Mwanangu "nawa uso" Obama anakuja!!!

Mwanangu "nawa uso" Obama anakuja!!!

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2007
Posts
4,189
Reaction score
3,548
Kumekuwa na tabia ambayo serikali imekuwa ikifanya jambo ambalo limetuathiri sisi wananchi na hakika kama hatutabadilika basi usafi hautakuja kuwa utamaduni wetu. Kuna hii desturi ya kufanya usafi wa uhakika pindi kunapokuwa na ziara za viongozi wakuu. Nadhani kwa mrundikano wa "Perfume zetu huko mitaani" serikali hutumia kiasi kikubwa sana cha fedha kuondosha "lumbesa za taka taka mitaani.

Ili kutufunza tabia njema sisi wananchi wazazi wetu walitakiwa kutuhimiza kufanya usafi mwili mzima tangu tukiwa wadogo lakini siyo hili zoezi la kutuhimiza "kunawa uso Obama anakuja" Ikiwa Obama huyu angeamua yeye binafsi kuitembelea Dar es Salaam sehemu yoyote hakika angegundua kwamba kumbe tumenawa uso pekee bali makwapa yetu yana uoto asilia.

CCM Oyeeeee!!!!
 
that means that we are living in disguise.............we dont have what we can call our real life, our culture is destructed.
 
Zamani kwa tuliosoma shule za Vijijini siku wakija wakaguzi wa elimu lazima mkaguliwe masikio, kucha na kutakiwa kunyoa nywele kabla ya siku ya ukaguzi. Mkiwa mnasubiri siku ya ukaguzi kila eneo utaona moshi wa takataka zinazochomwa ukifuka ili mkaguzi akifika shule ionekane clean. Hivi kumbe hako katabia bado kako? Yaani hapa tunasanifika tu kwani balozi na Maafisa mbalimbali wa Marekani hupita hiyo mitaaa na mauchafu yake eti siku ya OBAMA wanaikuta safi; ujinga na unafiki mtupu,
 
Ameulizwa Mkuu wa mkoa hilo swali leo akaishia kujikanyaga.
 
Umesahau barabara ya Sam Nujoma kupandwa PALMS kubwa (kwa umri) kwa ajili ya wageni waliokutana Mlimani City na baada ya muda zikajifia na barabara kurudia hali yake ya kawaida. Sijui nani alitoa fedha hizo lakini itoshe tu kusema kwamba hatuna viongozi wenye upeo, ni abrakadabra tu kila uchao. Halafu wakiitwa wapumbavu wanalalamika, kumbe waitweje?
 
Baba mimi sinawi uso kuondoa matongotongo! Mbona mgeni mwenyewe anajua kuwa sisi ni Matonya? Tena akija nitamwomba pesa za kununulia bunduki,risasi,mabomu na maji ya kuwasha kwa sababu watoto wa jirani wanataka kutuzidi akili na kuichukua ofisi yetu ya OMBA OMBA COMPANY LIMITED.
 
Back
Top Bottom