MWANAMUME aliyening'inia kwenye helikopta, amtaka Odinga amsaidie aachiliwe na polisi na ampe kazi

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,267
e15cf37b47a22dead0d493851402a396.jpg
Mwanamume aliyening'inia kwenye helikopta iliyombeba kiongozi wa CORD Raila Odinga Alhamisi, katika Kaunti ya Meru amemtaka Bw Raila Odinga amsaidie aachiliwe na polisi na ampe kazi

Akiongea na wanahabari kituo cha polisi cha Maua anakozuiliwa, Julias Rigo Mwithali kutoka Kangeta kaunti ndogo ya Igembe Kati, alisema yeye ni mfuasi sugu wa Bw Odinga na alining'inia katika helikopta yake ili ampeleke nyumbani kwake na ampe kazi
0612ed9249048f6a6e170328617019f5.jpg
"Natoka katika familia yenye umaskini mwingi na nilitaka kuhepa ufukara na kwenda na 'baba", Bw Mwithali aliwaambia wanahabari

Jamaa huyo mwenye umri wa miaka 28 ambaye aliachia masomo yake katika darasa la nne alisema aliruka kutoka katika helikopta hiyo katika shule ya msingi ya Athimba, Igembe Kusini na kuchukua boda boda kurudi nyumbani

Kamanda wa polisi Meru, Bw Nelson Taliti alithibitisha kukamatwa kwa Bw Rigo, baada ya safari hiyo ya hatari, Bw Taliti alieleza kuwa Mwanamume huyo alishukishwa katika shule ya msingi ya Athimba baada ya Rubani kutua ghafla

Mwanamume huyo alishuka akiwa salama bila majeraha yoyote baada ya kusafiri kwa zaidi ya kilometa 15 kutoka uwanja wa Maili Tatu ambapo helikopta hiyo ilipaa

Bw. Odinga alikuwa amezuru eneo hilo kuhimiza watu wajitokeze kusajiliwa kama wapiga kura

Rubani aliposikia nduru kutoka kwa umati wa watu alijaribu kwenda taratibu ili ampatie nafasi ya kushuka lakini Mwanamume huyo aliendelea kushikilia helikopta huku akiwapungia watu mkono

Wakazi walisema Bw Rigo alikuwa ameapa kuandamana na Bw Odinga hadi Nairobi kwa kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kupata nafasi ya kupanda helikopta

"Alikuwa akisema anataka kupanda helikopta kwa mara ya kwanza na kwamba lazima iwe ya Raila Odinga", alieleza mkazi Bw John Mwiti

Wenyeji waliwashtumu polisi kwa kuzembea kazini wakisema kuwa Mwanamume huyo angeweza kuzuiwa kupanda ikiwa maafisa wangekuwa macho

Mwaka 2016, Saleh Wanjala ambaye alikuja kufahamika maarufu kama 'James Bond wa Bungoma' alining'inia kwenye helikopta iliyokuwa imeubeba mwili wa Mfanyabiashara aliyeuawa Jacob Juma katika Kaunti ya Bungoma. Alishtakiwa kwa kuhatarisha maisha yake.
 
Back
Top Bottom