Mwanaume kimbia

Muuza simu used

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2017
Posts
4,393
Reaction score
7,101
Kukimbia pia ni moja kati ya mbinu za kivita pindi unapoona umezidiwa,unaweza ukajiona jasiri usikimbie ukabaki ukauwawa!

Nasema hivi mwanaume pindi unapoona uchumi wako umeyumba na ikifika kipindi huwezi tena kuendesha familia yaani inafika kipindi yaani huna mishe kabisa hadi unaamua kushinda nyumbani,maana hata ukitoka ni hola utaanza kuulizwa mbona umerudi mikono mitupu!

Ikifika hatua hii ni bora kukimbia na kwenda kusikojulikana kwa usalama wa afya yako maana sonona utayoipata kwa mkeo sio poa maana itafika kipindi ataanza kutoa papuchi kwa wajuba bila hofu yeyote na atakufanyia dharau kila aina!

Hii inaweza kupelekea kupata kesi ya mauaji uende jela maisha ama ujiue wewe mwenyewe ama uteketeze familia nzima!
Kwahiyo ni bora kukimbia mapema maana yajayo yanasikitisha!

All in all mwanaume tupambane sana kuhakikisha tunakuwa na uchumi imara kutunza familia zetu kinyume na hapo hakuna upendo wala heshima kwa Mwanamke
 
Huo ushauri wako mtoa mada wa kifa.la sana. Kuna shemeji yangu mmoja alikuwa anamkataza mkewe kufanya kazi yoyote, ila sasa hali ikiwa mbaya nyumbani anatafuta safari anaacha mkewe anahangaika na watoto. Baadae walikorofishana na mkewe akaenda kukaa kwenye nyumba yao nyingine, watoto wakawa wanapenda kwenda kule maana akiwa na hela kunakuwa na mapochopocho kama yote
ila siku akiishiwa hela anasafiri kimya kimya anawaacha watoto wanashangaana
 
Bora agongwe huku nashuhudia kuliko kuwakimbia wanangu,. Yaani. Niwatekeze!
Hapana aisee !bora hio fedheha nipate kikamilifu lakini sio kuwakimbia .

Ninachojua hakuna heshima yoyote, hakuna ufahari wowote hakuna furaha yoyote katika umaskini, hii ndio sala yangu kwa sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…