Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,462
- 21,334
Na Salim Said
KAMPENI za kuwania Ubunge Jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam zimeanza kwa kasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga kumwaga fulana na vitambaa vyenye picha yake kwa wanachama wa chama hicho wakati akisimikwa kuwa Kamada wa Umoja wa Vijana wa CCM wa Kata.
Mwangunga ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na mbunge wa kuteuliwa, ni mmoja kati ya vigogo wa CCM wanaotarajia kugombea Jimbo hilo la Ubungo lenye upinzani mkali ndani na nje ya chama chake.
Hali hiyo inatokea wakati CCM wala Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), hazijatangaza kuanza kwa kampeni za uchaguzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.
Diwani huyo wa Ubungo, William Masanja aliitisha mkutano huo juzi, kwa ajili ya kumsimika Mwangunga kuwa Kamanda wa Vijana wa CCM kata hiyo, huku akiutelekeza uongozi wa chama na wa vijana katika kata ambao ndio walengwa.
Shamra shamra za hafla hiyo zilipambwa na maandamano ya vijana waliovaa fulana na vitambaa vyenye picha ya Mwanguna na kusindikizwa na kikundi cha matarumbeta kutoka Tabata, yaliyoanza katika kituo cha Daladala cha Rombo hadi katika uwanja wa mpira wa Kibo Ubungo.
KAMPENI za kuwania Ubunge Jimbo la Ubungo jijini Dar es Salaam zimeanza kwa kasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga kumwaga fulana na vitambaa vyenye picha yake kwa wanachama wa chama hicho wakati akisimikwa kuwa Kamada wa Umoja wa Vijana wa CCM wa Kata.
Mwangunga ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na mbunge wa kuteuliwa, ni mmoja kati ya vigogo wa CCM wanaotarajia kugombea Jimbo hilo la Ubungo lenye upinzani mkali ndani na nje ya chama chake.
Hali hiyo inatokea wakati CCM wala Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), hazijatangaza kuanza kwa kampeni za uchaguzi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.
Diwani huyo wa Ubungo, William Masanja aliitisha mkutano huo juzi, kwa ajili ya kumsimika Mwangunga kuwa Kamanda wa Vijana wa CCM kata hiyo, huku akiutelekeza uongozi wa chama na wa vijana katika kata ambao ndio walengwa.
Shamra shamra za hafla hiyo zilipambwa na maandamano ya vijana waliovaa fulana na vitambaa vyenye picha ya Mwanguna na kusindikizwa na kikundi cha matarumbeta kutoka Tabata, yaliyoanza katika kituo cha Daladala cha Rombo hadi katika uwanja wa mpira wa Kibo Ubungo.