Mwanasheria mkuu wa serikali wapi busara zako?

Mwanasheria mkuu wa serikali wapi busara zako?

drmkumba

Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
52
Reaction score
1
Nimechoka sana na kauli iliyotolewa leo na mwanasheria mkuu wa serikali " eti kuwa na nywele sio kuwa na uwezo wa kufikiri".Kauli hii aliitoa leo bungeni pindi Mh.Tundu Lissu akiungwa mkono na Mh.Deo Filiponjombe na Mosesi Machali kutaka bunge lijadili kuhusu ajali ya meli ya Stargic.Baada ya hapo Mh.Tundu Lissu aliomba mwongozo wa spika kuhusu kauli hiyo lakini alichinjiwa baharini na Mh.Ndugai kwa madai ya kwamba hoja yake haikuungwa mkono!
 
Werema hampendi Lissu na jinsi Werema akili yake ilivyo ndogo ukute anafikiri Lissu ataichukua kazi yake ndio maana anamkosoa kila mara kwa siku ya leo ingekuwa vizuri kama wangekubali hoja ya Lissu ili tuweze jua nini kilitokea je hao TMA walikuwa hawajui hali ya hewa ilivyokuwa?
 
Kwa akili ya Werema huwa anamwangalia mtu na sio hoja, lakini kiti (mwanasheria mkuu)anachokalia kinataka kuangalia hoja, hivi kwa mantiki hiyo Werema anapishana na kiti chake anajitumikia yeye mwenyewe matakwa ya nafsi yake huku akila posho ya mwanasheria mkuu. Huu ni sawa na wizi.
Ndungai naye kama kawaida yake anamwangalia Lisu kama CHADEMA na anajiona yeye kama CCM. Lakini kiti anachokalia ni cha Bunge Tukufu la Jamhuri ya Tanzania. Nywele za Ndungai na Werema zinaonyesha jinsi wanavyofikiri tofauti na wanvyopaswa kufikiri ingawa wote wawili wana nywele.
Waingereza wana usemi wanasema 'Self qualification is no qualification' ikimaanisha sifa ya kujipa wewe mwenyewe haina thamani. Sasa tuwaangalie hawa watu watatu: Lisu, Ndungai na Werema, nani hajui kufikiri japokuwa anazo nywele? Nipeni jibu wana JF wekeni na supportings zenu bila biasness
 
Nimechoka sana na kauli iliyotolewa leo na mwanasheria mkuu wa serikali " eti kuwa na nywele sio kuwa na uwezo wa kufikiri".Kauli hii aliitoa leo bungeni pindi Mh.Tundu Lissu akiungwa mkono na Mh.Deo Filiponjombe na Mosesi Machali kutaka bunge lijadili kuhusu ajali ya meli ya Stargic.Baada ya hapo Mh.Tundu Lissu aliomba mwongozo wa spika kuhusu kauli hiyo lakini alichinjiwa baharini na Mh.Ndugai kwa madai ya kwamba hoja yake haikuungwa mkono!
Saa ya ukombozi inakaribia
 
warema sijui hata hiyo kazi ya ujaji alikuwa naifanyaje.... nina imani aliyoyasema Lisu kuhusiana na uteuzi wa majaji yana ukweli
 
Nimechoka sana na kauli iliyotolewa leo na mwanasheria mkuu wa serikali " eti kuwa na nywele sio kuwa na uwezo wa kufikiri".Kauli hii aliitoa leo bungeni pindi Mh.Tundu Lissu akiungwa mkono na Mh.Deo Filiponjombe na Mosesi Machali kutaka bunge lijadili kuhusu ajali ya meli ya Stargic.Baada ya hapo Mh.Tundu Lissu aliomba mwongozo wa spika kuhusu kauli hiyo lakini alichinjiwa baharini na Mh.Ndugai kwa madai ya kwamba hoja yake haikuungwa mkono!

AG Werema amedhihirisha kuwa ni kilaza wa kutupwa!!

Tunaomba CV yake hapa ukumbini ili tumjadili. HAIWEZEKANI HATA KIDOGO WEREMA AONGEE UTUMBO KAMA HUU BUNGENI! JE,INA MAANA WEREMA HAIJUI ILE METHALI INAYOSEMA,
''AKILI NI NYWELE KILA MTU ANA ZAKE????

Nashindwa kuoanisha maneno ya Werema na hiyo methali maarufu ambayo hata mtoto wa darasa la 1 anaifahamu. Werema ni janga la Kitaifa ndani ya Bunge.
 
Back
Top Bottom