Mwanza City: The Photo Gallery

Zipelekwe stendi ya kisesa
Stand ya Kisesa ?

  • Ilemela wanataka pesa.
  • Stand ya Kisesa ipo ipo tu, nadhani Magu wanasita kuwekeza pale kutukana na stori za Wilaya mpya ya Kisesa.

Ingawa nadhani ingesaidia kuchangamsha pale, maana Kuna daladala huwa zinaenda pale utafikiri wamelazimishwa, nyingi zinageuzia stand ya zamani hapo Round about ya Usagara.
 
Umetumia facts na logic kuwasilisha Hoja yako
 
Waweke stendi ndogo pembeni kam nyamagana wanavyotaka kufanya pale nyabulogoya, kiukweli hiyo stendi ni ndogo asee.
Of course, ni wazo zuri hasa kama wakijenga stand ya daladala ikawa pamoja na hizo coaster. Ila isiwe pale nje ya stand wanaposhushia daladala wanapotaka kuweka pelvings
 
Ndugu nimetoa mawazo yangu kwa sababu ya hoja kwamba stendi imejaa.
Pili gari nyingi zinaondoka asubuhi, mpaka hiyo gari ya Musoma ifike mza gari nyingi ziliisha ondoka na stendi iko tupu kwa kiwango Kikubwa tu.
 
Hata pakikaa tupu kuna shida gani
 
Hii sio changamoto, mimi naona ndio vizuri ili magari mabovu yaondoke menyewe.
Hili sio jambo jipya kwa tuliokuwa zamani kidogo mtakumbuka njia ya pasiansi ilivyokuwa na express nzuri zaidi na zilikuwa na mpaka burudani ya video ndani, yaani watu walikuwa wanachungulia ndani ndio wapande.
Samahani kutumia neno express, ni neno lilokuwa linatumika mza, dar walitumia daladala, Arusha ni vifodi
 
Kwanza mwanza ni Moja ya miji yenye daladala nzuri..nimekaa dodoma ,daladala za kule vyuma chakavu vyenye injini .
.hasa ruti ya st gema ,na mnada Mpya ,,,...
 
Humu nilishagundua kuna watu huwa wazuri kwa imagination kuliko uhalisia.
Halafu wanadaka sana maneno ya mitaani kuliko yale ya kweli.
 
Dodoma ni mji wenye daladala mbovu nyingi ...uzuri wa kule makonda wake ni wastaarabu Hadi mia mbili unapanda ..makonda wa mwanza ni wahuni sana na wakorofi
Hiyo kuchukua 200 ni ustaarabu au wateja ni shida?
 
Hiyo kuchukua 200 ni ustaarabu au wateja ni shida?
Vyote pia vinachangia ...Kwa sababu ruti nyingi zinategemea wanafunzi wa vyuo . Wanafunzi wanapofunga vyuo Hali ya abiria inakuwaga ndogo mjini
 
Majengo yote ya Nyanza yamepigwa nembo ya NHC, sijui kwanini?
 
Niliiipiga kwa haraka haraka nilikua jengo la NSSF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ