Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,198
- 162,731
Kwa mujibu wa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu,Mwanasheria Mkuu wa Serikali si mshauri wa Bunge bali ni mshauri wa serikali na kwamba Bunge lina mshauri wake wa maswala hayo ya kisheria.
Kauli hiyo mh.Lissu aliitoa bungeni na hata Mwanasheri Mkuu mwenye hakuwahi kuipinga kauli hii kwa namna yoyote ile jambo linalothibitisha kuwa mh.Lissu alikuwa sahihi kabisa.
Lakini je,kiuhalisia,mwanasheria huyu awapo bungeni,ni kweli hutoa ushauri kwa serikali tu na si kwa bunge zima?Na je si kweli kuwa huyu mwanasheria hupewa nafasi ya kuongea ndani ya bunge pengine kuliko hata wabunge wenyewe?
Alafu mwanasheria huyu anaposimama bungeni na kuchangia huwa ana tofauti gani na wabunge zaidi ya kutumia nafasi yake vibaya kutaka kuwaburuza wabunge na kuibeba serikali?
Kama kigezo ni kuwa mwanasheria mkuu wa serikali na timu yake ndio huandaa miswaada hiyo kabla ya kuileta bungeni na hivyo anapaswa kuwepo Bungeni ili kutoa ufafanuzi pale itapohitajika,mbona basi dhamira au nia njema kama hiyo haikutumika kwa aliekuwa mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Katiba na wajumbe wake kwa kuruhusiwa kuingia katika Bunge Maalumu la Katiba?
Mh.Lissu alisema Bunge lina mshauri wake wa mambo ya kisheria,kama ni hivyo,ni kwanini mwanasheria huyu wa Bunge nae asiruhusiwe kuingia ndani ya Bunge ili nae aweze kuwashauri wabunge wawapo bungeni.
Mimi si mwanasheria,lakini najiuliza kama mwanasheria/mshauri wa bunge wa mambo ya kisheria haingii bungeni,kwanini basi na huyu mwanasheria mkuu wa serikali nae asipigwe "stop" kuingia bungeni na abaki kuishauri serikali nje ya bunge tu?
Je,huu utaratibu huu wa mwanasheria mkuu wa serikali kuingia Bungeni uko duniani kote?Kama kuna nchi hazina utaratibu huu,naamini hata sisi hatuna budi kuiga utaratibu huu kwani huyu mwanasheria wetu anaonekana kutumika kisiasa zaidi awapo ndani ya Bunge.
Kauli hiyo mh.Lissu aliitoa bungeni na hata Mwanasheri Mkuu mwenye hakuwahi kuipinga kauli hii kwa namna yoyote ile jambo linalothibitisha kuwa mh.Lissu alikuwa sahihi kabisa.
Lakini je,kiuhalisia,mwanasheria huyu awapo bungeni,ni kweli hutoa ushauri kwa serikali tu na si kwa bunge zima?Na je si kweli kuwa huyu mwanasheria hupewa nafasi ya kuongea ndani ya bunge pengine kuliko hata wabunge wenyewe?
Alafu mwanasheria huyu anaposimama bungeni na kuchangia huwa ana tofauti gani na wabunge zaidi ya kutumia nafasi yake vibaya kutaka kuwaburuza wabunge na kuibeba serikali?
Kama kigezo ni kuwa mwanasheria mkuu wa serikali na timu yake ndio huandaa miswaada hiyo kabla ya kuileta bungeni na hivyo anapaswa kuwepo Bungeni ili kutoa ufafanuzi pale itapohitajika,mbona basi dhamira au nia njema kama hiyo haikutumika kwa aliekuwa mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Katiba na wajumbe wake kwa kuruhusiwa kuingia katika Bunge Maalumu la Katiba?
Mh.Lissu alisema Bunge lina mshauri wake wa mambo ya kisheria,kama ni hivyo,ni kwanini mwanasheria huyu wa Bunge nae asiruhusiwe kuingia ndani ya Bunge ili nae aweze kuwashauri wabunge wawapo bungeni.
Mimi si mwanasheria,lakini najiuliza kama mwanasheria/mshauri wa bunge wa mambo ya kisheria haingii bungeni,kwanini basi na huyu mwanasheria mkuu wa serikali nae asipigwe "stop" kuingia bungeni na abaki kuishauri serikali nje ya bunge tu?
Je,huu utaratibu huu wa mwanasheria mkuu wa serikali kuingia Bungeni uko duniani kote?Kama kuna nchi hazina utaratibu huu,naamini hata sisi hatuna budi kuiga utaratibu huu kwani huyu mwanasheria wetu anaonekana kutumika kisiasa zaidi awapo ndani ya Bunge.