuwepo.

Signed,
Amba Jnr.
1744694251520.png
 
Kitu kikubwa na cha umuhimu ni uwezo wa kutambua fursa na kuzifanyia kazi hayo mengine hayana umihimu sana, kuna watu wana kipaji na waaminifu na wana uvimilivu huko mtaani na wapo pale pale
Uaminifu unakupa bingo any time,
Unaweza uka pewa mali kauli yaani kupewa mzigo ukauze kisha upeleke pesa ya mzigo huku wewe ukilamba faida ,

Ama hata mtu kukupa kabisa pesa kwa lengo ukisha uza umludishie pesa yake,
Hizi ni faida za uaminifu mkuu,
 
Unasema mo akurithi utajili mkubwa?? Broo dola milioni 20 hivi unaionaje kwani???............ndogo eehh??
Kwako Dola 20m ni hela kubwa, lakini sasa hivi anaskuma zaidi ya $1.5B. Yaani amekuwa zaidi ya mara 70. We huoni udogo hapo? Ama umeona 20m ukahaha
 
Kitu kikubwa na cha umuhimu ni uwezo wa kutambua fursa na kuzifanyia kazi hayo mengine hayana umihimu sana, kuna watu wana kipaji na waaminifu na wana uvimilivu huko mtaani na wapo pale pale
Hivyo vitu vitatu ni kama pedo ya baiskeli na tairi zake mbili. Vyote vinaendana.
 
Kwako Dola 20m ni hela kubwa, lakini sasa hivi anaskuma zaidi ya $1.5B. Yaani amekuwa zaidi ya mara 70. We huoni udogo hapo? Ama umeona 20m ukahaha
Swali kwako pia..........naomba unitajie kwenye ukoo wenu wote nani anayo hiyo pesa ambayo sio kubwa kwako???.........au basi jumlisha wote ukoo wenu na ukoo wa mke wako wote kwa pamoja mnaweza kuichanga hiyo ndogo dola milioni 20............???? Jibu utalipost kwa faida yako
 
Back
Top Bottom