UTASHI
Senior Member
- Jan 19, 2013
- 135
- 56
Nilipata kusikia mazungumzo ya wanawake fulani,tena ni wasomi na wenye fedha zao,baadhi wakisema kua mwanaume bahili ni mzuri kua Mume kwa sababu hana tabia ya kuhonga honga wanawake/vimada na kiujumla hana wanawake wengi au hana kabisa,kwa vile wanawake wengi wanapenda hela nae hayuko tayari kutoa hela (pesa za familia zinatunzwa vizuri) na anaepuka magonjwa ya kuambukizwa (magonjwa ya zinaa),Na wengine wakisema hatoitunza familia vizuri,yaani atakua anabana kutoa hela kwa mambo muhimu ya kuendeleza familia.Hivi ndugu wana JF hii suala likoje,hivi hili suala la ubahili ni sehemu ya kuelezea ubaya au ubora wa MUME?