Mwanamke mwenye mtoto!

M.E.M.A

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2013
Posts
1,373
Reaction score
472
Wakuu salaam

Husika na kichwa cha habari hapo juu, pasi na kutoa kisa kirefu naomba mnisaidie kwa kujibu swali hili: Kuna tatizo gani kuoa mwanamke aliyezaa na mwanaume mwingine, na huyo mwanaume hajafa,na mtoto pia yupo ila yupo kwa baba yake?

NB: Mwanamke anasema kwa mwanaume huyo hakuna future na sio mtu ambaye anaweza kuishi naye. Anafanya mpango wa kumchukua mwanae na ikishindikana basi atamuacha huko,akiwa mkubwa atatamtafuta.

Mpaka sasa watu wa upande wa baba wa mtoto hawataki mtoto achukuliwe.
 
^^
Mtoto wa jinsia gani ambae akikua atamfuata? Future ipi anayosemea? Pato lako la yule mwingne likoje?
Nisaidie majibu hapo
^^
 

Hakuna ubaya wowote uliopo kuoa mwanamke mwenye mtoto maadamu mnapendana.

Lakini mwenye mtoto ataendelea kugegeda mamatoto kama zamani.

Kama hiyo siyo shida kwako, basi unaweza kumuoa huyo mama mtoto.
 
Kisa chako hakijakamilika...

Hebu tuelezee sababu za hao wazazi kutengana, walifunga ndoa kabla au lah?
 
^^
Mtoto wa jinsia gani ambae akikua atamfuata? Future ipi anayosemea? Pato lako la yule mwingne likoje?
Nisaidie majibu hapo
^^

Mtoto ni jinsia ya kike miaka mitano. Future anayoisemea ni tofauti za kidini na mengineyo ambayo hayaelezeki. Kipato yule mwingine yupo juu kuliko mimi.
 
Inategemea na akili,msimamo na uwezo wa mwanamke kuchanganua mambo!!!!
Mwanaume pia ina mchango katika hilo sababu wewe ndio nguzo ya huyo mwanamke so ukikomaa na kama yeye ana dhamira juu yako mnaweza ishi! !!!!Ila changamoto zipo

Ila kama huyo mwanamke ana lengo tu la kutaka kumuonesha mzazi mwenzie kuwa "yeye bado wamo" hapo mkuu utaliwa!!!!!
 
Hakuna shida ilimladi mmependana unamuoa tu kilichopo yule aliezaa nae inabidi aheshimu maamuzi si tena aanze kutaka kukumbushia mambo fulani hapo ni kuonana wabaya tu.
 

itabidi na wewe uwe na mtoto wa nje ili kuhusu kuchapiwa iwe kitu cha kawaida tu..
 
Hakuna ubaya wowote uliopo kuoa mwanamke mwenye mtoto maadamu mnapendana.

Lakini mwenye mtoto ataendelea kugegeda mamatoto kama zamani.

Kama hiyo siyo shida kwako, basi unaweza kumuoa huyo mama mtoto.

Hawana uhusiano wa kimapenzi tena.
 
Kisa chako hakijakamilika...

Hebu tuelezee sababu za hao wazazi kutengana, walifunga ndoa kabla au lah?

Hawajawahi kufunga ndoa. Ni matokeo ya mgegedo wa adolescent.
 

Kwa mwanamke anasema hata kama sitamuoa au hatatokea mtu wa kumuoa basi atakaa hivyo hivyo kuliko kuishi na huyo baba wa mtoto.

Hizo changamoto ni zipi mkuu? Japo nyingine nimeanza kuziona mfano; mama na ndugu hawataki kusikia hiyo habari..kwa sababu tu ya huyo mtoto.
 
Ila kama huyo mwanamke ana lengo tu la kutaka kumuonesha mzazi mwenzie kuwa "yeye bado wamo" hapo mkuu utaliwa!!!!!

Hili jambo wanawake wengi hufanya mpwa hata wale ambao hawana watoto lakini walikuwa tu kwenye mahusiano na watu ambao mwishoni waliwatelekeza.
 
Hakuna shida ilimladi mmependana unamuoa tu kilichopo yule aliezaa nae inabidi aheshimu maamuzi si tena aanze kutaka kukumbushia mambo fulani hapo ni kuonana wabaya tu.

Kuna gazeti fulani nimeona jamaa anaomba ushauri. Yeye pia alioa mwanamke ambaye ana mtoto na jamaa mwingine. Na huwa anaaga anaenda kuchukua matumizi na harudi hadi kesho yake. Well kwa case yangu mtoto yupo kwa baba wa mtoto na hawataki achukuliwe na mama yake.
 
mh! ngoja lakini...wewe wasiwasi wako ni nini hasa?

Sina wasiwasi ila tu.. miluzi mingi humpoteza mbwa. Nampenda ananipendana...tunapendana.., tatizo baadhi ya ndugu na mama wanaona kuna siku ataniacha na kurudi kwa baba wa mtoto. Kitu ambacho kwa kwa tulivyoliongelea hilo swala na bibie ni kitu ambacho hakitatokea..japo OLESAIDIMU kaniasa nisijihakikishie vitu ambavyo havina uthibitisho kisayansi.

Pamoja na hayo tumepanga tuwe na simple function this coming june...na wengine wameanza kutangaza kutokuja.
 
Last edited by a moderator:
jitengenezee role model ya maisha yako binafsi kwakuwa, kila atakayekushauri kuhusu hilo atakushauri kutokana na uzoefu wake binafsi ambao unaweza kuwa na madhara makubwa mno, au usikusaidie kabisa
 
Jilipue tu, matatizo yanakuaga mengi hata kama si leo ni kesho, akishakuwa kama ni mtoto wa kiume anakuwa kama ndio mume wake kila kitu ushauri ni kwake
 
Mtoto ni jinsia ya kike miaka mitano. Future anayoisemea ni tofauti za kidini na mengineyo ambayo hayaelezeki. Kipato yule mwingine yupo juu kuliko mimi.

^^
Kama umempenda kupita kiasi, love is all about risk taking
^^
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…