stanslausk
New Member
- Feb 9, 2012
- 4
- 7
Nionavyo mimi mwanamke mwolewaji anasifa zifuatazo. (zingatia: mapenzi hayana formula only use this as a rough guide).
- Huruhusu mapenzi yawe wazi.hivyo mara nyingi atakutambulisha kwa ngudu na marafiki zake.
- Hapendi kukuingiza gharama. Daima atakushauri kuhusu matumizi mazuri ya pesa. Si mpenda makuu na mara nyingi kabla hajakutolea shida inayohitaji fedha nyingi, kwanza atazingatia umuhimu/ulazima wa hiyo shida sambamba na uwezo wako.
- Ni mkweli na muwazi. Akipata matatizo au changamoto mbalimbali atapenda kukushirikisha ili umsaidie hata kimawazo. Atakueleza mambo mengi kuhusu familia yake. Atakueleza hata mambo yake binafsi ambayo ni siri na labda hajawahi kumweleleza mtu mwingine.
- Ni mshauri mzuri. Atapenda kukushauri ufanye nini ili ufanikiwe. Yuko tayari kuishi kwa kujibana ili kuku-support utekeleze mambo Fulani ya kimaendeleo.
- Ni msaidizi. Yuko tayari kujitoa hata kifedha kukusaidia. Ni kama anakipato atapenda kuchangia gharama ktk mambo mbalimbali kwa mfano mnapoenda viwanja kuspend
- Ni mwaminifu na mwenye upendo wa kweli.
- Atakuheshimu na kukuthamini. Mapungufu yako hatayatangaza kwa watu
- Atawapenda na kuwaheshimu ndugu zako.
- Atapenda kuwa karibu na wewe.atawasiliana nawe mara kwa mara hasa mnapokuwa mbali.
- Ni msikivu.yu tayari kukosolewa. Huwa tayari kubadilika ili muendane.mathalani, ataepuka kurudia kufanya mambo ambayo huyapendi. Yoku makini katika kauli zake. Kwa mfano wanawake wasio serious na mahusiano pindi mnapolumbana haraka hurukia kauli eg: kama vipi tuachane: unaweza ku-quit kama unaona sikufai.
- Hupenda suluhu pale mnapotofautiana. Mwepesi wa kukiri kosa na kuomba msamaha pale anapokukosea.
- Mvumilivu. Atakuvumilia pamoja na mapungufu uliyonayo.
- Anaweza kuanza kuassume responsibilities za mke hata wakati bado hamjaoana (chonde simaanishi tendo la ndoa).Mfano anapokutembelea kwako anaweza kukupikia,kukufulia,kukuchagulia nguo za kuvaa n.k