SAFARI HURU
New Member
- Dec 3, 2020
- 1
- 1
1. Ni siku ya tatu leo.
Nipo hoi kitandani
Natweta sijitambui.
HAKIKA mwanamke ameniponya.๐ฆ
2. Tumbo limenitesa,
Tumbo limekatakata
Nimekwenda NENDA nenda rudi, mbio bila mshindani.๐๐พโโ๏ธ
3. Muziki mkali ulipigwa,
Huo bila ya nota,
Nikifumba macho
Kwa maumivu tele,
Lakini mwanamke dawa.
Mchana kutwa mbio
Mbio hazikukoma mbio.๐ผ
4. Mwanamke ni dawa kwa mengi,
Labda ni ndoto,
Ndoto ambayo ni tenzi. Na imetenda,
Ndoto yenye tiba
Tiba ya kuhuisha.๐ช๐ฟ
5. Nikwambie jambo,
Ni gumu kutekeleza,
Kwa njozi limefanyika,
Ipo kazi kulitimiza peupe, kwa njozi limetendeka,
Ni vigumu kujipangia njozi ya kuota
Kama upangavyo safari.๐ซ
6. Mwanamke huyu wa ndotoni,
Nililala na wanawake wawili mkekani,
Mmoja kulia na mmoja kushoto.
โ๏ธ
6. Wote hao nawafahamu,
Ni watumishi serikalini,
Ni wake za watu
Angalia usije ukasema ingawa nimeandikaโ๐ฟ
7. Kati yao mmoja ni mja mzito wa tumbo la kujifungua
Na mwingine sijui,
Mwanamke ni dawa
Amenitibu njozini.๐
8. Mjamzito akiwa mgongoni na mwingine tukila muwa wa kiutu uzima,
Kwa pigo moja la mshindo wa umsolopogazi
Sote tukijitambua kwa raha la kijasho.๐ฅ
9. Yapata saa 10:10 kuamka usiku wa njozi,
Wanawake siwaoni
Nikiwa Mzungu wa nne kitandani.๐
10. Nakumbuka tendo la mwisho
Kwa mwanamke dawa,
Bila kujali mke wa mtu tamu ya muwa,
Nikamwambia nakupenda tena,
Akatabasamu, meno meupe ingawa ni mweusi na mfupi.๐
11. Nikambusu paji la uso akanikumbatia kisha akaondoka.
Na wa mgongoni sikumuona kaishia wapi kweli, MWANAMKE dawa.๐น
12. Kuzinduka usingizini, mkato wa tumbo haupo,
Shuka limetapakaa
uji, huo uji sijui ulitokea wapi..!
Kumbe ndo kupona.๐๐ฟ
15. Ni usiku naandika
Njozi isinikimbie
Maono yasinitoroke
Nikwambie mwanamke dawa japo ni hatari kwa mke wa mtu.๐ฆ
16. Tumaini la kuiona siku mpya lipo,
Nilikata tamaa, kwa kuuma meno,
Ati nikizuia maumivu ya mkato wa tumbo la mchamchaka. Kumbe dawa ni mwanamke wa njozini. โค๏ธ
17. Nilijitahidi kula dozi majani,
Majani ya mpera juisi yake ikiwa na asali mbichi,
Kwa nusu kikombe kwa masaa kadhaa. Imeniletea na njozi ya uponyaji.
Ajabu..๐คท๐ฟโโ๏ธ
18. Namshukuru MAULANA kunitibu, kwa majani na
Wanawake kuhitimisha,
Iwapo ni jambo gumu kuwa na wake wawili kwa tendo moja kwa wake za watu๐ค๐ฟ
19. Hilo kwa WENGINE, lahitaji mipango,
Kwangu Mola kalitimiza kiajabu,
Amini mzimu wako, vya Wazungu
HAKIKA hivyo vinanyonga. Na wengi vimewameza๐บ
20. Kumbuka kuwa kila SHETANI ana mbuyu wake,
Kwa nini uabudu mzimu wa mwenzio..!
Mwanamke ni dawa. Ni tiba kwa kila namna. ๐ฟ๐๐ฝ
Ah...! Kumbe naota..โ๏ธ
Nipo hoi kitandani
Natweta sijitambui.
HAKIKA mwanamke ameniponya.๐ฆ
2. Tumbo limenitesa,
Tumbo limekatakata
Nimekwenda NENDA nenda rudi, mbio bila mshindani.๐๐พโโ๏ธ
3. Muziki mkali ulipigwa,
Huo bila ya nota,
Nikifumba macho
Kwa maumivu tele,
Lakini mwanamke dawa.
Mchana kutwa mbio
Mbio hazikukoma mbio.๐ผ
4. Mwanamke ni dawa kwa mengi,
Labda ni ndoto,
Ndoto ambayo ni tenzi. Na imetenda,
Ndoto yenye tiba
Tiba ya kuhuisha.๐ช๐ฟ
5. Nikwambie jambo,
Ni gumu kutekeleza,
Kwa njozi limefanyika,
Ipo kazi kulitimiza peupe, kwa njozi limetendeka,
Ni vigumu kujipangia njozi ya kuota
Kama upangavyo safari.๐ซ
6. Mwanamke huyu wa ndotoni,
Nililala na wanawake wawili mkekani,
Mmoja kulia na mmoja kushoto.
โ๏ธ
6. Wote hao nawafahamu,
Ni watumishi serikalini,
Ni wake za watu
Angalia usije ukasema ingawa nimeandikaโ๐ฟ
7. Kati yao mmoja ni mja mzito wa tumbo la kujifungua
Na mwingine sijui,
Mwanamke ni dawa
Amenitibu njozini.๐
8. Mjamzito akiwa mgongoni na mwingine tukila muwa wa kiutu uzima,
Kwa pigo moja la mshindo wa umsolopogazi
Sote tukijitambua kwa raha la kijasho.๐ฅ
9. Yapata saa 10:10 kuamka usiku wa njozi,
Wanawake siwaoni
Nikiwa Mzungu wa nne kitandani.๐
10. Nakumbuka tendo la mwisho
Kwa mwanamke dawa,
Bila kujali mke wa mtu tamu ya muwa,
Nikamwambia nakupenda tena,
Akatabasamu, meno meupe ingawa ni mweusi na mfupi.๐
11. Nikambusu paji la uso akanikumbatia kisha akaondoka.
Na wa mgongoni sikumuona kaishia wapi kweli, MWANAMKE dawa.๐น
12. Kuzinduka usingizini, mkato wa tumbo haupo,
Shuka limetapakaa
uji, huo uji sijui ulitokea wapi..!
Kumbe ndo kupona.๐๐ฟ
15. Ni usiku naandika
Njozi isinikimbie
Maono yasinitoroke
Nikwambie mwanamke dawa japo ni hatari kwa mke wa mtu.๐ฆ
16. Tumaini la kuiona siku mpya lipo,
Nilikata tamaa, kwa kuuma meno,
Ati nikizuia maumivu ya mkato wa tumbo la mchamchaka. Kumbe dawa ni mwanamke wa njozini. โค๏ธ
17. Nilijitahidi kula dozi majani,
Majani ya mpera juisi yake ikiwa na asali mbichi,
Kwa nusu kikombe kwa masaa kadhaa. Imeniletea na njozi ya uponyaji.
Ajabu..๐คท๐ฟโโ๏ธ
18. Namshukuru MAULANA kunitibu, kwa majani na
Wanawake kuhitimisha,
Iwapo ni jambo gumu kuwa na wake wawili kwa tendo moja kwa wake za watu๐ค๐ฟ
19. Hilo kwa WENGINE, lahitaji mipango,
Kwangu Mola kalitimiza kiajabu,
Amini mzimu wako, vya Wazungu
HAKIKA hivyo vinanyonga. Na wengi vimewameza๐บ
20. Kumbuka kuwa kila SHETANI ana mbuyu wake,
Kwa nini uabudu mzimu wa mwenzio..!
Mwanamke ni dawa. Ni tiba kwa kila namna. ๐ฟ๐๐ฝ
Ah...! Kumbe naota..โ๏ธ